Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w07 2/1 uku. 16
  • Amosi—Je, Alikuwa Mkusanyaji au Mminyaji wa Tini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Amosi—Je, Alikuwa Mkusanyaji au Mminyaji wa Tini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Anatumia Watu wa Cheo Kidogo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Sema Neno la Mungu kwa Ujasiri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Matunda—Mazuri na Mabaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Kitabu Cha Biblia Namba 30—Amosi
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
w07 2/1 uku. 16

Amosi—Je, Alikuwa Mkusanyaji au Mminyaji wa Tini?

KATIKA karne ya tisa K.W.K., Amazia aliyekuwa mwovu na ambaye alikuwa kuhani wa ibada ya ndama alimwamuru nabii Amosi aache kutoa unabii katika Israeli. Amosi alikataa na kusema: “Nilikuwa mchungaji na mminyaji wa tini za mikuyu. Naye Yehova akanichukua nisifuatane na kundi tena, na Yehova akaendelea kuniambia, ‘Nenda, watolee unabii watu wangu Israeli.’” (Amosi 7:14, 15) Ndiyo, Yehova alimtuma Amosi awe nabii; hakujiweka mwenyewe kuwa nabii. Lakini Amosi alimaanisha nini aliposema kwamba alikuwa “mminyaji” wa tini za mikuyu?

Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “mminyaji” linapatikana mara hiyo moja tu katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Tafsiri nyingine za Biblia zinatumia neno “mkusanyaji,” “mkulima,” au “mtunzaji” wa mikuyu, badala ya “mminyaji,” wa tini za mikuyu. Hata hivyo, gazeti moja (Economic Botany) linasema kwamba tafsiri inayofaa ya neno hilo inapaswa kuwa “mwenye kuchanja” kwa sababu neno hilo linaonyesha tendo fulani la pekee ambalo lilifanywa na mkulima wa tini za mikuyu.

Zoea la kuminya, au kuchanja, yaani, kukata mikato midogo kwenye tini za mikuyu, limejulikana sana huko Misri na Saiprasi tangu zamani za kale. Kuchanja, au kuminya, hakufanywi tena katika nchi ya Israeli kwa sababu aina nyingine mbalimbali za tini zinapandwa katika nchi hiyo. Hata hivyo, Waisraeli wa siku za Amosi waliminya tini, kwa kuwa mikuyu iliyopandwa katika nchi ya Israeli wakati huo ilitokana na mikuyu ya Misri.

Inaelekea kwamba kuchanja tini kunaziwezesha kufyonza maji na hivyo kuwa na umajimaji. Kufanya hivyo pia kunatokeza gesi nyingi ya ethilini, ambayo inafanya tini ziive haraka na kuwa kubwa na tamu zaidi. Kwa kuongezea, tini zinapoiva haraka haziharibiwi na wadudu wanaoitwa nyigu ambao wanapenda matunda hayo.

Ingawa Amosi alikuwa na malezi ya hali ya chini akiwa mchungaji na mminyaji wa tini, hakuogopeshwa na maadui wake. Badala yake, alitangaza kwa ujasiri ujumbe wa Yehova wa hukumu juu ya Israeli. Aliwawekea watumishi wa Mungu leo mfano mzuri kama nini, kwa sababu wao pia wanapaswa kutangaza ujumbe usiopendwa na wengi!—Mathayo 5:11, 12; 10:22.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki