Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 2/1 uku. 15
  • ‘Wang’aa Wakiwa Wamulikaji Katika Ulimwengu’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Wang’aa Wakiwa Wamulikaji Katika Ulimwengu’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Mashahidi wa Yehova na Suala la Damu
    Mashahidi wa Yehova na Suala la Damu
  • Maswali ya Funzo la Kijitabu Mashahidi wa Yehova na Suala la Damu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Kuokoa Uhai kwa Damu—Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Kwa Kweli Ingefaa Uitazame Video No Blood—Medicine Meets the Challenge
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 2/1 uku. 15

Wapiga-Mbiu wa Ufalme Waripoti

‘Wang’aa Wakiwa Wamulikaji Katika Ulimwengu’

MASHAHIDI WA YEHOVA ni watu wa kipekee nao hutangazwa vibaya kwa sababu ya kukataa kutiwa damu mishipani. Hata hivyo, msimamo huu wategemea Biblia kabisa. Biblia huonyesha kwamba Mungu hushutumu kutumia damu vibaya, kwa kuwa damu ni yenye thamani machoni pake. (Mwanzo 9:3, 4; Mambo ya Walawi 17:14) Kwa sababu ya kuchunguza Maandiko katika habari hii, Mashahidi wa Yehova wameamua kwamba mwongozo wa Biblia wa ‘kujiepusha na damu’ kwa wazi ulitia ndani zoea la kisasa la kutia damu mishipani.—Matendo 15:19, 20, 28, 29.

Katika miaka ya majuzi washiriki wa jamii ya kitiba, na vilevile mahakama katika baadhi ya nchi, wameunga mkono Mashahidi wa Yehova katika suala hili. Kwa kielelezo, katika Denmark, mama mmoja mchanga aliyefahamu maoni ya Biblia juu ya damu alikufa katika aksidenti ya gari. Kwa sababu ya kukataa kutiwa damu mshipani, madaktari wake walichochea kampeni ya mwezi mzima ya utangazaji mbaya kupitia vyombo vya habari dhidi ya Mashahidi wa Yehova.

Wazazi wa mwanamke huyo mchanga wakaomba uchunguzi ufanywe, na katika Aprili 1994 uamuzi ulitangazwa na Tume ya Malalamiko ya Wagonjwa ya Denmark. Uamuzi huo ulisema kwamba mgonjwa huyo hakufa kwa sababu ya kukataa damu, bali kwa sababu wanatiba walikosa kufanya kazi yao. Uamuzi huo ulitegemea uchunguzi mbalimbali uliofanywa na Halmashauri ya Tiba na Sheria pamoja na wenye mamlaka wa mambo ya afya. Katika barua iliyopelekewa vituo vyote vya afya katika Denmark, Halmashauri ya Kitaifa ya Afya ilisema kwamba madaktari wana wajibu wa kuwapa Mashahidi wa Yehova tiba ya badala iliyo bora zaidi ipatikanayo, wakifikiria kukataa kwao damu.

Kisa kingine kilihusu Dan, Shahidi mwenye umri wa miaka 15 aliyekufa kutokana na leukemia. Katika kisa hiki madaktari walifuata uamuzi wenye ujasiri wa Dan wa kukataa utiaji-damu mshipani. Hilo lilitokeza kampeni yenye kuenea pote ambamo vyombo vya habari vililaumu madaktari kwa ajili ya kifo cha Dan. Hata hivyo, wengi hawakukubaliana na matangazo hayo mabaya.

Kwa kielelezo, mwalimu-mkuu wa shule aliyokuwa akihudhuria Dan alikuwapo kwenye Jumba la Ufalme kwa ajili ya hotuba ya maziko. Alishangaa sana juu ya kutangazwa vibaya kwa kifo cha Dan kwenye habari. Baada ya kumfikia Shahidi mmoja mfanyakazi mwenzake akiwa na maswali kadhaa kuhusu Mashahidi wa Yehova, alikubali kuchukua nakala ya vidio Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name. Vidio hiyo ilimvutia sana hivi kwamba akapanga walimu wote katika shule waione. Baadaye, wanafunzi wote walionyeshwa vidio hiyo, darasa moja baada ya jingine.

Waziri wa afya wa Denmark pia hakukubaliana na jinsi madaktari wa Dan walivyotangazwa vibaya. Alisema kwamba madaktari walifanya jambo lifaalo katika kuheshimu uamuzi mkomavu na imani yenye nguvu ya Dan.

Kuna mamilioni ya wapiga-mbiu wa Ufalme wanaotii sheria za Mungu. Kwa sababu ya utii wao, wao hutokeza sana, ‘waking’aa wakiwa wamulikaji katika ulimwengu.’—Wafilipi 2:12, 15, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki