Yaliyomo
Januari 15, 2011
Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania. Haki Zote Zimehifadhiwa
Toleo la Funzo
MAKALA ZA FUNZO ZA MAJUMA YA:
Februari (Mwezi wa 2) 28–Machi (Mwezi wa 3) 6, 2011
‘Pata Kimbilio Katika Jina la Yehova’
UKURASA WA 3
Machi 7-13, 2011
Heshimu Ndoa kwa Kuwa Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
UKURASA WA 13
Machi 14-20, 2011
Tumia Vizuri Kabisa Useja Wako
UKURASA WA 17
Machi 21-27, 2011
Tunatiwa Nguvu ili Kushinda Vishawishi na Kutovunjika Moyo
UKURASA WA 22
Machi 28, 2011–Aprili (Mwezi wa 4) 3, 2011
Tunatiwa Nguvu ili Kushinda Jaribu Lolote
UKURASA WA 26
Kusudi la Makala za Funzo
MAKALA YA 1 YA FUNZO UKURASA WA 3-7
Tunaweza kupata wapi kimbilio katika wakati huu mgumu? Neno la Mungu linaeleza kwamba tunaweza kupata kimbilio katika jina la Yehova. Habari hii inazungumzia jinsi tunavyoweza kupata ulinzi sasa na pia wakati “ile siku kuu ya Yehova” itakapokuja ghafula. Habari hii inakazia andiko la mwaka wa 2011.
MAKALA YA 2 NA YA 3 YA FUNZO UKURASA WA 13-21
Ndoa na useja ni zawadi kutoka kwa Mungu, na kila moja ina baraka zake. Iwe tumefunga ndoa au sisi ni waseja, makala hizi zitaonyesha kwa nini tunapaswa kuthamini zawadi hizo na kueleza jinsi tunavyoweza kuonyesha kwamba tunazithamini.
MAKALA YA 4 NA YA 5 YA FUNZO UKURASA WA 22-30
Tunahitaji msaada wa Yehova ili tuishi kulingana na wakfu wetu kwake. Makala hizi zitazungumzia jinsi roho takatifu inavyotusaidia kupambana na majaribu, kukabiliana na hali tunapovunjika moyo, kuvumilia mateso, kukataa kusongwa isivyofaa na marafiki, na kuvumilia matatizo.
PIA KATIKA TOLEO HILI:
7 Unaweza Kuona Jina la Mungu Katika Bonde Hili
9 Ninashukuru Kwamba Nimemtumikia Yehova, Hata Chini ya Majaribu
31 Tafakari Mambo Ambayo Yehova Amekufanyia
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 2]
© Stähli Rolf A/age fotostock