Habari za Kitheokrasi
◆ Australia ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 48,558 katika Oktoba. Hili ni ongezeko la 3,144 zaidi ya Oktoba uliopita.
◆ Côte d’Ivoire iliripoti kilele kipya cha wahubiri 2,926 katika Oktoba. Hesabu ya mapainia wa kawaida inaongezeka kila mwezi. Kwa sasa asilimia 18 ya wahubiri wanapainia.
◆ Saiprasi ilikuwa na kilele chao cha nne mfululizo katika Oktoba 1,168 wakiripoti.
◆ Hong Kong ilifurahi kuripoti kilele kipya cha wahubiri 1,795 na kilele kipya cha mafunzo ya Biblia 2,929 katika Oktoba. Wahubiri wa kundi walifikia wastani wa saa 16.4.
◆ Mfululizo wa mikusanyiko minane ya “Haki ya Kimungu” ilikuwa na hudhurio lililounganishwa la 17,302 na 479 walibatizwa katika Afrika Mashariki. Habari kuhusu “Kujitoa Kimungu” mkusanyiko wa wilaya wa 1989 zitatolewa kwa taratibu.
Martiniki ilikuwa na ongezeko la asilimia 7 katika Oktoba kwa kilele kipya cha wahubiri 2,598.
◆ Katika Oktoba, Swaziland ilifikia kilele kipya cha wahubiri 1,093 na kilele kipya cha magazeti 5,734. Waliongoza mafunzo ya Biblia 1,508. Kuna uwezekano mzuri sana wa ukuzi katika nchi hii ndogo.