Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w12 6/1 uku. 4
  • Unabii wa Biblia Hutimia Kikamili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unabii wa Biblia Hutimia Kikamili
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Ugiriki—Ile Serikali Kubwa ya Tano ya Ulimwengu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Ni Nani Atakayeutawala Ulimwengu?
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Kitabu Kinachotegemeka—Sehemu ya 5
    Amkeni!—2011
  • Aleksanda Mkuu na Mifano ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 6/1 uku. 4

Unabii wa Biblia Hutimia Kikamili

“Halikukosa kutimia hata neno moja kati ya maneno yote mema ambayo Yehova Mungu wenu amewaambia ninyi.”​—YOSHUA 23:14.

BIBLIA INATOFAUTIANAJE NA VITABU VINGINE? Utabiri wa kale haukueleweka vizuri wala haukutegemeka, nao uaguzi unaofanya leo kwa kutumia nyota, vilevile hautegemeki. Wanadamu hujaribu kutabiri mambo yatakayotokea wakati ujao kwa kuchunguza mambo yanayotukia leo, lakini mara nyingi, hawatabiri matukio hususa yatakayotukia miaka mingi ijayo. Kinyume na hayo, unabii wa Biblia hutaja mambo hususa na siku zote hutimia, hata ikiwa unatabiri “kutoka zamani za kale mambo ambayo hayajafanywa.”​—Isaya 46:10.

MFANO: Katika karne ya sita K.W.K., nabii Danieli aliona maono yaliyotabiri kwamba milki ya Ugiriki ingeshinda kwa ghafla Muungano wa Umedi na Uajemi. Pia, yalitabiri kwamba muda mfupi baada ya mfalme wa Ugiriki kupata ushindi na ‘kuwa na nguvu,’ ufalme wake ‘ungevunjwa.’ Nani angekuwa mfalme badala yake? Danieli aliandika: “Kuna falme nne zitakazosimama kutoka katika taifa lake, lakini si kwa nguvu zake.”​—Danieli 8:5-8, 20-22.

MAONI YA WANAHISTORIA: Zaidi ya miaka 200 baada ya kipindi ambacho nabii Danieli aliishi, Aleksanda Mkuu alianza kutawala milki ya Ugiriki. Miaka kumi tu baada ya kuanza kutawala, Aleksanda alikuwa ameshinda Milki ya Umedi na Uajemi na kupanua utawala wa Ugiriki kufikia Mto Indus (kwa sasa uko Pakistan). Lakini alikufa kwa ghafula akiwa na umri wa miaka 32. Mwishowe, vita vilivyopiganwa karibu na kijiji cha Ipsus, katika Asia Ndogo, vilifanya milki yake igawanyike. Washindi wanne wa pigano hilo waligawana Milki ya Ugiriki. Hata hivyo, hakuna yeyote kati yao aliyewahi kuwa na nguvu kama za Aleksanda.

UNA MAONI GANI? Je, kuna kitabu kingine chochote kinachoweza kudai kwamba unabii wake umetimia kikamili? Au je, Biblia ni kitabu cha kipekee?

“Biblia ina unabii . . .  mwingi hivi kwamba haiwezekani kudai kuwa unatimia tu wenyewe.”​—KITABU A LAWYER EXAMINES THE BIBLE, CHA IRWIN H. LINTON

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki