Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 9/1 uku. 4
  • Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Aina Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Aina Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Sehemu ya 5—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • “Wana Nguvu Nyingi Ajabu za Kiadili”
    Amkeni!—1991
  • Kwa Nini Tunahubiri?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Kumrudia Mungu wa Kweli
    Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 9/1 uku. 4
Mashahidi wa Yehova wa kila jamii wakisalimiana katika Jumba la Ufalme

HABARI KUU | MASHAHIDI WA YEHOVA NI NANI?

Mashahidi wa Yehova ni watu wa aina gani?

Sisi ni tengenezo la kimataifa lisilokuwa na uhusiano wowote na vikundi vingine vya kidini. Ijapokuwa makao yetu makuu yako Marekani, idadi kubwa ya Mashahidi wa Yehova wanaishi katika nchi tofauti-tofauti. Mashahidi zaidi ya milioni nane hivi wanawafundisha watu Biblia katika nchi zaidi ya 230. Tunatii maneno haya ya Yesu: “Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote.”—Mathayo 24:14.

Bila kujali tunaishi wapi, sisi hutii sheria. Hata hivyo hatuungi mkono upande wowote wa siasa. Tunafanya hivyo kwa kuwa tunafuata agizo la Yesu kwa Wakristo la ‘kutokuwa sehemu ya ulimwengu.’ Hivyo, hatuungi mkono vita au kushiriki katika siasa. (Yohana 15:19; 17:16) Katika Vita vya Pili vya Ulimwengu, Mashahidi wa Yehova walifungwa gerezani, waliteswa, na kutendewa kikatili kwa sababu walikataa kulegeza msimamo wao wa kutounga mkono upande wowote. Mwanamume mmoja kutoka Ujerumani aliyewahi kuwa askofu aliandika hivi: “Wana haki ya kusema kwamba wao ndio kikundi kikubwa cha dini ambacho, kwa sababu ya dhamiri, kilikataa kujiunga na vita wakati wa utawala wa Nazi.”

“[Mashahidi wa Yehova] ni watu wenye maadili. Tungewapa watu hao wasio na ubinafsi vyeo vikubwa vya kisiasa—lakini kamwe hawawezi kukubali. . . . Wanaheshimu mamlaka za serikali lakini wanaamini kwamba Ufalme wa Mungu tu ndio utakaoondoa matatizo yote ya mwanadamu.”​—Gazeti la Nová Svoboda, Jamhuri ya Cheki.

Hata hivyo, hatujitengi na watu. Yesu alisali hivi kwa Mungu kuhusu wafuasi wake: “Ninakuomba, si kwamba uwatoe ulimwenguni.” (Yohana 17:15) Hivyo, huenda ukatuona tukifanya kazi, tukinunua bidhaa, na tukienda shule.

NCHI ZILIZO NA MASHAHIDI WENGI

  • Marekani 1,190,000

  • Mexico 800,000

  • Brazili 770,000

  • Nigeria 330,000

  • Italia 250,000

  • Japani 220,000

Waisraeli-wa-sasa

Tazama video yenye kichwa Kusanyiko la Wilaya la Pekee Nchini Israel, katika www.jw.org/sw, uone jinsi Mashahidi Waisraeli na Wapalestina wanavyoweza kushirikiana pamoja bila kujali tofauti za kitaifa na kijamii.(Tafuta kwenye KUTUHUSU > MAKUSANYIKO)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki