Kutangaza Habari Njema—Kwa Msaada Kutoka kwa Roho ya Yehova
1 Ili kuwa na mafanikio katika huduma ya Ufalme, tunahitaji mwelekezo na baraka ya Yehova. Ni jambo la muhimu tusali kwa ajili ya msaada wa roho takatifu katika utendaji wetu, kwa kuwa Yesu aliwahakikishia wanafunzi wake kwamba Mungu atawapa roho takatifu wale wanaoomba waipate.—Luka 11:13.
2 Wakati tunapotoa ushuhuda kwa watu wa aina fulani, huenda tukahisi uhitaji wa kujitayarisha vizuri zaidi. (Linganisha 1 Wakorintho 2:1-5.) Lakini roho ya Yehova itatusaidia ikiwa sisi tunaomba tuipate, nasi tutaweza kuutoa ukweli kwa usahihi na waziwazi.
3 Roho takatifu itatupa ujasiri unaohitajiwa ili tuwaambie “watu wa aina zote” ukweli. (1 Tim. 2:3, 4, NW; 1 The. 2:2) Bila shaka, kuwa mjasiri hakumaanishi kwamba Mkristo atakuwa mwenye uvumilivu kupita kiasi au kukaidi katika tabia yake.
KUZA TUNDA LA ROHO
4 Mtume Petro anataarifu kwamba tunapozungumza, twapasa kuwa na “upole na staha yenye kina kirefu.” (1 Pet. 3:15, NW) Upole ni tunda la roho na ni la maana sana hasa tunaposhughulika na watu wasiokubali sababu. Matunda mengine ya roho yatasaidia pia katika kushugulika na hali zenye kujaribu. (Gal. 5:22, 23) Hakuna haja ya kuona kukataliwa na wengine kuwa chuki ya kibinafsi. Badala yake, ng’amua kwamba huenda wasifahamu thamani ya ujumbe tunaopeleka. Kuwa na mwelekeo huo wa akilini kutatusaidia tuwe wapole na wenye staha. Ikiwa inafaa, sema neno lenye fadhili unapoondoka. Hili linaweza kuwa na matokeo yenye mafaa kwa watu wasio na mwelekeo mwema.—Mit. 15:1.
5 Tuwe tunafanya kazi katika huduma ya nyumba kwa nyumba au barabarani, tunatazamwa na wengine. Sikuzote mazungumzo yetu na tabia zapasa ziwe zisizochukiza na zisizoleta suto. Si kila mtu anathamini kazi yetu. Wengi hawatasikiliza. Usivunjike moyo. Kumbuka kwamba tunatafuta watu wa aina ya kondoo. (Mt. 10:12-14) Tabia zetu tukiwa katika utumishi wa shambani zapasa zimeletee Mungu heshima kwa kuonyesha tunda la roho yake. Tabia nzuri na kuwafikiria wengine huenda kukalainisha mioyo ya wengine.—2 Kor. 6:3.
6 Ikiwa mtu tunayeongea naye kwa kweli ana shughuli nyingi, huenda tukaweza kusema maneno machache tu. Lakini kuwa kwetu wenye kufikiria wengine huenda kukatokeza itikio changamfu Shahidi anapotembea wakati mwingine. Roho ya Mungu itatusaidia tuonyesha upendo wa kweli na tuwe wavumilivu na wenye fadhili. Tunafurahi kwamba Mungu kwa rehema yake mara nyingi anawapa watu nafasi nyingi ya kusikiliza, matokeo yakiwa kwamba hatimaye wengine wanaitikadi.—1 Kor. 13:4.
7 Tukiacha roho ya Mungu iongoze jitihada zetu, tutatoa ujumbe wa Ufalme katika njia ambayo inapendeza kwa watu wenye kusababu na kumwogopa Mungu. Ufanye uwe mradi wako ‘kuyapamba mafundisho ya Mwokozi wetu, Mungu, katika mambo yote.’—Tito 2:10.