Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w11 10/1 uku. 11
  • Je, Watoto Wachanga Wanapaswa Kubatizwa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Watoto Wachanga Wanapaswa Kubatizwa?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Habari Zinazolingana
  • Wapendwa Wetu Walio Wafu Wako Wapi Sasa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Je! Watoto Wachanga Wabatizwe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Ubatizo Ni Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
w11 10/1 uku. 11

Wasomaji Wetu Wanauliza . . .

Je, Watoto Wachanga Wanapaswa Kubatizwa?

▪ “Nilikuwa na wasiwasi kwamba ndugu yangu mdogo, John, angeenda toharani (purgatori),” anasema Victoria. Kwa nini alikuwa na wasiwasi huo? “John alikufa kabla hajabatizwa,” akaeleza, “na kasisi wa Kanisa Katoliki alisema kwamba John angekaa toharani milele kwa sababu hakuwa amebatizwa.” Kwa kweli, imani kama hiyo inaogopesha, lakini je, inatokana na Biblia? Je, Biblia inafundisha kwamba watoto wanaokufa kabla ya kubatizwa wanahukumiwa kwenda toharani?

Biblia inafundisha kwamba Wakristo wanapaswa kubatizwa. Yesu aliwaagiza wafuasi wake hivi: “Mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, mkiwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, na kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.” (Mathayo 28:19, 20) Ona kwamba wale wanaobatizwa lazima wawe wanafunzi wa Yesu. Hilo linamaanisha kuwa ni watu waliojifunza kumhusu Yesu na wamechagua kumfuata—uamuzi ambao bila shaka hauwezi kufanywa na mtoto mchanga.

Hata hivyo, wengi wanasisitiza kwamba amri hiyo ya Yesu inawahusu pia watoto wachanga. Kasisi Richard P. Bucher wa Kanisa la Kilutheri anakazia hivi: “Kila mtu anapaswa kubatizwa, kutia ndani watoto wachanga. Kuwazuia wasibatizwe ni sawa na kuwazuia wasipate msamaha na hivyo kuwafanya wakabili hatari ya kuhukumiwa.” Hata hivyo, maelezo hayo yanapingana na mafundisho ya Yesu katika njia tatu hivi.

Kwanza, Yesu hakufundisha kwamba watoto wachanga wanapaswa kubatizwa. Kwa nini jambo hilo ni muhimu? Fikiria hili: Yesu aliwafundisha wanafunzi wake kwa bidii kuhusu matakwa ya Mungu. Mara kwa mara, alirudia mafundisho muhimu. Kwa nini? Ili kuhakikisha kwamba wanafunzi wake walielewa mafundisho hayo. (Mathayo 24:42; 25:13; Marko 9:34-37; 10:35-45) Lakini, hakuna wakati wowote ambapo Yesu alifundisha kuwa watoto wachanga wanapaswa kubatizwa. Je, huenda Yesu alisahau kutaja takwa hilo? Haiwezekani! Kwa kweli, kama ingekuwa lazima watoto wachanga wabatizwe, basi Yesu angesema hivyo.

Pili, Yesu hakufundisha kwamba mtu yeyote anateseka baada ya kufa. Aliamini Maandiko, ambayo yanasema hivi waziwazi: “Walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe.” (Mhubiri 9:5) Yesu alijua wafu hawateseki katika Limbo, moto wa mateso, toharani, au mahali pengine popote. Badala yake, alifundisha kwamba hawajui jambo lolote, ni kana kwamba wamelala usingizi.—Yohana 11:1-14.

Tatu,Yesu alifundisha kwamba “wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho” watafufuliwa. (Yohana 5:28, 29) Bila shaka, hao watatia ndani mamilioni ya watu ambao walikufa kabla ya kubatizwa. Baada ya kufufuliwa watakuwa na nafasi ya kujifunza kuhusu matakwa ya Mungu na kuishi milele katika Paradiso duniani.a—Zaburi 37:29.

Hivyo, ni wazi kuwa Biblia haifundishi kwamba watoto wachanga wanapaswa kubatizwa.

[Maelezo ya Chini]

a Ili kujifunza mengi kuhusu Paradiso duniani na tumaini la ufufuo, ona sura ya 3 na ya 7 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki