Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w12 7/1 uku. 3
  • Je, Kuna Yeyote Anayesikiliza Sala?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Kuna Yeyote Anayesikiliza Sala?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Watu Wengi Wana Shaka?
  • Zawadi ya Sala
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Mkaribie Mungu Kupitia Sala
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Kumkaribia Mungu Katika Sala
    Mungu Anataka Tufanye Nini?
  • Utangulizi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 7/1 uku. 3

Je, Kuna Yeyote Anayesikiliza Sala?

“Nilikuwa na shaka kuhusu kuwapo kwa Mungu. Hata hivyo, nyakati nyingine nilijaribu kusali. Sikuwa na hakika ikiwa kuna yeyote aliyenisikiliza, lakini kusema kweli niliamini kulikuwa na mtu anayesikiliza sala. Sikuwa na furaha wala kusudi maishani. Niliogopa kuamini kwamba kuna Mungu kwa sababu nilifikiri ni watu dhaifu tu ndio walioamini Mungu.”​—⁠PATRICIA,a IRELAND.

JE, UMEWAHI kuhisi kama alivyohisi Patricia? Je wewe husali hata kama unatilia shaka kwamba kuna Mungu? Ikiwa ndivyo, basi si wewe peke yako mwenye hisia kama hizo. Fikiria mambo yafuatayo.

◼ Utafiti uliohusisha raia 2,200 wa Uingereza ulionyesha kuwa ni asilimia 22 tu kati ya watu hao wanaoamini kwamba kuna Mungu aliyeumba ulimwengu na ambaye husikiliza sala. Hata hivyo, kati ya watu waliohojiwa, asilimia 55 husali mara chache tu.

◼ Utafiti mwingine uliohusisha watu 10,000 katika nchi mbalimbali ulionyesha kwamba wale wanaodai hakuna Mungu, karibu asilimia 30 kati yao husali.

Kwa Nini Watu Wengi Wana Shaka?

Allan mwanamume kutoka Uingereza anasema hivi: “Nilizoea kusema kwamba siamini kuna Mungu kwa sababu nilifikiri dini huanzishwa kwa kusudi la kuwadhibiti watu au kupata pesa. Vilevile, nilifikiri ikiwa kuna Mungu hakungekuwa na ukosefu mwingi sana wa haki. Hata hivyo, nyakati nyingine ningeketi peke yangu na kusali kwa ‘mtu’ asiyejulikana. Pia, ningejiuliza, ‘Chanzo cha uhai ni nini? ’ ”

Kila mtu mwenye hisia kama hizo ana sababu zake zinazomfanya atilie shaka kama sala hujibiwa. Mara nyingi, wanakuwa na shaka kwa sababu ya kukosa majibu ya maswali kama vile:

◼ Je, kuna Muumba?

◼ Kwa nini mara nyingi dini inachochea watu wafanye mambo mabaya?

◼ Kwa nini Mungu ameruhusu kuteseka?

Ikiwa ungepata majibu ya maswali hayo, je, ungesali ukiwa na uhakika?

[Maelezo ya Chini]

a Baadhi ya majina katika mfululizo huu yamebadilishwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki