Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 1/15 uku. 32
  • Kampeni Iliyopangwa Vizuri Yafanikiwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kampeni Iliyopangwa Vizuri Yafanikiwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “ALITARAJIA KUKUTANA NA MTU MZIMA”
  • Unapaswa Kusali kwa Njia Gani ili Mungu Akusikilize?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
  • Walijitoa Wenyewe kwa Hiari Nchini Norway
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Miili Midogo, Mioyo Mikubwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Usambazaji wa Mialiko ya Ukumbusho Utaanza Aprili 2
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/15 uku. 32

Kampeni Iliyopangwa Vizuri Yafanikiwa

[Picha katika ukurasa wa 32]

María Isabel ni mhubiri kijana mwenye bidii katika mji wa San Bernardo katika nchi ya Chile huko Amerika ya Kusini. Yeye na familia yake ni wa kabila la Mapuche. Familia nzima imekuwa ikiunga mkono kwa bidii jitihada za kuanzisha kutaniko jipya linalotumia lugha ya Mapuche linaloitwa pia Mapudungun.

Ilipotangazwa kwamba Ukumbusho wa kifo cha Kristo ungefanywa pia huko Mapudungun na kwamba mialiko 2,000 ya Ukumbusho iliyochapishwa katika lugha ya Mapuche ingesambazwa, María Isabel alifikiria jambo hilo. Angefanya nini ili kusaidia? Alikumbuka mambo yaliyoonwa ya vijana wengine Mashahidi waliopata matokeo mazuri walipowahubiria wanafunzi wenzao na walimu wao. Alizungumza na wazazi wake kuhusu jambo hilo na kwa pamoja wakaamua kwamba María Isabel afikirie jinsi atakavyosambaza mialiko hiyo shuleni. Alifanya mipango gani?

Kwanza, María Isabel aliwaomba wasimamizi wa shule ruhusa ya kubandika mwaliko kwenye lango kuu la shule. Walikubali na kumpongeza kwa kuwafikia. Siku moja asubuhi wanafunzi walipokusanyika, mwalimu mkuu alitangaza kwa kipaaza-sauti kuhusu mwaliko huo!

Kisha, María Isabel akaomba ruhusa ya kutembelea madarasa yote. Baada ya kupewa ruhusa na walimu, alianza kuwauliza wanafunzi katika kila darasa ikiwa yeyote kati yao ni wa jamii ya Wamapuche. Anasema hivi: “Nilifikiri kwamba huenda katika shule nzima kungekuwa na wanafunzi 10 au 15 tu waliotoka katika familia za Wamapuche. Lakini walikuwa wengi zaidi kwa kuwa mialiko 150 ilichukuliwa!”

“ALITARAJIA KUKUTANA NA MTU MZIMA”

Mwanamke mmoja aliyeona mwaliko kwenye lango kuu la shule aliuliza angepata wapi habari zaidi kuhusu tukio hilo. Wazia jinsi alivyoshangaa wakati alipoelekezwa kwa msichana mwenye umri wa miaka kumi! María Isabel asema hivi huku akitabasamu: “Alitarajia kukutana na mtu mzima.” Baada ya kumpa mwaliko na kumfafanulia kifupi, María Isabel alimuuliza anaishi wapi ili wazazi wake waweze kumtembelea na kumweleza mengi zaidi kuhusu Ufalme wa Mungu. Wahubiri 20 wanaohubiri katika eneo linalozungumza lugha ya Mapuche walifurahi kama nini kumwona mwanamke huyo pamoja na Wamapuche wengine 26 wanaopendezwa wakiwa wamehudhuria Ukumbusho. Kikundi hicho sasa ni kutaniko linaloendelea kukua!

Haidhuru una umri gani, je, unaweza kuchukua hatua kama hiyo ya kuwaalika wanafunzi au wafanyakazi wenzako kwa ajili ya Ukumbusho, hotuba ya watu wote, au kusanyiko la wilaya? Kwa nini usifanye utafiti katika machapisho yetu ili uone mambo yaliyoonwa yatakayokusaidia kufanikiwa kufanya hivyo? Sali pia ili roho takatifu ya Yehova ikusaidie kupata ujasiri wa kuwaambia wengine kumhusu. (Luka 11:13) Ukifanya hivyo, wewe pia utasisimuka kwa furaha na pia utatiwa moyo sana na matokeo ya mipango yako mizuri.

Kampeni Iliyopangwa Vizuri Yafanikiwa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki