Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/88 uku. 2
  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • JUMA LINALOANZA FEBRUARI 29
  • JUMA LINALOANZA MACHI 7
  • JUMA LINALOANZA MACHI 14
  • JUMA LINALOANZA MACHI 21
  • JUMA LINALOANZA MACHI 28
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 3/88 uku. 2

Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

JUMA LINALOANZA FEBRUARI 29

Wimbo 61 (141)

Dak. 7: Matangazo ya kwenu. Watie moyo wote wategemeze siku ya magazeti juma hili. Wapate akiba ya vitabu Creation na magazeti ya kutumia katika utumishi wa shambani wakati wa juma hili.

Dak. 18: “Wasaidie Wengine Wathamini Upendo wa Mungu.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu. Watie moyo wote wanaoweza wafanye upainia msaidizi wakati wa Machi na Aprili.

Dak. 20: Kichwa cha Mazungumzo kipya. Mazungumzo na wonyesho. Pitieni Kichwa cha Mazungumzo na kuonyesha jinsi kitabu Creation kinavyoweza kuunganishwa. Katika utangulizi kazia kwamba leo maisha ya jamaa yanatishwa kwa sababu nyingi. Kama matokeo, kuna jamaa zilizovunjika na ukosefu mwingi wa furaha. (Muulize mwenye nyumba anahisi utatuzi wa tatizo hili ni nini.) Baadaye onyesha kwamba kuna uhitaji wa kumtegemea Muumba wa aina ya wanadamu kwa mwelekezo. Mungu alianzisha mpango wa jamaa. (Soma Mwanzo 1:27, 28.) Kisha ungeweza kusema: “Wewe ulijua kwamba watu zaidi na zaidi, kutia na wanasayansi, wanaitikadi kwamba wanadamu waliumbwa? Neno la Mungu lililoandikwa, Biblia, lina mwelekezo ambao ukifuatwa unaweza kuchangia maisha ya jamaa yenye furaha na unaweza kuandaa tumaini kwa hali njema wakati ujao. (Soma Isaya 48:17, 18.) Ni jambo la muhimu kwa watu wenye unyofu wa moyo kusoma na kuelekeza fikira kwa Neno la Mungu lililoandikwa.” Toa kitabu Creation, ukionyesha kwamba kichapo hiki kinandaa ithibati inayotegemeza masimulizi ya uumbaji na kuthibitisha kwamba Mungu anataka wanaume na wanawake wapate uradhi na furaha maishani. (Zungumzia picha kwenye ukurasa 34.) Fungua sura 19 na uchague habari na picha zinazofaa kutoka kurasa 232-7, ukikazia kwamba watu wote wanaomwogopa Mungu watabarikiwa Paradiso itakaporudishwa. Kisha toa kichapo. Painia au mhubiri anayestahili atoe wonyesho kuhusu matumizi ya Kichwa kipya na kutoa kitabu Creation. Baada ya wonyesho, zungumzia habari nyingine zinazoweza kutumiwa kutoka kichapo hicho.

Wimbo 72 (135) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA MACHI 7

Wimbo 108 (200)

Dak. 7: Matangazo ya kwenu, tia moyo matumizi ya nyongeza ya Furahia Maisha. Zungumzia jinsi nyongeza ni yenye manufaa kwa mwanafunzi na umuhimu wa kufuata ratiba ya funzo iliyodokezwa.

Dak: 18: “Wasaidie Wale Wanaohudhuria Mikutano.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu. Kazia uhitaji wa kuwasaidia wapya wastahili kushiriki katika huduma ya shambani.

Dak. 12: Mazungumzo na mahojiano. Mzee azungumzia yale ambayo kundi la kwao linaweza kufanya ili kutoa msaada zaidi kwa wale wanaohudhuria mikutano, wakiwa na mradi wa kuwasaidia wawe wahubiri. Hoji wahubiri wawili au watatu, ukionyesha hasa yale ambayo wamefanya ili kuwasaidia na kuwatia moyo hawa.

Dak. 8: Sanduku la Swali. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji.

Wimbo 64 (127) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA MACHI 14

Wimbo 51 (92)

Dak. 10: Matangazo yanayofaa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu na matangazo ya kwenu. Tia ndani ripoti ya hesabu. Soma kwa uthamini shukrani za Sosaiti kwa michango yote, kutia na michango iliyotolewa kusaidia wamisionari wasafiri.

Dak. 15: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Msaada Kutoka kwa Roho ya Yehova.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu. Kazia uhitaji wa kuonyesha tunda la roho ya Yehova tunapokuwa katika huduma.

Dak. 8: Tumia Vizuri Kalenda ya Kitheokrasi. Hotuba. Watie moyo wote watumie kalenda ya Sosaiti. Andika maandishi kuhusu ratiba ya utumishi wa shambani na utendaji mwingine wa kitheokrasi. (Mhu. 3:1) Usomaji wa Biblia wa kila juma umechapishwa kwenye kalenda. Hii inatumika kama kikumbusha kusoma Biblia kila siku. (Zab. 1:2) Angalia usomaji wa Biblia wakati wa juma la Ukumbusho. Andiko la mwaka limekaziwa, na picha zinachochea tamaa yetu ya kushiriki katika huduma ya shambani. Pitia pamoja na wasikilizaji tamasha mbalimbali katika kalenda ya 1988. Pia picha zinatukumbusha udugu wetu wa ulimwenguni pote. Tumia kalenda kuwaelekeza wanafunzi wa Biblia kwenye tengenezo. Weka kalenda mahali panapofaa katika nyumba ili itumikie mahitaji ya jamaa nzima vizuri. (Angalia Huduma ya Ufalme Yetu, Mei 1983, ukurasa 1.)

Dak. 12: Waalike watu wanaopendezwa kwenye Ukumbusho. Mazungumzo na wonyesho ikitolewa na mwangalizi wa utumishi. Kazia uhitaji wa kualika washiriki wote wa jamaa, wanafunzi wa Biblia, na watu wanaopendezwa kwenye Ukumbusho siku ya Ijumaa jioni, Aprili 1. Tumieni vizuri vikaratasi vilivyochapishwa vya ukaribishaji. Panga ili mhubiri anayestahili atoe wonyesho jinsi ya kumkaribisha mwanafunzi wa Biblia kwenye Ukumbusho, kwa kutumia habari zilizo chini ya kichwa “Ukumbusho” katika kitabu Reasoning, kurasa 266-9. Mwangalizi wa utumishi anamalizia kwa kuwatia moyo wote kuandika majina ya watu tunaotaka kualika na kujitahidi katika njia ya pekee kuwafikia hao.

Wimbo 29 (11) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA MACHI 21

Wimbo 25 (151)

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Watie moyo wote washiriki katika utumishi wa shambani mwisho juma huu. Wakati unavyoruhusu, eleza kifupi kuhusu mambo yaliyoonwa katika kuangusha kitabu Creation.

Dak. 15: “Tegemeza Mipango ya Utumishi wa Katikati ya Juma.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu. Tangaza mipango ya kwenu.

Dak. 8: Matayarisho kwa ajili ya Ukumbusho. Hotuba ikitolewa na mwangalizi msimamizi. Tangaza saa ya Ukumbusha na utoe muhtasari wa mipango ya kwenu. (Angalia Huduma ya Ufalme Yetu, Machi 1987, ukurasa 4, “Mambo ya Kutayarisha.”) Taja hadhirina ya mwaka uliopita ya ulimwenguni pote na ya mahali penu na wakumbushe wote kuwafikia watu wanaopendezwa ambao hawajaalikwa bado.

Dak. 12: Je! Wewe Unaweza Kufanya Upainia Msaidizi Wakati wa Aprili? Mazungumzo. Watie moyo wote wanaoweza wafanye upainia msaidizi wakati wa mwezi wa Aprili. Hoji mhubiri mmoja au wawili ambao wamefanya mipango ya kufanya upainia. Walipanga ratiba yao jinsi gani ili watoe saa 60 katika huduma? Wao wanatazamia kupata furaha na manufaa zipi? Watie moyo wote wanaoweza wafanye kazi pamoja na mapainia na kutumia wakati mwingi iwezekanavyo katika huduma ya shambani wakati wa Aprili. Malizia kwa kutangaza kwamba Mashahidi wote waliobatizwa wapaswa kufanya jitihada za pekee kuwapo wakati wa Mkutano wa Utumishi juma lijalo.

Wimbo 47 (87) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA MACHI 28

Wimbo 110 (212)

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote kwamba Ukumbusho utafanywa Ijumaa jioni, Aprili 1. Watie moyo wahubiri watoe uandikishaji wakati wote wa Aprili. Onyesha makala halisi kutoka magazeti ambayo inaweza kuunganishwa na Kichwa cha Mazungumzo cha sasa. Toa wonyesho mfupi ukionyesha utoaji wa uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi.

Dak. 15: “Thamani ya Kuimba Katika Ibada ya Kweli.” Hotuba ikitegemea Mnara wa Mlinzi, wa Desemba 1, 1987, ukurasa 25-7. Kazia uhitaji wa wote kuimba kwa idili na kutoka moyoni.

Dak. 15: Medical Directive and Identity Card. (Mwandishi atagawanya kadi kabla ya mkutano kwa Mashahidi wote waliopo waliobatizwa.) Mwangalizi msimamizi atalisomea kundi barua ya Sosaiti ya Desemba 21, 1987, kuhusu utumizi wa kadi hizi. Atatumia habari zilizo nyuma ya barua ya Sosaiti ili kueleza waziwazi jinsi kadi zapaswa kujazwa. Mashahidi waliobatizwa ambao hawakuwa kwenye mkutano huu wanaweza kumwomba mwangalizi msimamizi kadi hizi. Akina ndugu wanatiwa moyo wajaze kadi hizo mara moja na kuhakikisha kwamba zimetiwa sahihi inavyofaa na kuandikwa tarehe.

Wimbo 118 (205) na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki