Je, Wakumbuka?
Je, umethamini kusoma matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Basi, ona ikiwa waweza kujibu maswali yafuatayo:
▫ Kwa nini Wakristo wa mapema hawakusherehekea siku ya kuzaliwa kwa Yesu?
Kulingana na The World Book Encyclopedia, “Wakristo wa Mapema hawakusherehekea siku ya kuzaliwa kwa [Yesu] kwa sababu waliiona sherehe ya kuzaliwa kwa mtu yeyote kuwa desturi ya wapagani.”—12/15, ukurasa 4.
▫ Je, sala zielekezwe kwa Yesu?
La, kwa sababu sala ni namna ya ibada inayopewa Mungu Mweza Yote pekee. Kwa kuelekeza sala zetu zote kwa Yehova Mungu, tunaonyesha kwamba tumezingatia mwongozo wa Yesu wa kusali: “Baba yetu uliye mbinguni.” (Mathayo 6:9)—12/15, ukurasa 25.
▫ Kwa nini hukumu tofauti ilitolewa kwa ajili ya dhambi nzito ya Mfalme Daudi kwa kulinganishwa na dhambi za Anania na Safira? (2 Samweli 11:2-24; 12:1-14; Matendo 5:1-11)
Dhambi ya Mfalme Daudi ilikuwa kwa sababu ya udhaifu wa kimwili. Alipokabiliwa na lile alilokuwa amefanya, alitubu, na Yehova alimsamehe—ingawaje alilazimika kuishi na matokeo ya dhambi yake. Anania na Safira walitenda dhambi kwa njia ya kwamba walidanganya kwa unafiki, wakijaribu kufanyia hila kutaniko la Kikristo na hivyo ‘kufanya isivyo kweli kwa roho takatifu na kwa Mungu.’ (Matendo 5:3, 4) Hilo lilihakiki kuwa uthibitisho wa moyo mwovu, kwa hiyo walihukumiwa vikali zaidi.—1/1, kurasa 27, 28.
▫ Ni nini laweza kutusaidia tumtumikie Yehova kwa moyo wenye shangwe?
Twapaswa kukuza maoni mazuri na yenye uthamini ya baraka zetu na mapendeleo ya utumishi tuliyopewa na Mungu, na hatupaswi kamwe kusahau kwamba kwa kufuata Neno la Mungu, sisi tunampendeza.—1/15, kurasa 16, 17.
▫ Ni mambo gani mawili ambayo ni lazima tukumbuke ikiwa tutatoa kitia-moyo chenye matokeo?
Kwanza, fikiria kuhusu utakalosema ili kitia-moyo kiwe hususa. Pili, tafuta fursa ya kufikia mtu astahiliye sifa au ahitajiye kujengwa.—1/15, ukurasa 23.
▫ Kwa nini “umati mkubwa” una “matawi ya mitende mikononi mwao”? (Ufunuo 7:9, NW)
Kupungwa kwa matawi ya mitende kwaonyesha kwamba “umati mkubwa” hukaribisha kwa shangwe Ufalme wa Yehova na Mfalme wake mtiwa-mafuta, Yesu Kristo. (Ona Mambo ya Walawi 23:39, 40.)—2/1, ukurasa 17.
▫ Ni masomo gani yenye thamani yanayopatikana katika kitabu cha Ayubu?
Kitabu cha Ayubu chatuonyesha jinsi ya kushughulika na matatizo. Chaandaa vielelezo vyenye kutokeza vya jinsi mtu anayekabili majaribu apasavyo—na asivyopasa—kushauriwa. Isitoshe, ono la Ayubu mwenyewe laweza kutusaidia kuitikia kwa njia yenye usawaziko tunapojipata tumekumbwa na hali mbaya.—2/15, ukurasa 27.
▫ Miujiza ya Yesu yatufundisha nini?
Miujiza ya Yesu yamtukuza Mungu, ikiwekea Wakristo kigezo cha kumtukuza Mungu. (Warumi 15:6) Inatia moyo kufanya mema, kuonyesha ukarimu, na kuonyesha huruma.—3/1, ukurasa 8.
▫ Ni kusudi jipi linalotimizwa na kule kupitia kwa wazee maswali yaliyotayarishwa pamoja na waliojiweka wakfu karibuni?
Hilo lahakikisha kwamba kila atakaye kubatizwa aelewa kikamili mafundisho ya msingi ya Biblia na afahamu yale yanayohusika katika kuwa Shahidi wa Yehova.—3/1, ukurasa 13.
▫ Sala za Kibiblia zaweza kutunufaishaje?
Kwa kuchunguza kwa ukaribu sala za Kimaandiko, sisi twaweza kutambulisha zile zilizotolewa katika hali zinazofanana na zetu wenyewe. Kupata, kusoma, na kutafakari juu ya sala hizo kwaweza kusaidia kutajirisha uwasiliano wetu wenyewe na Yehova.—3/15, kurasa 3, 4.
▫ Hofu ya kimungu ni nini?
Hofu ya kimungu ni woga kuelekea Yehova, staha nyingi kuelekea yeye, pamoja na ogofyo lifaalo la kutompendeza. (Zaburi 89:7)—3/15, ukurasa 10.
▫ Ni nini njia tatu ambazo Biblia huonyesha kwamba sisi ni wenye thamani machoni pa Mungu?
Biblia hufundisha kwamba kila mmoja wetu ana thamani machoni pa Mungu (Luka 12:6, 7); huelewesha wazi yale ambayo Yehova huthamini ndani yetu (Malaki 3:16); na husimulia yale Yehova amefanya ili kuonyesha upendo wake kwetu. (Yohana 3:16)—4/1, kurasa 11, 12, 14.
▫ Kwa nini Waebrania 10:24, 25 ni zaidi ya kuwa amri tu kwamba Wakristo wakutane pamoja?
Maneno hayo ya Paulo yaweka kiwango kilichopuliziwa kimungu kwa ajili ya mikutano yote ya Kikristo—kwa kweli, kwa ajili ya pindi yoyote ile ambayo Wakristo hushiriki pamoja.—4/1, ukurasa 16.