Silaha zote za vita zitaharibiwa
Biblia Inasema Nini?
Je, amani itapatikana duniani?
Ungejibuje?
Ndiyo
Hapana
Labda
Biblia inasema nini?
Yesu atakapoitawala dunia, kutakuwa na “wingi wa amani mpaka mwezi utakapokuwa haupo tena,” yaani milele.—Zaburi 72:7.
Mambo mengine tunayojifunza katika Biblia
Waovu wataharibiwa, na waadilifu “watapata furaha yao tele katika wingi wa amani” duniani.—Zaburi 37:10, 11.
Mungu atakomesha vita vyote. —Zaburi 46:8, 9.
Je, inawezekana kuwa na amani ya akili leo?
Baadhi ya watu wanaamini . . . kwamba haiwezekani kuwa na amani ya kweli ya akili kwa sababu ya mateso na ukosefu wa haki uliokithiri duniani. Wewe una maoni gani?
Biblia inasema hivi:
Hata leo, wale walio na uhusiano wa karibu na Mungu wanaweza kuwa “na amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote.”—Wafilipi 4:6, 7.
Ni nini kingine tunachojifunza katika Biblia?
Mungu anaahidi kuondoa mateso na ukosefu wote wa haki, na “kufanya vitu vyote kuwa vipya.”—Ufunuo 21:4, 5.
Tunaweza kupata amani ya akili ikiwa tutatosheleza “uhitaji [wetu] wa kiroho.” —Mathayo 5:3.