Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w09 2/1 kur. 3-4
  • Je, Unamjua Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Unamjua Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Ni Muhimu Kupata Majibu?
  • Ni Ibada ya Nani Anayoikubali Mungu?
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Wakristo Huabudu kwa Roho na Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • “Kweli Itawaweka Nyinyi Huru”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • “Njia na Kweli na Uzima”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
w09 2/1 kur. 3-4

Je, Unamjua Mungu?

UNGEJIBU swali hilo jinsi gani? Watu fulani wanahisi kwamba wanamjua Mungu vizuri, eti yeye ni kama rafiki wa karibu. Wengine wanamwona Mungu kuwa kama mtu wa ukoo wa mbali sana. Wanaamini kwamba yuko lakini hawamjui vizuri. Ikiwa unaamini kuna Mungu, ungejibu namna gani maswali yaliyoandikwa hapa chini?

1. Je, Mungu ni mtu halisi?

2. Je, Mungu ana jina?

3. Je, Yesu ni Mungu Mweza-Yote?

4. Je, Mungu ananijali?

5. Je, Mungu anakubali dini zote?

Ukiwaomba watu wajibu maswali hayo, yaelekea utapata majibu mengi sana yanayotofautiana. Basi, si ajabu kwamba kuna maoni na mafundisho mbalimbali yasiyo ya kweli kumhusu Mungu.

Kwa Nini Ni Muhimu Kupata Majibu?

Alipokuwa akizungumza na mwanamke aliyekutana naye kwenye kisima ambaye alikuwa na imani katika Mungu, Yesu Kristo alikazia umuhimu wa kujua ukweli kumhusu Mungu. Mwanamke huyo Msamaria, alikubali kwamba Yesu alikuwa nabii. Lakini kuna jambo lililomhangaisha. Dini ya Yesu ilikuwa tofauti na yake. Alipomweleza Yesu hangaiko lake, Yesu alimwambia hivi waziwazi: “Ninyi mnaabudu msichokijua.” (Yohana 4:19-22) Kutokana na maneno hayo ni wazi Yesu alifundisha kwamba si watu wote wanaomwamini Mungu wanaomjua kikweli.

Je, maneno ya Yesu yamaanisha kwamba hakuna mtu anayeweza kumjua Mungu kikweli? Hapana. Yesu alimwambia mwanamke huyo hivi: “Waabudu wa kweli watamwabudu Baba kwa roho na kweli, kwa maana, kwa kweli, Baba anawatafuta watu wa namna hiyo wamwabudu.” (Yohana 4:23) Je, wewe ni mmoja wa watu wanaomwabudu Mungu “kwa roho na kweli”?

Ni muhimu sana ufikirie jibu lako kwa swali hilo. Kwa nini? Yesu alikazia umuhimu wa kuwa na ujuzi sahihi aliposali hivi: “Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.” (Yohana 17:3) Naam, matarajio yako ya kuishi wakati ujao yanahusiana sana na kujua ukweli kumhusu Mungu!

Je, kweli inawezekana kujua ukweli kumhusu Mungu? Ndiyo inawezekana! Basi unaweza kujua ukweli huo jinsi gani? Yesu alisema hivi kujihusu: “Mimi ndiye njia na kweli na uzima. Hakuna anayekuja kwa Baba ila kupitia kwangu.” (Yohana 14:6) Pia alisema hivi: “Hakuna anayemjua Baba ni nani ila Mwana, na yule ambaye Mwana anapenda kumfunulia.”—Luka 10:22.

Kwa hiyo, siri ya kumjua Mungu inapatikana katika mafundisho ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu. Hata Yesu anatuahidi hivi: “Kama mkiyazingatia mafundisho yangu mtakuwa kweli wanafunzi wangu. Mtaujua ukweli, nao ukweli utawapeni uhuru.”—Yohana 8:31, 32, Biblia Habari Njema.

Hivyo basi, Yesu angejibu jinsi gani yale maswali matano yaliyoulizwa awali?

[Picha katika ukurasa wa 4]

Je, unamwabudu Mungu ambaye humjui vizuri?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki