“Umati mkubwa” wa watu, usiokuwa na idadi, kutoka katika mataifa yote utaokoka Har–Magedoni
Biblia Inasema Nini?
Har–Magedoni Ni Nini?
Baadhi ya watu wanaamini . . .
kwamba itakuwa ni uharibifu wa ulimwengu utakaosababishwa na silaha za nyuklia au uharibifu wa mazingira. Una maoni gani?
Biblia inasema hivi
Har–Magedoni ni mahali pa mfano pa “vita vya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote,” vita dhidi ya waovu. —Ufunuo 16:14, 16.
Ni nini kingine tunachojifunza katika Biblia?
Mungu atapigana vita vya Har–Magedoni si ili kuiharibu dunia, bali kuiokoa ili isiharibiwe zaidi na wanadamu.—Ufunuo 11:18.
Vita vya Har–Magedoni vitakomesha vita vingine vyote.—Zaburi 46:8, 9.
Je, inawezekana kuokoka vita vya Har–Magedoni?
Ungejibuje?
Ndiyo
Hapana
Labda
Biblia inasema hivi
“Umati mkubwa” wa watu kutoka mataifa yote utaokoka “dhiki kuu,” ambayo itafikia mwisho katika vita vya Har–Magedoni.—Ufunuo 7:9, 14.
Ni nini kingine tunachojifunza katika Biblia?
Mungu anataka watu wengi iwezekanavyo waokoke Har–Magedoni. Anawaharibu waovu pale tu wanapokataa kabisa kubadilika. —Ezekieli 18:32.
Biblia inaelezea jinsi ya kuokoka vita vya Har–Magedoni.—Sefania 2:3.