Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 9/1 uku. 5
  • Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini?
    Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini?
  • Mashahidi wa Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Kwa Nini Tunahubiri?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 9/1 uku. 5
Wenzi wa ndoa ambao ni Mashahidi wa Yehova wakijifunza Biblia pamoja na watoto wao

HABARI KUU | MASHAHIDI WA YEHOVA NI NANI?

Mashahidi wa Yehova wanaamini nini?

Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba “andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu nalo ni lenye faida.” (2 Timotheo 3:16) Tunatumia Biblia kujifunza kuhusu Muumba na inatusaidia kuishi maisha yenye kusudi.

Biblia inasema hivi: “Ili watu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.” (Zaburi 83:18) Hivyo, sisi tunamwabudu Yehova Mungu peke yake na tukiwa Mashahidi wake tunajitahidi kuwaambia wengine kuhusu jina lake.—Isaya 43:10-12.

Tukiwa Wakristo, tunaamini kwamba Yesu, “Mwana wa Mungu,”a alikuja duniani na kisha akawa Masihi. (Yohana 1:34, 41; 4:25, 26) Baada ya kufa, alifufuliwa na kwenda mbinguni. (1 Wakorintho 15:3, 4) Baadaye, akawa Mfalme wa Ufalme wa Mungu. (Ufunuo 11:15) Ufalme huo ni serikali halisi itakayoleta Paradiso tena. (Danieli 2:44) Biblia inasema hivi: “Wapole wataimiliki dunia, nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.”—Zaburi 37:11, 29.

“Wanapoisoma Biblia, wanaamini kwamba Mungu anazungumza nao. Kila mara wanapopata matatizo katika maisha yao, wao huchunguza Neno la Mungu ili kupata suluhisho. . . . Wanaamini kwamba Neno la Mungu bado liko hai.”​—Kasisi Mkatoliki Benjamin Cherayath, gazeti la Münsterländische Volkszeitung, Ujerumani

Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba kanuni za Biblia zinaweza kuwanufaisha watu leo. (Isaya 48:17, 18) Hivyo, sisi hujitahidi sana kufuata kanuni hizo. Kwa mfano, sisi hatuvuti sigara au kutumia dawa za kulevya kwa sababu Biblia inasema tunapaswa kuepuka matendo yanayochafua akili na miili yetu. (2 Wakorintho 7:1) Pia, tunaepuka matendo yanayoshutumiwa na Biblia kama vile ulevi, uasherati, na wizi.—1 Wakorintho 6:9-11.

a Pia, Biblia inamtaja Yesu kuwa “Mwana mzaliwa-pekee wa Mungu” kwa sababu ni yeye peke yake aliyeumbwa moja kwa moja na Yehova.—Yohana 3:18; Wakolosai 1:13-15.

Wazazi wakifurahia kijana wao anapofungua zawadi

Ili kujua mengi zaidi kuhusu mambo tunayoamini, kutia ndani sababu inayotufanya tusisherehekee sikukuu au tusikubali kutiwa damu mishipani, tembelea www.jw.org/sw, na utafute kwenye KUTUHUSU > MASWALI YANAYOULIZWA MARA NYINGI.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki