Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w05 1/15 kur. 3-4
  • Ni Nini Huamua Wakati Wako Ujao?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nini Huamua Wakati Wako Ujao?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Unaweza Kuamua Wakati Wako Ujao Utakuwaje?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Kutafuta Mambo Yaliyokusudiwa Kimbele ya Mwanadamu
    Amkeni!—1999
  • “Siku Yangu Haikuwa Imefika”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Je, Wakati Ujao Wetu Umeandikwa Kimbele?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
w05 1/15 kur. 3-4

Ni Nini Huamua Wakati Wako Ujao?

“SAWA tu na wanyama, wanadamu hawawezi kuamua jinsi wakati wao ujao utakavyokuwa,” aandika mwana-mageuzi John Gray. Katika kitabu chake An Intelligent Person’s Guide to Judaism, mwandishi Shmuley Boteach anatoa maoni yaliyo tofauti kabisa na hayo. Anasema: “Mwanadamu si kama mnyama, kwa hiyo sikuzote anaweza kuamua jinsi wakati wake ujao utakavyokuwa.”

Watu wengi wanakubaliana na Gray, nao wanaamini kwamba nguvu za asili zisizoweza kudhibitiwa ndizo huamua jinsi wakati ujao wa wanadamu utakavyokuwa. Wengine huona kwamba mwanadamu ni kiumbe cha Mungu naye ana uwezo wa kuamua jinsi wakati wake ujao utakavyokuwa.

Wengine huhisi kwamba wakati wao ujao huamuliwa na wanadamu wenye mamlaka. Kulingana na mwandikaji Roy Weatherford, “watu wengi ulimwenguni—na hasa wanawake wengi katika historia—hawana . . . nguvu au uwezo juu ya maisha yao kwa sababu ya kukandamizwa na kutendewa vibaya.” (The Implications of Determinism) Ndoto za wengi kuhusu wakati ujao wenye furaha zimevunjwa na mamlaka za kisiasa au za kijeshi zinazoshindana.

Wengine katika historia yote wamehisi kuwa hoi kwa sababu walifikiri kwamba wakati wao ujao huamuliwa na nguvu zisizo za kibinadamu. Boteach asema kwamba, “Wagiriki wa kale walishikilia sana wazo la kwamba tumaini lote ni ubatili kwa kuwa mwanadamu hana uwezo wa kubadili wakati wake ujao ambao umeamuliwa kimbele.” Walihisi kwamba wakati ujao wa kila mtu uliamuliwa na miungu ya kike yenye kigeugeu. Waliamini kwamba miungu hiyo iliamua wakati ambapo mtu angekufa na pia kiwango cha maumivu na taabu ambayo angepata maishani.

Leo watu wengi huamini kwamba wakati ujao wa mtu huamuliwa na nguvu zisizo za kibinadamu. Kwa mfano, watu wengi wanaamini Kismet au majaliwa. Wanasema kwamba Mungu amepanga mapema matokeo ya matendo ya kila mwanadamu na wakati atakapokufa. Pia fundisho la kwamba mambo hupangwa mapema huendeleza wazo la kwamba Mungu Mweza-Yote “amepanga mapema wokovu au hukumu ya mwisho kabisa ya kila mwanadamu.” Watu wengi wanaodai kuwa Wakristo wanaamini fundisho hilo.

Wewe una maoni gani? Je, wakati wako ujao umeamuliwa tayari na nguvu zinazozidi uwezo wako? Au je, kuna ukweli fulani katika maneno haya yaliyoandikwa na mwandishi wa michezo ya kuigiza Mwingereza William Shakespeare: “Nyakati nyingine wanadamu hujiamulia jinsi wakati wao ujao utakavyokuwa”? Chunguza yale ambayo Biblia inasema kuhusu habari hii.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki