Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 8/15 uku. 8
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kushughulika na Mtu Aliyetengwa na Ushirika
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Onyesha Uaminifu wa Kikristo Mtu wa Ukoo Anapotengwa na Ushirika
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Mpende Yehova Zaidi ya Familia
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 8/15 uku. 8

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Je, ingefaa wazazi Wakristo kuketi pamoja na mtoto wao aliyetengwa na ushirika katika mikutano ya kutaniko?

Hakuna sababu ya kuhangaika isivyo lazima kuhusu mahali ambapo mtu aliyetengwa na ushirika anaketi kwenye Jumba la Ufalme. Gazeti hili limewatia moyo sana wazazi Wakristo kuandaa msaada wa kiroho kwa mtoto wao aliyetengwa na ushirika ambaye bado anaishi nyumbani ikiwa wanaona inafaa kufanya hivyo. Kama inavyoonyeshwa kwenye ukurasa wa 19 na 20 wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 15, 1988, wazazi wanaweza kujifunza Biblia pamoja na mtoto wao mdogo aliyetengwa na ushirika anayeishi pamoja nao. Kwa njia hiyo, inatumainiwa kwamba mtoto atapata msaada anaohitaji ili arekebishe mwenendo wake.a

Inapohusu mahali pa kuketi katika Jumba la Ufalme, huenda likawa jambo linalopatana na akili kwa mtoto mdogo aliyetengwa na ushirika kuketi kwa utulivu pamoja na wazazi wake. Kwa kuwa si sheria kwa mtu aliyetengwa na ushirika kuketi nyuma katika Jumba la Ufalme, hakuna sababu ya kumzuia mtoto mdogo aliyetengwa na ushirika kuketi na wazazi wake popote pale. Wazazi wanapohangaikia hali ya kiroho ya mtoto wao, bila shaka watahakikisha kwamba anafaidika kikamili mikutanoni. Wazazi wanapoketi na mtoto wao huenda hilo likawasaidia kutimiza jukumu hilo.

Hata hivyo, namna gani ikiwa mtoto aliyetengwa na ushirika haishi na wazazi wake? Je, hilo linamaanisha kwamba hawezi kuketi nao? Zamani, gazeti hili lilitaja waziwazi kuhusu mtazamo unaofaa ambao Mkristo anapaswa kujitahidi kudumisha inapohusu kushirikiana na mtu wa ukoo aliyetengwa na ushirika asiyeishi nyumbani.b Hata hivyo, mtu aliyetengwa na ushirika kuketi kwa utulivu pamoja na watu wake wa ukoo wakati wa mikutano ni tofauti na washiriki wa familia kutafuta kimakusudi fursa za kushirikiana naye. Ikiwa washiriki wa familia waaminifu wana mtazamo unaofaa kuelekea mtu wao wa ukoo aliyetengwa na ushirika, nao wanajitahidi kuheshimu shauri la Kimaandiko kuhusu kutoshirikiana naye, huenda kusiwe na sababu ya kuhangaishwa na jambo hilo.​—1 Kor. 5:11, 13; 2 Yoh. 11.

Iwe mtu aliyetengwa na ushirika anaketi pamoja na mtu wake wa ukoo au na mshiriki mwingine wa kutaniko, jambo hilo halipaswi kuhangaikiwa isivyo lazima ikiwa mtu huyo anajiendesha kwa njia nzuri. Kuweka sheria kuhusu mahali ambapo mtu anapaswa kuketi kunaweza kusababisha matatizo mbalimbali ikitegemea hali. Ikiwa watu wote kutia ndani watu wa ukoo wanajitahidi kwa uaminifu kuheshimu kanuni za Biblia zinazohusu kutenga na ushirika, na ikiwa jambo hilo haliwakwazi akina ndugu, hakuna sababu ya kuwawekea sheria kuhusu mahali pa kuketi wale wanaohudhuria mikutano ya Kikristo.

a Tazama Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 1982, ukurasa wa 22 na 23.

b Hili ni rekebisho la habari iliyochapishwa katika Mnara wa Mlinzi, Aprili 1, 1953, ukurasa wa 223, Kiingereza.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki