Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/88 uku. 2
  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • JUMA LINALOANZA MEI 2
  • JUMA LINALOANZA MEI 9
  • JUMA LINALOANZA MEI 16
  • JUMA LINALOANZA MEI 23
  • JUMA LINALOANZA MEI 30
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 5/88 uku. 2

Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

JUMA LINALOANZA MEI 2

Wimbo 101 (186)

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Watie moyo wote washiriki utendaji wa magazeti Jumamosi. Toa wonyesho wa sekunde 30 hadi 60 juu ya jinsi ya kutoa magazeti ya karibuni.

Dak. 20: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Shangwe.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Kuhusiana na fungu la 3, toa wonyesho wa mhubiri aliyekomaa akisaidia mpya ili atayarishe utoaji, akitumia Kichwa cha Mazungumzo na kitabu Reasoning.

Dak. 15: “Uwe na Bidii Kwa Ajili ya Ibada Safi.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu. Kwa kuzungumzia mafungu 3 na 4, toa wonyesho wa matumizi ya Kichwa cha Mazungumzo cha sasa pamoja na toleo la fasihi (vitabu).

Wimbo 111 (206) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA MEI 9

Wimbo 100 (180)

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na ripoti ya hesabu. Tia ndani maneno ya uthamini kwa utegemezo wa kifedha wa kundi. Soma shukrani zo zote kwa michango iliyopelekwa kwa Sosaiti.

Dak. 20: “Wafunze Wanafunzi Jinsi ya Kutumia Biblia.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Baada ya kuzungumzia fungu 3, toa wonyesho mfupi mhubiri akisaidia mwanafunzi wa Biblia kupata maandiko. Elekeza kwenye orodha ya vitabu vya Biblia na eleza jinsi ya kuvitafuta. Mwonyeshe mahali ambapo Maandiko ya Kiebrania na Kigiriki yanaanzia na kumalizikia na jinsi vitabu vya Biblia vimegawanywa katika sura na mistari. Onyesha mahali Mwanzo na Ufunuo, na pia kitabu cha Zaburi vinapatikana. Wakati wa kuzungumzia fungu 5, eleza jinsi ya kutumia sehemu ya “Fahirisi ya Maneno ya Biblia.”

Dak. 15: “Je! Utoaji Wako Ni Dhabihu?” Hotuba ikitolewa na mzee, ikitegemea kurasa 28-31 za Mnara wa Mlinzi wa Desemba 1, 1987.

Wimbo 99 (118 Tunza: Kwenye ukanda au rekodi, wimbo huu una mistari miwili tu) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA MEI 16

Wimbo 74 (139)

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na mazungumzo ya Sanduku la Swali-1.

Dak. 20: “Wasaidie Watoto Wanufaike Zaidi na Mikutano.” Mwenezo wa makala kwa maswali na majibu. Tia ndani mahojiano pamoja na vijana. Wamekuwa wakijifunza nini mikutanoni na katika funzo lao la kibinafsi? Wamepata mambo yapi yaliyoonwa shambani? Onyesha thamani ya kuwaleta watoto mikutanoni na kujifunza pamoja nao vilevile kuwapeleka shambani.

Dak. 15: “Maktaba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.” Mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi anazungumzia makala pamoja na wasikilizaji, akitumia habari zinazolingana na hali za kundi la kwenu.

Wimbo 73 (157) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA MEI 23

Wimbo 58 (130)

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Fikiria habari za mazungumzo kutoka magazeti ya karibuni. Toa maonyesho mawili yaliyotayarishwa vizuri kwa sekunde 30 mpaka 60, moja likionyesha Mnara wa Mlinzi na lile jingine Amkeni! Watie moyo wote washiriki katika kutoa ushuhuda kwa magazeti Jumamosi hii.

Dak. 15: .Mahitaji ya kwenu au hotuba juu ya “Somo la Kusamehe,” kurasa 8 na 9 katika Mnara wa Mlinzi wa Machi 1, 1988. Fanya matumizi ya mahali penu.

Dak. 20: “Kufanya Mambo Yanayohitajiwa Sana Ili Kupendeza Mungu.” Eneza kwa maswali na Majibu.

Wimbo 51 (92) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA MEI 30

Wimbo 36 (65)

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Sanduku la Swali-2. Fikiria habari za mazungumzo kutoka magazeti ya karibuni. Watie moyo wote washiriki kutoa ushuhuda kwa magazeti Jumamosi hii.

Dak. 20: “‘Nendeni Mkafanye Wanafunzi!’—Je! Wewe Unafanya Hivyo?” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu. Kazia umaana wa mwelekeo unaofaa, sala yenye kudumu kwa msaada wa Yehova, kuweka jitihada ya kupata funzo, na hiari ya kutumiwa na Yehova ili kusaidia mtu fulani ajifunze ukweli. Malizia kwa wonyesho wa dakika nne wa mhubiri akimwendea mwangalizi wa utumishi na kusema kwamba anathamini madokezo ambayo yamezungumziwa hivi sasa naye atayatumia. Auliza ikiwa mwangalizi wa utumishi anaweza kumsaidia zaidi katika njia nyinginezo zote. Mwangalizi wa utumishi anaonyesha kwamba mhubiri huyo amekuwa akiangusha vichapo katika kazi ya nyumba kwa nyumba naye anauliza kama anahisi angesaidika ikiwa mtu fulani angeenda pamoja naye wakati anapofanya ziara za kurudia na kujaribu kuanzisha funzo. Mhubiri anakubali. Mwangalizi wa utumishi anamhakikishia kwamba atakuwa na furaha kufanya mipango hiyo. Pia, mwangalizi wa utumishi anapotembelea Funzo la Kitabu la Kundi lake, angependa kufanya kazi pamoja naye katika kufanya ziara za kurudia kwa jitihada ya kuwa mwenye msaada zaidi kwake. Mhubiri anaonyesha uthamini. Mwangalizi wa utumishi anadokeza kwamba mhubiri anaweza pia kuwaendea majirani, watu wa ukoo, wafanya kazi wenzi, au wanashule wenzake kwa jitihada yake ya kuanzisha funzo. Akiwaona wapya kwenye Jumba la Ufalme, anaweza kuwaendea ili aone kama wana funzo.

Dak. 15: Toleo la kitabu kwa Juni na Julai. Kiongozi wa Funzo la Kitabu la Kundi mwenye bidii anazungumzia toleo pamoja na wasikilizaji, anadokeza mambo ya kuzungumzia katika eneo la kienyeji, na anatumia dakika tano kutoa wonyesho juu ya jinsi utoaji unavyounganishwa na Kichwa cha Mazungumzo kilichodokezwa kwa ajili ya Juni.

Wimbo 34 (62) na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki