Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w07 12/1 uku. 3
  • Je, Inawezekana Kuwa na Ulimwengu Wenye Umoja?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Inawezekana Kuwa na Ulimwengu Wenye Umoja?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Familia ya Yehova Hufurahia Muungano Wenye Thamani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Dumisheni Muungano Katika Siku Hizi za Mwisho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Watu Wanaunganishwa Ulimwenguni—Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Nani Anayependezwa na Dini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
w07 12/1 uku. 3

Je, Inawezekana Kuwa na Ulimwengu Wenye Umoja?

JE, ULIMWENGU wetu unakaribia kupata amani au msiba? Inaonekana kuna hoja zinazounga mkono mawazo hayo mawili.

Kwa upande mmoja, viongozi fulani wa ulimwengu wanasema kwa usadikisho kwamba amani ni mradi ambao unaweza kufikiwa. Labda wanasema hivyo kwa sababu amani isipopatikana, hali ya ulimwengu itakuwa yenye kuogopesha sana. Kwa upande mwingine, watu wengi wanaogopa sana maswali kama haya: Ni mataifa gani yaliyo na silaha za maangamizi makubwa? Je, yatathubutu kuzitumia? Ni nini kitakachotukia ikiwa yatazitumia?

Kwa muda mrefu historia imeonyesha kwamba uadui na ubaguzi ndiyo mambo ambayo yamevunja tumaini lolote la kupata amani, na mara nyingi dini imechochea mapambano badala ya kuyakomesha. “Jambo lolote ambalo linawagawanya watu linaweza kusababisha uadui, na dini ni moja ya mambo yanayoleta migawanyiko mikubwa zaidi,” anaandika mwandishi wa habari James A. Haught. “Ingawa watu wengi wanaamini kwamba dini inawafanya watu wawe ‘wazuri,’ ni wazi kwamba inawafanya watu fulani watende matendo ya unyama.” Mtungaji Steven Weinberg ana maoni hayohayo. Anaandika hivi: “Dini tu ndiyo inayoweza kuwafanya watu wema watende maovu.”

Je, kuna tumaini lolote kwamba ulimwengu wetu utakuwa na umoja? Ndiyo! Lakini kama tutakavyoona, umoja ulimwenguni hautaletwa na wanadamu au dini za wanadamu.

[Blabu katika ukurasa wa 3]

Je, ulimwengu ni kama gruneti iliyo tayari kulipuka?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki