Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 12/15 uku. 30
  • Je, Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Utasimamaje Mbele ya Kiti cha Hukumu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Kuna Wakati Ujao Gani kwa Kondoo na Mbuzi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Linda Hisi Yako ya Uharaka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 12/15 uku. 30

Je, Wakumbuka?

Je, umeyafikiria kwa makini matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Huenda ukapendezwa kukumbuka yafuatayo:

◻ Mtu anapataje ‘kumwendea Yesu’ kwa kupatana na mwaliko wake kwenye Mathayo 11:28?

Yesu alisema: “Ikiwa yeyote ataka kunifuata, na ajikane mwenyewe na kuchukua mti wake wa mateso na kunifuata kwa kuendelea.” (Mathayo 16:24, NW) Hivyo, kumwendea Yesu kwadokeza kunyenyekeza mapenzi ya mtu mwenyewe ili kufanya yale ya Mungu na Kristo, akikubali mzigo fulani wa daraka, na akifanya hivyo kwa kuendelea.—8/15, ukurasa wa 17.

◻ Kwa nini ni “wachache” tu hupata ‘njia nyembamba iendayo uzimani’ ambayo Yesu alitaja kwenye Mathayo 7:13, 14?

Njia nyembamba ina mipaka ya sheria na kanuni za Mungu. Hivyo, hiyo yaweza kuvutia tu mtu anayetamani kwa unyoofu kupatanisha maisha yake na viwango vya Mungu. Ingawa inaonekana kama ina mipaka, ‘njia yenye kusongamana’ huweka mtu huru kwa kila jambo muhimu. Mipaka yayo imewekwa na “sheria kamilifu iliyo ya uhuru.” (Yakobo 1:25)—9/1, ukurasa wa 5.

◻ Ufahamu unaweza kusitawishwaje?

Ufahamu hauji kwa urahisi au wenyewe tu. Lakini kwa saburi, sala, bidii-nyendelevu, ushirika wenye hekima, funzo la Biblia na kutafakari juu yayo, na kwa kutegemea roho takatifu ya Yehova, ufahamu unaweza kusitawishwa.—9/1, ukurasa wa 21.

◻ Wivu wa kibinadamu unaweza kutumikaje kwa kusudi zuri?

Unaweza kumsukuma mtu alinde mpendwa wake kutokana na uvutano mbaya. Isitoshe, wanadamu wanaweza kwa kufaa kuonyesha wivu kwa ajili ya Yehova na ibada yake. (1 Wafalme 19:10)—9/15, kurasa za 8, 9.

◻ Ni nini kimaanishwacho na usemi upatikanao kwenye Mwanzo 50:23 kuhusu wajukuu wa Yusufu: “Walizaliwa magotini mwa Yusufu”?

Jambo hilo laweza kumaanisha tu kwamba Yusufu alitambua hawa watoto kuwa wa ukoo wake. Laweza pia kuonyesha kwamba alicheza nao kwa shauku nyingi, akiwachezesha kati ya magoti yake. Akina baba leo wanafanya vema kuonyesha watoto wao shauku kama hiyo.—9/15, kurasa za 20, 21.

◻ Ni jambo gani lililo muhimu kabisa kwa ndoa na maisha ya familia yenye mafanikio?

Ili kupata matokeo mazuri, sikuzote ni lazima wenzi wa ndoa watangulize mapenzi ya Mungu. Wakifanya hivyo, wenzi wa ndoa hujaribu kushikamana pamoja na kujaribu kusuluhisha matatizo yao kwa kutumia shauri la Neno la Mungu. Hivyo wao huepuka maumivu mengi ya moyoni ambayo hutokea mapenzi yake yanapopuuzwa. (Zaburi 19:7-11)—10/1, ukurasa wa 11.

◻ Hisi ya kimungu ya uharaka ni muhimu kadiri gani leo?

Hisi ya kimungu ya uharaka ni sehemu ya maana sana ya utumishi wa nafsi yote kwa Yehova. Huondoa na kusaidia kukabili majaribu ya Ibilisi ya kuwafanya watumishi wa Mungu ‘wachoke na kuzimia katika nafsi zao.’ (Waebrania 12:3, NW) Huwalinda kutojiingiza kupita kiasi katika ulimwengu na ufuatiaji wao wa vitu vya kimwili, ikiweka akili zao kwenye “uzima ulio kweli kweli.” (1 Timotheo 6:19)—10/1, ukurasa wa 28.

◻ Katika mfano wa kondoo na mbuzi, Yesu aketi wakati gani juu ya kiti chake cha ufalme na kwa nini? (Mathayo 25:31-33)

Mfano huu haumwonyeshi akiketi kwa maana ya kuwa Mfalme. Badala ya hivyo, aketi akiwa Hakimu. Kuhukumu huko si kitu cha kuendelea kwa kipindi cha miaka mingi. Badala ya hivyo, huu mfano waelekezea wakati ujao ambapo Yesu kwa kipindi kifupi atatangaza na kutekeleza hukumu dhidi ya mataifa.—10/15, kurasa za 22, 23.

◻ Ni nini kile “kizazi” kilichorejezewa mara nyingi na Yesu?

Yesu alitumia usemi “kizazi hiki” kurejezea umati wa wakati wake ukiwa pamoja na “viongozi [wao] vipofu” ambao kwa pamoja walifanyiza taifa la Kiyahudi. (Mathayo 11:16; 15:14; 24:34)—11/1, ukurasa wa 14.

◻ Katika utimizo wa mwisho wa unabii wa Yesu unaopatikana kwenye Mathayo 24:34-39, usemi “kizazi hiki” hurejezea nini?

Yaonekana Yesu arejezea watu walioko duniani wanaoona ishara ya kuwapo kwa Kristo lakini wanakataa kurekebisha njia zao.—11/1, kurasa za 19, 31.

◻ Mpango wa majiji ya makimbilio na vikwazo vyayo ulinufaishaje watu katika Israeli la kale?

Uliwakazia Waisraeli kwamba hawakupaswa kuwa watu wa kuchukua mambo kijuu-juu au kutojali uhai wa kibinadamu. Pia ulikazia uhitaji wa kuonyesha rehema wakati kufanya hivyo kulipofaa. (Yakobo 2:13)—11/15, ukurasa wa 14.

◻ Ni nini jiji la makimbilio la ufananisho?

Huu ni uandalizi wa Mungu wa kutulinda kutokana na kifo kwa kukiuka amri yake kuhusu utakaso wa damu. (Mwanzo 9:6)—11/15, ukurasa wa 17.

◻ Udugu wa Kikristo waweza kutusaidiaje ‘kupata nguvu tena’? (Isaya 40:31, NW)

Miongoni mwa ndugu na dada zetu Wakristo, mna wale ambao huenda wanakabili mikazo au majaribu kama hayo na ambao huenda wanapata hisia zinazofanana na zetu kabisa. (1 Petro 5:9) Linatupa uhakikisho na kuimarisha imani kujua kwamba yale tunayopitia ni ya kawaida na kwamba hisia zetu ni za kawaida.—12/1, kurasa za 15, 16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki