Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 7/1 uku. 6
  • Je, Dini Inategemeka Kuhusiana na Maadili?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Dini Inategemeka Kuhusiana na Maadili?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • BIBLIA INAFUNDISHA NINI?
  • MASHAHIDI WA YEHOVA WANAFANYAJE?
  • Inamaanisha Nini Kuwa Mkristo?
    Amkeni!—2007
  • Nani Anayependezwa na Dini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Dini
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Dini Yako Inapasa Kufikiriwa Sana
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 7/1 uku. 6
[Picha katika ukurasa wa 6]

Je, Dini Inategemeka Kuhusiana na Maadili?

“Nilipokuwa chuoni wanafunzi wengi walidai kuwa wafuasi wa dini,” anasema Sylvia, ambaye ni muuguzi. “Hata hivyo waliiba mitihani na kutumia madawa ya kulevya. Dini haikuwasaidia kuwa na maadili safi.”

Mwanamume anayeitwa Lionel anasema: “Wafanyakazi wenzangu hudanganya kwamba ni wagonjwa ili wasije kazini. Kwao dini ni kama kitu ambacho hawatumii—kama kiti au meza ya maonyesho.”

Dini haijasaidia watu wengi kuwa na maadili safi. Watu wengi leo wana “namna ya ujitoaji-kimungu” lakini ‘wanazikana nguvu zake.’ (2 Timotheo 3:5) Viongozi wao wa kidini hawaweki mfano mzuri, wala hawatumii Biblia kuwashauri wafuasi wao wawe na maadili safi. Ndiyo sababu watu wengi wanafikiri Mungu hajali jinsi wanavyoishi.

BIBLIA INAFUNDISHA NINI?

Biblia inaonyesha kwamba Mungu ana hisia na anazingatia mwenendo wetu. Waisraeli wa kale walipomwasi Mungu, ‘walimhuzunisha.’ (Zaburi 78:40) Hata hivyo, kunakuwa na “shangwe zaidi mbinguni” mtu anapoacha maisha mapotovu. (Luka 15:7) Mtu anapojifunza kuhusu sifa nzuri za Baba yetu wa mbinguni, anaimarisha upendo wake kwa Mungu, anachochewa kupenda mambo ambayo Mungu anapenda na kuchukia mambo anayochukia.​—Amosi 5:15.

MASHAHIDI WA YEHOVA WANAFANYAJE?

Mashahidi wa Yehova “husaidia watu kuimarisha familia zao na kuwa raia wenye bidii na wanyoofu,” linasema gazeti Deseret News la Salt Lake City, Utah, Marekani. Gazeti hilo linaongezea hivi: “Washiriki wao hufuata viwango vya juu vya maadili. Wanaamini kwamba kuvuta sigara, kunywa pombe kupita kiasi, kutumia dawa za kulevya, kucheza kamari, kufanya uasherati, uzinzi, na ngono za jinsia moja kunaharibu uhusiano wa mtu pamoja na Mungu.”

Je, viongozi wa kidini wamewasaidia wafuasi wao kufuata viwango vya Mungu kuhusu maadili?

Kujifunza kumhusu Mungu kumewasaidiaje Mashahidi? “Ni jambo la kawaida kudanganya katika biashara zinazohusisha matibabu,” anasema Sylvia, aliyetajwa mapema. “Ni rahisi sana kudanganya. Lakini kukumbuka sheria za Yehovaa kumenisaidia kufanya mambo yanayofaa. Nina furaha na amani moyoni.” Sylvia anaamini kwamba kuishi kupatana na imani yake ya kidini kumeboresha maisha yake.

a Yehova ni jina la Mungu kama linavyofunuliwa katika Biblia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki