Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w04 9/15 kur. 3-4
  • “Ninyi Msali Hivi”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Ninyi Msali Hivi”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kusali—Je, Kukariri Sala ya Bwana Ndiyo Njia Bora Zaidi ya Kusali?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Sala ya Bwana Inachomaanisha Kwako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Uwe Imara Katika Sala
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Kumfikia Mungu Katika Sala
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
w04 9/15 kur. 3-4

“Ninyi Msali Hivi”

JE, UNAJUA maneno ya Sala ya Bwana? Ilikuwa sala ya kielelezo iliyofundishwa na Yesu Kristo. Katika Mahubiri yake maarufu ya Mlimani, Yesu alisema: “Basi, ninyi msali hivi.” (Mathayo 6:9) Kwa kuwa ilianzishwa na Yesu, mara nyingi inaitwa Sala ya Bwana au Baba Yetu.—Kilatini, Paternoster.

Mamilioni ya watu ulimwenguni pote wameitia akilini Sala ya Bwana, nao huirudia mara nyingi, pengine kila siku. Katika miaka ya karibuni, wengi wameikariri sala hiyo shuleni na katika matukio ya umma. Kwa nini Sala ya Bwana inathaminiwa sana?

Cyprian, mwanatheolojia wa karne ya tatu aliandika: “Je, kuna sala ambayo ni ya kiroho zaidi kuliko ile tuliyopewa na Kristo . . . ? Ni sala ya aina gani kwa Baba ambayo inaweza kuwa ya kweli zaidi kuliko ile tuliyopewa na Mwana ambaye ndiye Kweli?”—Yohana 14:6.

Katika katekisimu yake, Kanisa Katoliki huiona Sala ya Bwana kuwa “sala ya msingi ya Kikristo.” Kichapo The World Book Encyclopedia kinakiri jinsi sala hii ilivyo muhimu katika dini zote zinazojiita za Kikristo, na kuitaja kuwa mojawapo ya “taarifa za msingi za imani ya Kikristo.”

Hata hivyo, tunapaswa kutambua kwamba wengi ambao hukariri Sala ya Bwana hawaielewi kabisa. “Ikiwa umelelewa katika dini fulani ya Kikristo huenda unaweza kuisema Sala ya Bwana mbiombio bila kutulia ili kupumua,” lasema gazeti la Kanada Ottawa Citizen, “lakini huenda ukaona ni vigumu kuisema polepole na kwa kuielewa.”

Je, kweli ni muhimu kuelewa sala tunazomtolea Mungu? Kwa nini Yesu alitupa Sala ya Bwana? Inamaanisha nini kwako? Acheni sasa tuzungumzie maswali hayo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki