Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 1/15 kur. 3-4
  • Ni Nani Walio Wajumbe Halisi wa Amani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nani Walio Wajumbe Halisi wa Amani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Amani Halisi Yakaribia!
  • Wajumbe wa Amani wa Mungu
  • Amani ya Kweli—Kutoka Chanzo Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Acha “Amani Ya Mungu” Ilinde Moyo Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Jinsi Ambavyo Amani Yaweza Kupatikana Duniani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Kutumikia Tukiwa Wajumbe wa Amani ya Kimungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 1/15 kur. 3-4

Ni Nani Walio Wajumbe Halisi wa Amani?

KATIKA Mei 31, 1996, vyanzo vya habari vilipiga mbiu ya ule ulioonekana kuwa ujumbe wa amani. Siku iliyotangulia, taarifa rasmi ilitolewa iliyothibitisha kwamba Benjamin Netanyahu, ambaye punde tu angekuwa waziri mkuu wa Israeli, alikuwa “anajihusisha sana na kuendelezwa kwa zile harakati za amani, amani pamoja na usalama, kati ya serikali ya Israeli na majirani wayo wote, kutia na Wapalestina.”

Uchaguzi wa Netanyahu uliotangazwa sana ulifanya wengi wajiulize ikiwa amani katika Mashariki ya Kati yaweza kuwa uhalisi. Ikiwa ndivyo, je, mataifa mengine yangeweza kuiga Israeli kwa kusahau tofauti zao?

Bila shaka ni rahisi zaidi kuahidi amani kuliko kuipata. Kwa kuwa wengi walijua hilo, walishuku. Kama vile mwandishi wa habari Hemi Shalev alivyosema, “nusu ya watu katika Israeli sasa wanahisi kwamba ukombozi wakaribia na nusu ile nyingine waamini kwamba wamenaswa katika helo duniani.” Kwa ufupi, alitaarifu hivi: “Watu fulani wanashangilia; wengine wanaomboleza.”

Ndivyo inavyokuwa mwanadamu anapojaribu kuleta amani. Ushindi wa kiongozi mmoja na wanaomwunga mkono humaanisha ushinde wa wapinzani. Kutoridhika huongoza kwenye mzinduko, na mzinduko, mara nyingi huongoza kwenye uasi. Iwe ni katika Mashariki ya Kati, Amerika ya Latini, Ulaya Mashariki, au kwingine kokote—jitihada za wanadamu za kupata amani ni maono ya uwongo.

Amani Halisi Yakaribia!

Amani katika Mashariki ya Kati ilipokuwa kichwa cha habari motomoto, ujumbe mwingine wa amani ulisikiwa. Huo haukuwa usemi wa kisiasa uliotangazwa sana; wala haukuwa mkataba wa amani kati ya mataifa. Badala ya hivyo, ujumbe huo ulipiga mbiu ya amani ambayo itakuja kupitia tu Ufalme wa Mungu. Ujumbe huo ulisikiwa wapi? Kwenye “Wajumbe wa Amani ya Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya zaidi ya 1,900 iliyofanywa na Mashahidi wa Yehova ulimwenguni kote katika 1996/1997.

Kwenye mikusanyiko hiyo ilijulishwa waziwazi kwamba hakuna serikali yoyote ya kibinadamu iwezayo kuleta amani na usalama wa kweli. Kwa nini? Kwa kuwa hilo lingetaka kukomeshwa kwa mambo yanayotunyang’anya amani kila siku. Amani ya kweli yamaanisha kuamka kila asubuhi bila tisho la vita au jeuri. Yamaanisha hakuna uhalifu tena, hakuna makufuli milangoni petu tena, hakuna hofu ya kutembea mitaani tena, hakuna familia zilizotenganishwa tena. Ni serikali ipi duniani iwezayo kutimiza hayo yote? Kwa kweli, ni serikali ipi duniani ambayo hata ingejaribu kuahidi hayo?

Hata hivyo, Ufalme wa Mungu waweza, nao utafikiliza mambo hayo. Biblia yaahidi hivi: “Tazama! Hema la Mungu liko pamoja na wanadamu, naye atakaa pamoja nao, nao watakuwa vikundi vya watu wake. Na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. Naye atafuta kabisa kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala ombolezo wala kupaaza kilio wala umivu halitakuwapo tena kamwe. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.” (Ufunuo 21:3, 4) Hilo litaletea wanadamu wanaoteseka kitulizo kama nini!

Ahadi ya Yehova Mungu si maneno matupu. Biblia yatuhakikishia hivi: “Mungu si mtu, aseme uongo; wala si mwanadamu, ajute; iwapo amesema, hatalitenda? Iwapo amenena, hatalifikiliza?” (Hesabu 23:19) Ndiyo, yale ambayo Mungu ameahidi yatatimia—kwa baraka ya wale wote wanaochukua msimamo wao upande wake.

Wajumbe wa Amani wa Mungu

Mashahidi wa Yehova wanajulikana sana kwa kuhubiri kwao kwenye bidii kuhusu Ufalme wa Mungu. Kila mwaka, wote pamoja hutumia saa zaidi ya bilioni moja wakishiriki pamoja na wengine ujumbe wa Biblia wenye kutia moyo. Huo watimiza maneno ya Yesu: “Habari njema hii ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa kwa ajili ya kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:14) Ujumbe wanaoleta hao Mashahidi ni “habari njema” kwelikweli, kwa kuwa watangaza Ufalme wa kimbingu wa Mungu kuwa tumaini pekee la wanadamu. Nao ni tumaini la wakati ujao lenye nguvu kama nini!

Hata sasa Ufalme wa Mungu unatokeza kifungo halisi cha amani na upendo wa kidugu katika raia wao. Yesu alisema hivi: “Kwa hilo wote watajua kwamba nyinyi ni wanafunzi wangu, mkiwa na upendo miongoni mwenu wenyewe.” (Yohana 13:35) Mashahidi wa Yehova hujitahidi kuishi kwa kupatana na takwa hilo la msingi la Ukristo wa kweli. Tokeo ni kwamba, wana udugu wa ajabu unaounganisha Wayahudi na Waarabu, Wakroatia na Waserbia, Wahutu na Watutsi. Amani hiyo ambayo wengi wa wanadamu waweza tu kuiwazia sasa ni ya mamilioni ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote.

Kitia-moyo cha kuendelea kuishi kwa kupatana na kanuni za Biblia na kuendelea kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu kilikaziwa kwenye programu ya Mkusanyiko wa Wilaya wa “Wajumbe wa Amani ya Kimungu.” Twakualika usome ripoti ifuatayo juu ya huo mkusanyiko wa siku tatu wenye kuchochea ambao mamilioni ya watu wamekuwa wakifurahia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki