Kujifunza Kutokana na Makosa ya Wakati Uliopita
Sheria Za Maadili Za Muumba Wetu Ni Za Milele Nazo Hazibadiliki. Kwa Sababu Hiyo Kanuni Ipatikanayo Kwenye Wagalatia 6:7 Hutumika Leo: “Lolote Lile Mtu Analopanda, Hilo Atavuna Pia.” Ni Kweli Kwamba Huenda Mtu Akadai Kwamba Hana Wajibu Wowote Kuelekea Mungu, Lakini Kanuni Ya Kimungu Hudumu Vilevile Daima. Hatimaye, Kila Binadamu Hupatwa Na Matokeo Ya Matendo Yake.
Vipi Juu Ya Mtu Anayeishi Maisha Mapotovu, Kisha Abadilika, Na Kuwa Mtumishi Wa Mungu? Huenda Bado Akalazimika Kuvumilia Matokeo Ya Mtindo-maisha Wake Wa Awali. Hata Hivyo, Hilo Halimaanishi Kwamba Mungu Hajamsamehe. Uzinzi Wa Mfalme Daudi Na Bath-sheba Ulileta Misiba Mingi Maishani Mwake. Hangeweza Kuiponyoka. Lakini Alitubu, Naye Mungu Akamsamehe.—2 Samweli 12:13-19; 13:1-31.
Je, Umepata Kuvunjika Moyo Upatwapo Na Matokeo Ya Makosa Ambayo Umefanya? Kwa Maoni Mazuri, Kughairi Kwaweza Kuwa Kikumbusha Kwetu Cha ‘Kujitunza, Tusiutazame Uovu.’ (Ayubu 36:21) Naam, Kughairi Kwaweza Kutusaidia Kuepuka Kurudia Kosa. Jambo La Maana Hata Zaidi Ni Kwamba Daudi Alitumia Mambo Yaliyompata Kutokana Na Dhambi Aliyofanya Ili Kujifaidi Yeye Mwenyewe Na Wengine Pia. Alisema Hivi: “Nitawafundisha Wakosaji Njia Zako, Na Wenye Dhambi Watarejea Kwako.”—Zaburi 51:13.
[Picha katika ukurasa wa 7]
Daudi alijifunza kutokana na dhambi yake na Bath-sheba