Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 10/1 uku. 3
  • Kwa Nini Upendezwe na Ujumbe wa Biblia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Upendezwe na Ujumbe wa Biblia?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Ujifunze Biblia?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Kitabu Kinachoeleweka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Je! Kweli Biblia Ilitoka kwa Mungu?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Mafundisho ya Kweli Yanayompendeza Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 10/1 uku. 3
[Picha katika ukurasa wa 3]

HABARI KUU | BIBLIA INA UJUMBE GANI?

Kwa Nini Upendezwe na Ujumbe wa Biblia?

Biblia ndicho kitabu ambacho kimeenezwa zaidi ulimwenguni. Kwa nini? Kwanza, ni rahisi kuielewa. Ina habari kuhusu watu halisi, jinsi walivyoshirikiana na pia uhusiano wao na Mungu. Masimulizi hayo yanatufundisha mambo muhimu kwa sababu yameandikwa kwa maneno yanayoeleweka kwa urahisi. Hivyo, Biblia imetafsiriwa katika lugha nyingi, na watu wanaoishi eneo lolote na wakati wowote wanaweza kuielewa. Ushauri wa Biblia unatunufaisha sikuzote.

Jambo muhimu ni kwamba, Biblia si tu kitabu kinachozungumzia habari za Mungu bali pia ni kitabu kutoka kwa Mungu. Biblia inatujulisha jina la Mungu, utu wake, na kusudi lake lisilobadilika la kuumba dunia na wanadamu. Pia, inaeleza kuhusu vita kati ya wema na uovu, na jinsi mambo yatakavyokuwa mazuri wakati ujao. Ikiwa tutasoma Biblia tukiwa na maoni mazuri, tutaimarisha imani na tumaini letu.

Biblia ina habari ambazo hatuwezi kupata mahali pengine popote. Kwa mfano, Biblia hutueleza ukweli kuhusu mambo yafuatayo:

  • Historia ya wanadamu na chanzo cha mateso

  • Mpango wa Mungu wa kuwakomboa wanadamu

  • Mambo ambayo Yesu ametufanyia

  • Wakati ujao wa wanadamu na dunia

Soma kurasa zifuatazo ili uone ujumbe ulio katika Biblia.

TAARIFA FUPI KUHUSU BIBLIA

  • Habari Kuu: Jinsi Ufalme wa Mungu ulio mbinguni utakavyoleta amani na uadilifu duniani

  • Yaliyomo: Vitabu 39 vya Kiebrania (sehemu fulani ziliandikwa kwa Kiaramu) na 27 vya Kigiriki

  • Waandikaji: Vitabu hivyo viliandikwa na watu wapatao 40 kwa karibu miaka 1,600, kutoka mwaka wa 1513 K.W.K. hadi kufikia mwaka wa 98 W.K.

  • Lugha: Kufikia sasa imetafsiriwa katika lugha zaidi ya 2,500 ikiwa nzima au kwa sehemu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki