Habari za Kitheokrasi
◆ Lesotho iliweza kuripoti kilele kipya cha wahubiri 1,068 katika Oktoba. Tufani ya theluji isiyo ya kawaida katika milima ilikatiza kazi ya mapainia na wahubiri wengi lakini hakuna mmoja wa ndugu zetu aliyejeruhiwa wala kufa kwa sababu ya hali hiyo yenye baridi sana.
◆ Malesia ilifurahi kuripoti kilele kipya cha wahubiri 861 katika Oktoba.
◆ Panama ilifikia kilele chao cha nne mfululizo cha wahubiri 5,138 wakiripoti, ongezeko la asilimia 8 zaidi ya wastani wa mwaka uliopita.
◆ Ureno ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri katika Oktoba, 32,202 wakiripoti. Kulikuwa na ongezeko la asilimia 21 katika hesabu ya mapainia wa kawaida kwa kulinganisha na mwezi huo huo mwaka uliopita.
◆ Thailandi ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 952 katika Oktoba.
◆ Akina ndugu katika Truk waliripoti kilele kipya cha wahubiri 55 katika Oktoba, ongezeko la asilimia 45 zaidi ya wastani wa mwaka uliopita. Kusanyiko lao la mzunguko la karibuni lilikuwa na kilele cha hadhirina 108