Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp16 Na. 5 uku. 16
  • Biblia Inasema ni Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia Inasema ni Nini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ufalme wa Mungu ni nini?
  • Ufalme wa Mungu utakuja lini?
  • Ufalme Wa Mungu
    Amkeni!—2013
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2020
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2020
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
wp16 Na. 5 uku. 16
Nuru kutoka katika kiti cha ufalme mbinguni, ikiangazia dunia

Biblia Inasema Nini?

Ufalme wa Mungu ni nini?

BAADHI YA WATU HUSEMA kwamba Ufalme wa Mungu upo moyoni; wengine wanafikiri kwamba ni jitihada za wanadamu za kuleta ulimwengu wenye amani na undugu. Wewe una maoni gani?

BIBLIA INASEMA HIVI:

“Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe. . . . Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote [za wanadamu].” (Danieli 2:44) Ufalme wa Mungu ni serikali halisi.

MAMBO MENGINE TUNAYOJIFUNZA KATIKA BIBLIA

  • Ufalme wa Mungu unatawala kutoka mbinguni. —Mathayo 10:7; Luka 10:9.

  • Mungu anatumia Ufalme huo kutimiza mapenzi yake mbinguni na duniani.—Mathayo 6:10.

Ufalme wa Mungu utakuja lini?

UNGEJIBUJE?

  • Hakuna anayejua

  • Hivi karibuni

  • Hautakuja kamwe

BIBLIA INASEMA HIVI:

“Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:14) Baada ya habari njema kuhubiriwa kikamili, Ufalme huo utakuja na kukomesha mfumo huu mwovu.

NI NINI KINGINE TUNACHOJIFUNZA KATIKA BIBLIA?

  • Hakuna hata mtu mmoja duniani anayejua kikamili wakati ambao Ufalme wa Mungu utakuja.—Mathayo 24:36.

  • Unabii wa Biblia unaonyesha kwamba Ufalme huo utakuja hivi karibuni.—Mathayo 24:3, 7, 12.

Kwa habari zaidi, soma sura ya 8 ya kitabu hiki, Biblia Inafundisha Nini Hasa?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Pia kinapatikana kwenye www.jw.org/sw

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki