Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp19 Na. 2 kur. 10-11
  • Unapokuwa na Ugonjwa Mbaya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unapokuwa na Ugonjwa Mbaya
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MAMBO AMBAYO YAMEWASAIDIA WENGINE
  • Ugonjwa wa Kudumu—Hangaiko la Familia
    Amkeni!—2000
  • Kuishi kwa Mafanikio na Ugonjwa Wako—Jinsi Gani?
    Amkeni!—2001
  • Jinsi Ambavyo Familia Hukabiliana na Ugonjwa wa Kudumu
    Amkeni!—2000
  • Kwa Nini Ninalazimika Kuwa Mgonjwa Sana?
    Amkeni!—1997
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
wp19 Na. 2 kur. 10-11

Unapokuwa na Ugonjwa Mbaya

“Nilipoambiwa kwamba nina kansa kwenye pafu langu na kwenye utumbo, nilihisi kama nimehukumiwa kifo. Lakini nilipofika nyumbani, nilijiambia, ‘Ni kweli sikutazamia jambo hili, ila itabidi nitafute njia ya kupambana na hali hii.’”​—Linda, mwenye umri wa miaka 71.

“Nina ugonjwa unaoathiri neva kwenye upande wa kushoto wa uso wangu, na hunisababishia maumivu makali sana. Wakati fulani, maumivu hayo makali yamefanya nishuke moyo. Mara nyingi nilihisi hamna mtu anayenijali na hata nilifikiria kujiua.”​—Elise, mwenye umri wa miaka 49.

Mwanamume mgonjwa aliyeketi kwenye kiti chenye magurudumu akiwa pamoja na watu wanaompenda

IKIWA umeambiwa una ugonjwa unaoweza kusababisha kifo, au tatizo hilo limempata mtu unayempenda, basi unaelewa jinsi suala hilo linavyohangaisha. Zaidi ya kusumbuliwa na ugonjwa, bado unahitaji kupambana na hisia. Safari za kwenda kumwona daktari, ugumu wa kupata au wa kulipia matibabu, au madhara yanayosababishwa na dawa, ni mambo ambayo huongeza woga na wasiwasi. Hisia hizo zinaweza kumlemea sana mtu.

Tunaweza kupata wapi msaada? Watu wengi wametambua kwamba kumkaribia Mungu kupitia sala na kusoma mistari ya Biblia inayotia moyo huwafariji sana. Msaada mwingine huenda ukatoka kwa washiriki wa familia na marafiki, wanapokuunga mkono na kukuonyesha upendo.

MAMBO AMBAYO YAMEWASAIDIA WENGINE

Robert, aliye na umri wa miaka 58, anatoa ushauri huu: “Mwamini Mungu, naye atakusaidia kupambana na ugonjwa wako. Sali kwa Yehova. Mwambie jinsi unavyohisi. Mwombe akupe roho yake takatifu. Mwombe akupe nguvu ili uitie moyo familia yako na akuwezeshe kuwa na utulivu unapovumilia ugonjwa ulio nao.

“Inatia moyo sana washiriki wa familia yako wanapokuwa pamoja nawe unapowahitaji. Huwa ninapigiwa simu kila siku na kuulizwa, ‘Unaendeleaje?’ Marafiki kutoka sehemu mbalimbali hunitia moyo sana. Wao hunisaidia kupata nguvu, na hilo hufanya nisikate tamaa.”

Ikiwa unapanga kumtembelea mgonjwa, kumbuka jambo ambalo Linda anasema: “Bila shaka mgonjwa anatamani kuishi maisha ya kawaida kadiri awezavyo na huenda hangependa kuzungumzia ugonjwa wake kila wakati. Kwa hiyo, zungumza naye kuhusu mambo ya kawaida.”

Hivyo, tukitegemea nguvu kutoka kwa Mungu na faraja inayotolewa na Maandiko, na kupata msaada kutoka kwa marafiki na washiriki wa familia wanaotupenda, hatutakata tamaa ya maisha hata ikiwa tuna ugonjwa mbaya.

Maandiko Yanayoweza Kukusaidia

Mtegemee Mungu.

“Nilimwomba Yehova ushauri, naye akanijibu. Aliniokoa kutoka katika mambo yote yanayoniogopesha. Mtu huyo wa hali ya chini aliita, na Yehova akasikia.”​—Zaburi 34:4, 6.

Linda, aliyenukuliwa awali, anasema: “Mimi huwa simwombi Mungu anisaidie nipone. Huwa ninamwomba anipe nguvu na anisaidie kuvumilia ugonjwa nilio nao.”

Soma Neno la Mungu ili upate nguvu.

“Hakuna mkaaji atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’”​—Isaya 33:24.

Tafakari kuhusu ahadi za Mungu za wakati ujao. Ukifanya hivyo utakuwa na tumaini na utapata nguvu za kuvumilia.

Tafuta msaada kutoka kwa washiriki wa familia na marafiki.

“Rafiki wa kweli hupenda nyakati zote naye ni ndugu ambaye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.”​—Methali 17:17.

Elise, aliyenukuliwa awali, anatoa ushauri huu: “Usijitenge. Waruhusu rafiki zako wakusaidie.Nyakati nyingine huenda ukahisi uko peke yako na hata kufikiri Mungu hakusikilizi, lakini usijitenge.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki