Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 11/15 kur. 8-9
  • Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—New Zealand

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—New Zealand
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Habari Zinazolingana
  • 1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Mashahidi wa Yehova—Ripoti ya Kitabu-Mwaka 1994
    1994 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Kujenga Pamoja Duniani Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Katika New Zealand—Siku ya Kukumbukwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 11/15 kur. 8-9

Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—New Zealand

JE, VISIWA vinaweza kumsifu Yehova? Ndiyo, kulingana na Isaya 42:10: “Mwimbieni BWANA wimbo mpya, na sifa zake tokea mwisho wa dunia; . . . na visiwa, nao wakaao humo.” Visiwa vinavyofanyiza New Zealand kwa hakika humsifu Yehova. Pakiwa mahali pajulikanapo ulimwenguni kwa maziwa ya maji, viingilio vya bahari, milima mirefu, barafuto, bichi, misitu, na mandhari ya eneo lenye rutuba, New Zealand husema waziwazi juu ya ukuu na utukufu wa Muumba wa mbingu na dunia.

Tangu mwanzo wa karne hii, wakaaji wengi zaidi na zaidi wa New Zealand wameshiriki kumsifu Yehova kwa kumgeukia katika ibada safi na kushiriki na wengine habari njema ya Ufalme wa Mungu. Majuzi, Shahidi aliyekuwa amesikia jambo zuri lililoonwa kuhusu kutolea ushahidi watu wa ukoo aliamua kufanya jitihada na kutolea familia yake ushahidi. Akatolea washiriki kadhaa wa familia yake zawadi za nakala ya kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Matokeo yamekuwa nini kufikia sasa? Yeye aripoti kwamba dada mmoja na ndugu mmoja sasa wanajifunza Biblia, mpwa amebatizwa kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, na wengine sasa wana mwelekeo zaidi wa kukubali kweli ya Neno la Mungu. Bado ana shamba kubwa la kuhubiri; kando na wazazi wake, ana ndugu sita na dada tisa!

Yehova hupata sifa pia Mashahidi waunganishapo jitihada zao ili kujenga Majumba ya Ufalme. Kwa kielelezo, mwandikaji wa safu za magazeti Roy Perkins aliandika katika Opotiki News la Mei 17, 1994: “Nikiwa asiyeamini, nilivutiwa sana na kazi mbalimbali na jitihada za wafanyakazi wote wenye kujitoa watumiao wakati mwingi sana na jitihada nyingi sana katika mradi huo kwa ajili ya kumpenda Mungu wao.

“Katika saa hizi zote zilizotumiwa katika mwisho-juma sikuona au kusikia kamwe mabishano . . . Wanawake walikuwa juu ya ngazi wakifanya kazi kando ya wanaume wenzao, wakichonga, kuinua na kubeba vifaa vya ujenzi, yote hayo katika hali yenye starehe na yenye furaha.

“Na hakuna dakika moja iliyopotezwa huku mtu yeyote akivuta sigareti. Kwa watu hao wote wenye kufanya kazi zozote zile hewa ilikuwa safi ila kwa harufu za rangi na mavumbi ya mawe.”

Baraza la wazee la Kutaniko la Opotiki liliandika hivi: “Mradi wote umevutia sana watu wa mjini. Inaonekana kana kwamba kila mtu anazungumza juu yao. Mafunzo kadhaa ya Biblia yameanzishwa. Moja hasa ambalo tuliona kuwa lenye kusisimua sana ni mume na mke fulani wenye kufuata dini sana ambao kwa miaka mingi wameomba kwamba tusiwatembelee. Walikuja mahali pa ujenzi kila siku kisha mkutanoni. Baadaye mume alisema, ‘Naweza kuona nyinyi ni watu wa Mungu. Ndani, nimekuwa nikitamani maishani mwangu mwote kushirikiana na watu wa namna hii.’”

Mwaka uliofuata, mwandikaji wa safu ya gazeti la Otago Daily Times alisema yafuatayo kuhusu Jumba la Ufalme la kujengwa upesi katika Dunedin: “Ulikuwa utendaji wa kutazamisha, kielelezo chenye kutazamisha cha uchocheaji na kujitolea msaada.” Gazeti hilohilo lilisema: “Wakaaji wa jiji walitazama kwa mshangao huku jengo kubwa lililojengwa mbele za macho yao, na wengi ni lazima wawe wanafikiria ni mabadiliko gani mengine na miradi chanya inayoweza kutimizwa ikiwa kikundi kikubwa kama hicho cha wafanyakazi wa kujitolea na roho nyingi ya kushirikiana ingekuwapo. Jumba la Ufalme ni ishara ya kuonea fahari ya jitihada zenye maendeleo zinazopata matokeo.”

Kuhusu yale mamia mengi ya watu waliotembelea mahali pa ujenzi, mtu mmoja mashuhuri alionelea kwamba Mashahidi walikuwa wakijenga “makanisa” huku dini yake ikiyauza kwa sababu ya kupungua kwa washiriki. “Kama mngengoja miezi mingine kumi na miwili, mngalinunua letu moja,” akajasiria kusema. “Ni lazima tuliuze kwa sababu hatuwezi kulilipia. Lakini, bila shaka, nyinyi watu hamna makasisi wa kulipwa. . . . Halafu majengo yenu yanadumishwa kwa gharama ndogo, si majengo marefu yenye minara ambayo hayawezi kudumishwa.”

Kwa wazi, visiwa vinaweza kwelikweli kumsifu Mungu. Sifa za Yehova na ziendelee kusikiwa katika nchi hii maridadi ya Pasifiki—na ulimwenguni pote!

[Sanduku katika ukurasa wa 9]

HABARI ZA NCHI:

Mwaka wa Utumishi wa 1994

KILELE CHA WANAOTOA USHAHIDI: 12,867

UWIANO: Shahidi 1 kwa watu 271

HUDHURIO LA UKUMBUSHO: 24,436

WASTANI WA WAHUBIRI WALIO MAPAINIA: 1,386

WASTANI WA MAFUNZO YA BIBLIA: 7,519

IDADI YA WALIOBATIZWA: 568

IDADI YA MAKUTANIKO: 158

OFISI YA TAWI: MANUREWA

[Picha katika ukurasa wa9]

Mapainia wakiondoka kwenda shambani karibu 1930

[Picha katika ukurasa wa9]

Majengo ya tawi katika Manurewa

[Picha katika ukurasa wa9]

Kuhubiri ujumbe wa Ufalme katika Devonport, Auckland

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki