Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w03 3/15 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Tuadhimishe Mlo wa Jioni wa Bwana?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • “Endeleeni Kufanya Hivi Kwa Kunikumbuka Mimi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • ‘Fanyeni Hivi kwa Kunikumbuka Mimi’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
w03 3/15 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Je, mipango yoyote inaweza kufanywa iwapo Mkristo mtiwa-mafuta aliye mgonjwa hawezi kuadhimisha Mlo wa Jioni wa Bwana pamoja na kutaniko?

Ndiyo. Mipango inaweza na inapaswa kufanywa kwa kumfikiria Mkristo mtiwa-mafuta aliye mgonjwa ambaye hawezi kuwepo wakati kutaniko linapoadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Katika hali hiyo, baraza la wazee linaweza kupanga mzee mmoja au mwanamume Mkristo mkomavu ampelekee mwamini huyo mifano ya mkate na divai jioni hiyohiyo kabla ya jua kuchomoza siku inayofuata.

Ikitegemea hali, mzee au ndugu atakayemtembelea anaweza kutoa maelezo mafupi na kusoma maandiko yanayofaa. Anaweza kufuata kielelezo cha Yesu alipoanzisha Mlo wa Jioni wa Bwana. Kwa mfano, anaweza kusoma Mathayo 26:26 kisha ampe mkate usiotiwa chachu baada ya sala. Halafu, ndugu huyo anaweza kusoma Mathayo sura ya 26, mstari wa 27 na 28, kisha ampe divai baada ya kutoa sala nyingine. Maelezo mafupi yanaweza kutolewa kuhusu kinachowakilishwa na mifano hiyo, na sala ya kumalizia inapaswa kutolewa.

Bila shaka, tunapaswa kujitahidi juu chini kuwepo wakati kutaniko linapoadhimisha Mlo wa Jioni wa Bwana. Lakini ni nini kinachoweza kufanywa ikiwa Mkristo mtiwa-mafuta ni mgonjwa sana, amelazwa hospitalini, au kwa sababu fulani hawezi kuhudhuria Ukumbusho baada ya jua kutua Nisani 14? Mkristo huyo aliyetiwa mafuta anaweza kufuata kielelezo katika Sheria ya Musa na afanye Ukumbusho huo siku 30 baadaye.—Hesabu 9:9-14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki