Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp16 Na. 4 uku. 8
  • Kwa Nini Biblia Iliokoka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Biblia Iliokoka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Habari Zinazolingana
  • Biblia Ni Ujumbe Kutoka kwa Mungu
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Historia Muhimu Sana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Msaada Zaidi Kwa Ajili ya Familia
    Amkeni!—2018
  • Una Maoni Gani Kuhusu Biblia?
    Una Maoni Gani Kuhusu Biblia?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
wp16 Na. 4 uku. 8
Mwanamume akisoma Biblia

HABARI KUU | JINSI BIBLIA ILIVYOOKOKA

Kwa Nini Biblia Iliokoka?

Biblia iliokoka. Ndiyo sababu tunaweza kuipata na kuisoma. Unapochagua tafsiri bora ya Maandiko, unaweza kuwa na uhakika kwamba unasoma nakala yenye kutegemeka ya maandishi ya kale.a Hata hivyo, kwa nini Biblia imedumu licha ya mazingira ambayo yangefanya iharibike, upinzani mkali, na jitihada za kubadili ujumbe wake? Kitabu hiki kina ujumbe gani wa pekee?

“Sasa ninaamini kwamba Biblia niliyo nayo ni zawadi kutoka kwa Mungu”

Wanafunzi wengi wa Biblia wanakubaliana na maneno ya mtume Paulo, aliyeandika hivi: “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu.” (2 Timotheo 3:16) Wanaamini kwamba Biblia imeokoka kwa sababu ni Neno la Mungu, Naye ameihifadhi hadi leo. Faizal, aliyetajwa mwanzoni mwa makala hii aliamua kuchunguza madai hayo kwa kujifunza Biblia. Mambo aliyojifunza yalimshangaza. Alijifunza kwamba mafundisho mengi ya dini zinazodai kuwa za Kikristo hayapatikani katika Biblia. Pia, alitiwa moyo sana kujua kusudi la Mungu kwa dunia kama linavyofunuliwa katika Neno Lake.

Faizal anasema, “Sasa ninaamini kwamba Biblia niliyo nayo ni zawadi kutoka kwa Mungu. Kwa kuongezea, kwa kuwa Mungu aliumba ulimwengu, bila shaka ana uwezo wa kutupatia kitabu na kukihifadhi kwa ajili yetu. Kufikiri kwamba Mungu hana uwezo huo ni kupinga nguvu za Mungu Mweza Yote. Mimi ni nani nipinge nguvu za Mungu?”​—Isaya 40:8.

a Soma makala “Jinsi ya Kuchagua Tafsiri Nzuri ya Biblia” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 1, 2008.

Tunawezaje Kuwa na Uhakika Kwamba Biblia ni Sahihi?

Mfululizo wa makala hii umeeleza jinsi Biblia ilivyookoka. Hata hivyo, unawezaje kuwa na uhakika kwamba Biblia “ni neno la Mungu” wala si mkusanyo wa hekaya? (1 Wathesalonike 2:13) Tazama video fupi, Tunawezaje Kuwa na Hakika Kwamba Yale Yaliyoandikwa Katika Biblia Ni ya Kweli? kwenye www.jw.org/sw. (Tafuta kwenye MACHAPISHO > VIDEO)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki