Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 10/1 uku. 3
  • Kwa Nini Upendezwe na Ufalme wa Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Upendezwe na Ufalme wa Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari Zinazolingana
  • “Ufalme Wako Uje”—​Sala Ambayo Mamilioni ya Watu Husali
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2020
  • Kile Ufalme wa Mungu Unachomaanisha kwa Wengi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Ufalme wa Mungu—Tumaini Peke Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Mafundisho ya Yesu Kuhusu Ufalme wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 10/1 uku. 3
Watu wa mataifa mbalimbali wakijifunza kuhusu Ufalme wa Mungu

HABARI KUU | UFALME WA MUNGUKINGDOM—UNA UMUHIMU GANI KWAKO?

Kwa Nini Upendezwe na Ufalme wa Mungu?

Ufalme wa Mungu umewapa tumaini mamilioni ya watu ulimwenguni pote. Wanafuata mfano uliowekwa na Yesu, ambaye aliwafundisha wafuasi wake wasali hivi: “Ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani.”—Mathayo 6:9, 10, Union Version.

Kwa kushangaza, ingawa watu wengi wanapendezwa na Ufalme wa Mungu, dini nyingi hazifundishi sana kuuhusu. Kuhusiana na hilo, mwanahistoria H. G. Wells alikazia jinsi Yesu “alivyozingatia sana . . . kufundisha kuhusu Ufalme wa Mbinguni” ingawa fundisho hilo, akaendelea kusema Wells, “si muhimu sana katika . . . mafundisho ya makanisa mengi ya Kikristo leo.”

Tofauti na makanisa hayo, Mashahidi wa Yehova wanakazia sana Ufalme wa Mungu. Hebu fikiria: Gazeti letu kuu ambalo unasoma sasa, linachapishwa katika lugha 220. Kwa kila toleo, tunachapisha nakala milioni 46 hivi, na hivyo kulifanya liwe gazeti linalosambazwa kwa wingi zaidi ulimwenguni. Gazeti hili lina ujumbe gani wa msingi? Linaitwa: Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova.a

Kwa nini Mashahidi wa Yehova wanajitahidi sana kuhubiri na kutangaza kuhusu Ufalme wa Mungu? Kwanza kabisa, tunaamini kwamba Ufalme wa Mungu ndio ujumbe wa msingi wa kitabu muhimu zaidi ulimwenguni, yaani, Biblia. Isitoshe, tunasadiki kwamba Ufalme wa Mungu ndio suluhisho pekee na la kudumu la matatizo yanayowapata wanadamu leo.

Mashahidi wa Yehova wanajitahidi kumwiga Yesu kwa kutangaza kuhusu Ufalme wa Mungu. Alipokuwa duniani, alizingatia sana Ufalme wa Mungu katika maisha na huduma yake. (Luka 4:43) Kwa nini Ufalme ulikuwa muhimu sana kwa Yesu? Na unaweza kuwa na umuhimu gani kwako? Tunakuomba uchunguze majibu ya Biblia katika makala zifuatazo.

a Yehova ni jina la Mungu kama linavyofunuliwa katika Biblia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki