Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w99 11/1 kur. 7-8
  • Jitayarishe kwa Milenia Yenye Maana!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jitayarishe kwa Milenia Yenye Maana!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Kujipanga Kitengenezo Sasa kwa Ajili ya Miaka Elfu Itakayokuja
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Kuponda Kichwa cha Nyoka
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Miaka Elfu ya Faraja kwa Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
w99 11/1 kur. 7-8

Jitayarishe kwa Milenia Yenye Maana!

UTAWALA wa Miaka Elfu wa Kristo utailetea familia ya kibinadamu baraka kemkemu. Chini ya mwelekezo wenye upendo wa Yesu, wanadamu watainuliwa kutoka katika hali yao ya sasa yenye kusikitisha wafikie ukamilifu wenye utukufu. Ebu wazia hilo laweza kumaanisha nini kwako. Afya nzuri! Ebu wazia ukiamka kila asubuhi ukihisi vyema zaidi kuliko siku iliyotangulia. Mamilioni ya wanaume, wanawake, na watoto wanatazamia kwa hamu kuishi katika wakati huo wenye furaha. Wanautumainia na kusali kwa ajili yake. Funzo lao la Biblia limewahakikishia kwamba wanaweza kufurahia baraka hizo.

Hata hivyo, kabla ya kuanza Utawala wake wa Miaka Elfu, ni lazima Yesu Kristo awaondoe duniani wale wote wanaopinga utawala wake. Atafanya hivyo kwenye vita ambayo huitwa Har–Magedoni katika Biblia. (Ufunuo 16:16) Wakristo wa kweli duniani hawatapigana katika vita hiyo. Ni vita ya Mungu. Nayo haitapiganwa mahali fulani hususa. Biblia husema kwamba itafika sehemu za mbali zaidi za dunia. Adui za utawala wa Kristo watauawa. Hakuna hata mmoja wao atakayeponyoka!—Yeremia 25:33.

Ndipo Yesu atakapomgeukia Shetani Ibilisi na roho waovu wake. Ebu wazia vile hali itakavyokuwa, kama vile mwandishi wa kitabu cha Ufunuo alivyoiona: “Nikaona malaika [Yesu Kristo] akiteremka kutoka mbinguni mwenye ufunguo wa abiso na mnyororo mkubwa mkononi mwake. Naye akalikamata joka kubwa, nyoka wa awali, aliye Ibilisi na Shetani, na kumfunga kwa miaka elfu.” (Ufunuo 20:1, 2) Baadaye, Shetani na roho waovu wake wataangamizwa milele.—Mathayo 25:41.

“Umati mkubwa, ambao hakuna mtu a[na]yeweza kuuhesabu,” utaokoka Har–Magedoni. (Ufunuo 7:9) Kristo atawaongoza hao wanufaike kabisa na “mabubujiko ya maji ya uhai,” kama vile mchungaji aongozavyo kondoo zake kwenye maji yenye kuokoa uhai. (Ufunuo 7:17) Maendeleo yao ya kiroho yakiwa hayazuiwi na Shetani na roho waovu wake, waokokaji hawa wa Har–Magedoni watasaidiwa hatua kwa hatua kushinda mielekeo ya kutenda dhambi hadi hatimaye wafikie ukamilifu!

Chini ya utawala wenye upendo wa Kristo, hali za maisha zitazidi kuwa bora. Yehova Mungu, kupitia Yesu Kristo, ataondoa visababishi vyote vya maumivu na huzuni. “Atafuta kabisa kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala ombolezo wala kupaaza kilio wala umivu halitakuwapo tena kamwe.” (Ufunuo 21:4) Nabii Isaya amalizia maelezo hayo kwa kusema: “Ndipo macho ya vipofu yatafumbuliwa, na masikio ya viziwi yatazibuliwa. Ndipo mtu aliye kilema ataruka-ruka kama kulungu, na ulimi wake aliye bubu utaimba.” (Isaya 35:5, 6) Nao wafu, “wakubwa na wadogo,” watafufuliwa wakitazamia kuishi bila kufa kamwe!—Ufunuo 20:12.

Hata sasa, “umati mkubwa” utakaookoka Har–Magedoni unakusanywa. Watu hao wanajitayarisha kwa ajili ya Utawala wa Milenia wa Kristo. Ingawa hawajui utawala huo utaanza lini, wana hakika kwamba utaanza katika wakati wa Mungu uliowekwa. Unaweza kuwa miongoni mwao, lakini wewe pia ni lazima ujitayarishe—si kwa kuuza mali zako na kusafiri kwenda sehemu fulani hususa, lakini kwa kutwaa ujuzi sahihi juu ya Yehova Mungu na makusudi yake kupitia kujifunza Biblia. Bila malipo yoyote au masharti yoyote, Mashahidi wa Yehova watafurahi kukuonyesha jinsi funzo la Biblia liwezavyo kukunufaisha wewe na familia yako. Wachapishaji wa gazeti hili watafurahia kukupasha habari zaidi.

[Sanduku katika ukurasa wa 7]

Ile Miaka Elfu—Ni Halisi au Ni ya Ufananisho?

Kwa kuwa karibu kitabu chote cha Biblia cha Ufunuo kiliandikwa kwa lugha ya ufananisho, swali linazuka. Namna gani ule Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo unaotajwa katika Ufunuo? Je, ni halisi au ni wa ufananisho?

Kuna mambo mengi yaonyeshayo kwamba hiyo miaka elfu moja ni halisi. Fikiria: Mtume Paulo anaurejezea Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo, wakati ambapo wanadamu watahukumiwa, kuwa siku moja. (Matendo 17:31; Ufunuo 20:4) Mtume Petro aliandika kwamba siku moja (muda wa saa 24) kwa Yehova ni kama miaka elfu moja. (2 Petro 3:8) Maandiko hayo yanathibitisha kwamba “siku” hii ya hukumu ina urefu halisi wa miaka elfu moja. Isitoshe, katika Ufunuo 20:3, 5-7, UV, tunasoma kwenye sehemu nne tofauti juu ya ‘ile miaka elfu’ wala si “miaka elfu.” (Italiki ni zetu) Yaonekana jambo hilo laonyesha kipindi chenye urefu hususa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki