Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 10/1 uku. 4
  • Historia ya Wanadamu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Historia ya Wanadamu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Kusudi la Mungu kwa Wanadamu Ni Nini?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Kwa Sababu Gani Wanadamu Wanakufa?
    Furahia Milele Maisha Duniani!
  • Paradiso Yapotea
    Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Kwa Nini Uovu Unaendelea
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 10/1 uku. 4
[Picha katika ukurasa wa 4]

HABARI KUU | BIBLIA INA UJUMBE GANI?

Historia ya Wanadamu

Kwa ufupi, kitabu cha kwanza cha Biblia cha Mwanzo, kinaeleza chanzo cha ulimwengu kwa maneno haya: “Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.” (Mwanzo 1:1) Baada ya Mungu kuumba mimea na wanyama, aliwaumba wanadamu wa kwanza, Adamu na Hawa. Walikuwa tofauti na wanyama kwa sababu kwa kiasi fulani wanadamu wana sifa kama za Mungu, kutia ndani uhuru wa kuchagua. Hivyo, waliwajibika kwa mambo waliyofanya. Ikiwa wangemtii Mungu, wangeshiriki kutimiza kusudi la Mungu wakiwa wazazi wa kwanza wa familia ya wanadamu ulimwenguni. Wanadamu wangefurahia amani na maisha makamilifu milele hapa duniani.

Hata hivyo, malaika fulani aliwatumia wanadamu kutimiza tamaa yake mbaya. Hivyo akawa Shetani, jina linalomaanisha “Mpinzani.” Kupitia nyoka, Shetani alimdanganya Hawa kwa kumwambia kwamba angekuwa na maisha mazuri bila mwongozo wa Mungu. Adamu and Hawa walimfuata Shetani na hivyo wakaharibu uhusiano na Muumba wao. Kwa sababu ya uamuzi wao mbaya, wazazi wetu wa kwanza walipoteza nafasi ya kuishi milele na hivyo sote tukarithi dhambi, kutokamilika, na kifo.

Mara moja, Mungu alitangaza nia yake ya kurekebisha hali hiyo yenye kusikitisha na kuwafungulia wazao wa Adamu njia ya kupata uzima wa milele. Mungu alitabiri kwamba “uzao”​—mtu fulani wa pekee—​ungemwangamiza Shetani na kuondoa mateso yote ambayo Shetani, Adamu, na Hawa walisababisha. (Mwanzo 3:15) Ni nani angekuja kuwa huo “uzao”? Hilo lingejulikana baada ya muda.

Hata hivyo, Shetani aliendelea kujaribu kuzuia kusudi zuri la Mungu lisitimie. Dhambi na uovu ulienea haraka sana. Mungu aliazimia kuwaangamiza watu waovu kupitia gharika. Alimwelekeza Noa mwadilifu ajenge safina, yaani, sanduku kubwa lililoelea juu ya maji, ili ajiokoe yeye na familia yake, pamoja na wanyama alioagizwa awaingize kwenye safina.

Mwaka mmoja baada ya Furiko hilo, Noa na familia yake walitoka ndani ya safina dunia ikiwa imesafishwa. Lakini bado “uzao” haukuwa umetokea.

​—Habari hii inategemea Mwanzo sura ya 1-11; Yuda 6, 14, 15; Ufunuo 12:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki