Maktaba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
1 Mtume Paulo alisihi Timotheo aendelee ‘kufanya bidii katika kusoma na kuonya na kufundisha na kutafakari juu ya yale aliyokuwa amejifunza; kukaa katika hayo; ili kuendelea kwake kuwe dhahiri kwa watu wote.’ (1 Tim. 4:13, 15) Njia moja tunayoweza kutumia onyo hili la upole ni kupitia funzo la kibinafsi na utafiti. Maktaba nzuri ya kitheokrasi inaweza kuwa yenye msaada katika kufanya hivyo. Ni vizuri kuwa na maktaba ya kibinafsi nyumbani na kuitumia. Lakini maktaba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi iliyoko kwenye Jumba la Ufalme huenda ikawa na vichapo zaidi vya kurejezea, hasa kwa wapya ambao hawana nakala za kibinafsi za vichapo vya zamani.
2 Katika 1944 makundi yalitiwa moyo kuweka maktaba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kwenye Jumba la Ufalme. Kusudi la maktaba hiyo lilikuwa kuwawezesha wanafunzi kupata vichapo vya Sosaiti na vitabu vingine vya marejezo vinavyofaa kwa ajili ya utafiti na funzo la Biblia lakini visivyopatikana kwa njia nyingine.—Mdo. 17:3.
VITABU VYA KUTIA NDANI
3 Ni vichapo gani vinavyopaswa kutiwa katika maktaba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi? Kwa kuwa kusudi yalo ni kutusaidia katika funzo la Biblia, inapasa kutia ndani vichapo vya karibuni vya Sosaiti na tafsiri mbalimbali za Biblia. Pia, kamusi nzuri inaweza kuandaliwa. (Ona Sanduku la Swali, Huduma ya Ufalme ya Juni, 1972.) Fahirisi ya Mnara wa Mlinzi ya 1930-1985, ambayo imetayarishwa kwa ajili ya utafiti na funzo, ni kifaa cha maana katika maktaba nzuri ya kitheokrasi. Hata hivyo, Majumba ya Ufalme mengi hayana vichapo vyote ambavyo vimeonyeshwa katika Fahirisi. Ili kuwezesha vingi vipatikane, Sosaiti inapanga kuchapa tena mabuku yaliyojalidiwa ya Watchtower kwa miaka 1960 mpaka 1979, katika kiingereza pekee. Hii itakuwa nyongeza nzuri kwa maktaba hizo za Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ambazo tayari hazina marejezo haya.
4 Mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ana daraka la maktaba. Huenda mtumishi wa huduma akapewa mgawo wa kusaidia kutunza maktaba hiyo. Mwangalizi wa shule anapaswa kupendezwa katika kuwasaidia wapya wajifunze jinsi ya kutumia maktaba ili wapate manufaa zaidi. Apaswa kuwa macho pia kuona kwamba vichapo vipya vinavyofaa vinaongezewa na kwamba vitabu vimeandikwa vizuri kuonyesha kwamba ni mali ya kundi. Wote wapaswa kushirikiana pamoja na mwangalizi wa shule katika kutunza maktaba na kuiweka katika hali nzuri. Ukiwa na vichapo ambavyo ungependa kuchanga kwa maktaba, basi unaweza kumjulisha mwangalizi wa shule ili ajue vile ambavyo unavyo.
IWEKENI KATIKA HALI NZURI
5 Mwangalizi wa shule atapanga kuangalia maktaba katika pindi yake ili kuona kwamba imo katika hali nzuri na kwamba vyo vyote vinavyohitajiwa kutengenezwa upya au kubadilishwa vinatunzwa. Mwe huru kutumia vichapo vyo vyote katika maktaba kabla na baada ya mikutano. Hata hivyo, vitabu vyo vyote visitolewe kwenye Jumba la Ufalme. Ikiwa kuna uhitaji wa pekee, basi jambo hilo linapaswa kuzungumziwa na mwangalizi wa shule. Wakati makundi zaidi ya moja yanakutana kwenye Jumba la Ufalme, kila kundi linapasa kuwa na maktaba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi yalo lenyewe.
6 Maktaba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi inatumikia kusudi linalofaa sana. Tunapotumia uandalizi huu kwa ajili ya utafiti, tunaweza kuwa na shangwe ya kugubua ‘hazina zilizositirika’ za Neno la Mungu ambalo linatoa maarifa, hekima, na ufahamu.—Mit. 2:4-6.