Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 10/1 uku. 5
  • Mpango wa Mungu wa Kuwakomboa Wanadamu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mpango wa Mungu wa Kuwakomboa Wanadamu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Mambo Ambayo Mungu Aliahidi Kupitia Manabii
    Imani ya Kweli—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha
  • Ni Nini Kusudi la Mungu kwa Ainabinadamu?
    Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?
  • Masihi! Njia ya Mungu ya Wokovu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • “Tumempata Masihi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 10/1 uku. 5
[Picha katika ukurasa wa 5]

HABARI KUU | BIBLIA INA UJUMBE GANI?

Mpango wa Mungu wa Kuwakomboa Wanadamu

Mungu alimwahidi Abrahamu kwamba ule “uzao” ulioahidiwa ungetokana na yeye. Kupitia “uzao” huo, watu wa “mataifa yote” wangepata baraka. (Mwanzo 22:18) Baadaye, Yakobo mjukuu wa Abrahamu alihamia Misri ambako familia yake iliongezeka na kuwa taifa la kale la Israeli.

[Picha katika ukurasa wa 5]

Hatimaye, Farao mkatili aliwafanya Waisraeli wawe watumwa huko Misri hadi Mungu alipomweka Musa kuwa nabii aliyeliongoza taifa la Israeli kutoka kwenye nchi hiyo na kupita katikati ya maji yaliyogawanyika ya Bahari Nyekundu. Baada ya hilo, Mungu aliwapa Waisraeli sheria, kutia ndani zile Amri Kumi, ili kuwaongoza na kuwalinda. Sheria hizo zilionyesha dhabihu hususa walizopaswa kutoa ili wapate msamaha wa dhambi. Mungu alimwongoza Musa kuliambia taifa la Israeli kwamba angewatumia nabii mwingine. Nabii huyo angekuwa ule “uzao” ulioahidiwa.

Zaidi ya miaka mia nne hivi baadaye, Mungu alimwahidi Mfalme Daudi kwamba yule anayekuja, yaani, ule “uzao” uliotabiriwa katika Edeni, angetawala ufalme ambao ungedumu milele. Huyo angekuwa Masihi, Mkombozi aliyechaguliwa na Mungu ili kuwaokoa wanadamu na kuigeuza dunia iwe paradiso.

Kupitia Daudi na manabii wengine, hatua kwa hatua Mungu alifunua zaidi habari kuhusu Masihi. Walitabiri kwamba angekuwa mnyenyekevu na mwenye fadhili na kwamba angeondoa njaa, ukosefu wa haki, na vita. Chini ya utawala wake wanadamu wote wangekuwa na amani kati yao na pia na wanyama. Kifo, magonjwa, na mateso ambayo hayakuwa sehemu ya kusudi la awali la Mungu yangeondolewa, na wafu wangefufuliwa hapa duniani.

Mungu alitabiri kupitia nabii Mika kwamba Masihi angezaliwa katika mji wa Bethlehemu na akatabiri kupitia nabii Danieli kwamba baadaye angeuawa. Hata hivyo, Mungu angemfufua Masihi na kumfanya awe Mfalme mbinguni. Pia, Danieli alitabiri hatimaye Ufalme wa Masihi ungeondoa kabisa serikali nyingine zote. Je, Masihi alikuja kama ilivyotabiriwa?

​—Habari hii inategemea Mwanzo sura ya 22-50, vilevile Kutoka, Kumbukumbu la Torati, Samweli wa 2, Zaburi, Isaya, Danieli, Mika, Zekaria 9:9.

JINA TAKATIFU LA MUNGU

Jina Yehova linapatikana kwa mara ya kwanza katika Biblia kwenye andiko la Mwanzo 2:4. Jina hili la pekee linapatikana mara 7,000 hivi katika maandishi ya awali ya Maandiko Matakatifu. Jina hilo linamaanisha “Yeye Husababisha Kuwa.” Hilo linatuhakikishia kwamba Mungu anaweza kutimiza jambo lolote ambalo amekusudia au ameahidi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki