Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 12/15 kur. 4-5
  • Yehova Huwabariki Sana Wenye Nia ya Kutoa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yehova Huwabariki Sana Wenye Nia ya Kutoa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari Zinazolingana
  • “Kazi Ni Kubwa”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Thamini Ukarimu wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Ziada Yao Ilijazia Upungufu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Jinsi Tunavyoweza Kuwasaidia Wenye Uhitaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 12/15 kur. 4-5
Mtu akitoa mchango

Yehova Huwabariki Sana Wenye Nia ya Kutoa

MUUMBA wetu amewaheshimu wanadamu kwa kuwapa zawadi yenye thamani sana ya hiari. Kwa kuongezea, Yehova huwabariki sana wale wanaotumia hiari yao kuendeleza ibada ya kweli na ambao hushiriki kutakasa jina lake takatifu na kuunga mkono kusudi lake kuu. Yehova hataki tumtii ili kutimiza wajibu tu au kwa kulazimishwa au kutishwa. Badala yake, anathamini sana tunapojitoa kwa hiari kwa sababu tunampenda kikweli na kumthamini kutoka moyoni.

Kwa mfano, Waisraeli walipokuwa katika nyika ya Sinai, Yehova aliwaagiza wajenge mahali pa ibada. Alisema hivi: “Kutoka katikati yenu toeni mchango kwa ajili ya Yehova. Kila mtu mwenye moyo wenye nia na aulete ukiwa mchango wa Yehova.” (Kut. 35:5) Kila Mwisraeli angetoa chochote alichoweza kutoa, na kila mchango wa hiari ulitumiwa kwa njia inayofaa ili kutimiza kusudi la Mungu, haidhuru mtu alitoa kitu gani au kiasi gani. Waisraeli waliitikiaje?

“Kila mtu ambaye moyo wake ulimsukuma” na “kila mtu ambaye roho yake ilimchochea” alitoa mchango wa hiari, “kila mtu mwenye moyo wenye nia.” Wanaume na wanawake walileta kwa hiari kitu fulani kwa ajili ya kazi ya Yehova. Walileta bizimu, vipuli, pete, dhahabu, fedha, shaba, uzi wa bluu, sufu iliyotiwa rangi ya zambarau, kitambaa chenye rangi nyekundu, kitani bora, manyoya ya mbuzi, ngozi za kondoo-dume zilizotiwa rangi nyekundu, ngozi za sili, mbao za mshita, mawe yenye thamani, zeri, na mafuta. Hatimaye, “vitu hivyo vikawa vya kutosha kwa ajili ya kazi yote iliyopasa kufanywa, na kuzidi.”—Kut. 35:21-24, 27-29; 36:7.

Jambo lililomfurahisha zaidi Yehova si vitu walivyotoa, bali ni roho ya kutoa kwa hiari ya wale ambao walitegemeza ibada safi. Walichochewa pia kutumia kwa hiari wakati na nguvu zao. Masimulizi hayo yanasema: “Wanawake wote waliokuwa wenye hekima ya moyo wakasokota kwa mikono yao.” Kwa kweli, “wanawake wote ambao mioyo yao iliwasukuma kwa hekima wakasokota manyoya ya mbuzi.” Isitoshe, Yehova alimpa Bezaleli ‘hekima, uelewaji, na ujuzi katika kila aina ya ufundi.’ Kwa kweli, Mungu aliwajaza Bezaleli na Oholiabu ustadi uliohitajiwa ili kufanya kazi aliyowaagiza.—Kut. 35:25, 26, 30-35.

Yehova alipowaomba Waisraeli watoe mchango, alikuwa na uhakika kabisa kwamba “kila mtu mwenye moyo wenye nia” angetegemeza ibada ya kweli. Na Yehova aliwabariki sana waliokuwa na roho ya kutoa kwa hiari kwa kuwaongoza na kuwapa shangwe isiyo na kifani. Kwa njia hiyo, Yehova alionyesha kwamba anapobariki roho ya kutoa kwa hiari ya watumishi wake, anaweza kuhakikisha kwamba wana mali na ujuzi wa kutimiza mapenzi yake. (Zab. 34:9) Unapomtumikia Yehova bila ubinafsi, kwa hakika atabariki nia yako ya kutoa.

JINSI AMBAVYO WENGINE HUTOA MICHANGO KWA AJILI YA KAZI YA ULIMWENGUNI POTE

Kama ilivyokuwa katika siku za mtume Paulo, wengi leo ‘huweka kando kitu fulani,’ au kiasi fulani cha pesa ambacho wanatumbukiza katika masanduku ya michango yaliyoandikwa “Kazi ya Ulimwenguni Pote.” (1 Kor. 16:2) Kila mwezi, makutaniko yanatuma pesa hizo kwenye ofisi ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi katika nchi yao. Unaweza pia kutuma michango moja kwa moja kwa shirika la kisheria linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova katika nchi yenu. Ili kujua shirika la kisheria linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova katika nchi yenu, tafadhali wasiliana na ofisi ya tawi inayosimamia kazi katika nchi yenu. Anwani za ofisi za tawi zinaweza kupatikana katika tovuti ya www.jw.org. Unaweza kutuma michango ifuatayo moja kwa moja:

MICHANGO YA MOJA KWA MOJA

  • Michango hii hutumwa kupitia mfumo wa kielektroniki, kadi ya benki au kadi ya mkopo. Ofisi nyingine za tawi zinatumia pia Tovuti ya jw.org au Tovuti nyingine inayopendekezwa kupokea michango.

  • Michango hii inatia ndani pesa taslimu, vito, au mali yoyote ya kibinafsi iliyo na thamani. Ambatanisha na barua inayoonyesha kwamba pesa taslimu au mali hizo ni michango ya moja kwa moja.

MPANGO WA MICHANGO YENYE MASHARTI

  • Hii ni michango ya pesa taslimu zinazotolewa kwa masharti kwamba zinaweza kurudishwa kwa aliyechangia akizihitaji.

  • Ambatanisha na barua inayoonyesha kwamba ni mchango wenye masharti.

UTOAJI ULIOPANGWA

Mbali na zawadi za pesa na mali za kibinafsi zenye thamani, kuna njia nyingine za kutoa michango kwa ajili ya kazi ya Ufalme ya ulimwenguni pote. Njia hizo zimeorodheshwa hapa chini. Haidhuru ni njia gani ambayo ungependa kutumia, tafadhali wasiliana kwanza na ofisi ya tawi inayosimamia kazi nchini mwenu ili kuona ni njia zipi zinazotumika katika nchi yenu. Kwa kuwa matakwa ya kisheria na sheria za kodi zinatofautiana, ni muhimu kuwasiliana na wataalamu wa mambo ya kodi na sheria kabla ya kuchagua njia bora ya kutoa mchango.

Bima: Huu ni mchango unaotolewa kwa kutaja kihususa shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova litakalofaidika na bima ya maisha au mpango wa malipo ya uzeeni au ya kustaafu.

Akaunti za Benki: Akaunti za benki, hati za amana, au akiba za pesa za kustaafu za mtu mmoja-mmoja zinaweza kuwekwa zikiwa amana, au mtu akifa zinaweza kulipwa kwa shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova kulingana na matakwa ya benki za kwenu.

Hisa na Dhamana: Hisa na dhamana zinaweza kuchangwa kwa shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova zikiwa zawadi ya moja kwa moja au mtoaji anaweza kuandika kwamba akifa shirika hilo lipewe hisa na dhamana zake.

Ardhi na Nyumba: Ardhi au nyumba zinazotolewa kama mchango kwa shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova zinaweza kutolewa zikiwa zawadi ya moja kwa moja au zawadi yenye masharti, yaani, mtoaji anaweza kuendelea kuishi humo hadi kifo chake.

Malipo ya Mwaka: Pesa au amana zinazotolewa kama mchango kwa shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova chini ya makubaliano kwamba anayetoa mchango huo, au mtu fulani aliyechaguliwa na mtoaji, anapata kiasi fulani cha pesa kila mwaka katika maisha yake yote. Huenda mtoaji akapunguziwa kodi ya serikali katika mwaka ambao mpango huo unaanzishwa.

Wosia na Amana: Mali au pesa zinaweza kuachiwa shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova kama urithi kwa njia ya wosia halali, au linaweza kutajwa kuwa shirika ambalo litafaidika na mkataba wa amana. Chini ya mpango huu, kodi fulani zinaweza kupunguzwa.

Maneno “utoaji uliopangwa” yanaonyesha kwamba mtu anapaswa kufanya mipango hususa ili atoe michango ya aina hiyo. Broshua ya Kiingereza na Kihispania yenye kichwa Charitable Planning to Benefit Kingdom Service Worldwide imetayarishwa ili kuwasaidia watu wanaotaka kutumia mpango huo kutegemeza kazi inayofanywa na Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote. Broshua hiyo iliandikwa ili kutoa habari kuhusu njia mbalimbali za kutoa zawadi sasa au baadaye kama urithi mtu anapokufa. Huenda habari fulani katika broshua hiyo zisikuhusu kwa sababu ya sheria za kodi au sheria nyingine nchini mwenu. Baada ya kusoma broshua hiyo, zungumza na wataalamu wa mambo ya kisheria au kodi. Kwa kutumia njia kama hizo za utoaji uliopangwa, watu wengi wametegemeza utendaji wetu wa kidini na kazi yetu ya kutoa misaada ulimwenguni pote, na hivyo wamepunguziwa sana kodi. Unaweza kupata broshua hiyo kwa kuomba nakala kutoka kwa mwandishi wa kutaniko ikiwa inapatikana nchini mwenu.

Kwa habari zaidi, unaweza kuwasiliana na ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi katika nchi yenu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki