Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/88 uku. 2
  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 5
  • JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 12
  • JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 19
  • JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 26
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 9/88 uku. 2

Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 5

Wimbo 104 (175)

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yanayofaa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu na “Uandalizi kwa Ajili ya Mapainia.” Tia moyo utendaji wa magazeti kwa ajili ya siku za Jumamosi. Dokeza mambo ya kuzungumziwa kadiri wakati uruhusuvyo.

Dak. 20: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Kitabu Creation” likiwa toleo badala. Mazungumzo ya maswali na majibu. Tia ndani wonyesho mfupi juu ya jinsi unavyoweza kutolea kijana kitabu Creation. Pia fanya wonyesho mfupi juu ya mambo makuu kutoka mafungu 4-6. (Anza wonyesho baada ya kusoma andiko la mwisho katika Kichwa.) Malizia kwa maono ya kwenu juu ya kuangusha kitabu Creation.

Dak. 15: Vijana—Je! Nyinyi Mwaweza Kuongoza Funzo? Ishughulikiwe na mzee. Julisha kundi mna wahubiri wangapi walio chini ya umri wa miaka 20 na ni wangapi wa hawa ambao wanaongoza mafunzo. Zungumzia nafasi kwa ajili ya maendeleo. Matineja wangeweza kuanza mafunzo pamoja na wanadarasa wenzi, wakitumia kitabu Creation au Ujana. Unaweza kuwagawia vijana walio mifano mizuri waeleze maono. Chagua machache tu yanayoelekea kufaa zaidi. (Ona yb88 uku. 53 maf. 1-3; w84 4⁄1 uku. 30 fu. 4; yb71 uku. 150 fu. 1.) Walio wachanga zaidi wanaweza kuanzisha mafunzo pamoja na wachanga wengine katika vitabu ama Hadithi za Biblia au Mwalimu Mkuu. (Ona yb75 uku. 13 fu. 4; km 8⁄73 uku. 4 fu. 6; yb70 uku 93 fu. 2.) Vijana wanaweza kujaribu kuanzisha mafunzo na watu wanaokuta katika utumishi. (Ona wSW82 5⁄15 uku 10 fu. 7; yb71 uku. 264 fu. 2.) ikiwa maono ya kwenu yanapatikana, tumia hayo kutolea mambo vielezi.

Wimbo 73 (157) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 12

Wimbo 63 (123)

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Taja shukrani kwa michango kwa Sosaiti.

Dak. 18: “Kujiwekea Miradi ya Mwaka Mpya wa Utumishi.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Ili kuonyesha maendeleo yaliyofanywa, huenda ukataka kuuliza kama baadhi ya wasikilizaji walianza kutoa maelezo kwenye mikutano, wakaanza kuongoza mafunzo ya Biblia, wakafanya upainia msaidizi kwa mara ya kwanza, au wakachukua upainia wa kawaida wakati wa mwaka uliopita.

Dak. 15: Utendaji wa Kundi Letu. Mwangalizi Msimamizi azungumza pamoja na kundi kazi iliyotimizwa wakati wa mwaka wa utumishi uliopita. Tumieni Ripoti ya Mchanganuo wa Kundi (S-10) kuwa msingi wa kutaja mambo yaliyofanyiwa maendeleo na mambo yanayohitaji uangalifu. Unganisha mambo yanayofaa yaliyotajwa na mwangalizi wa mzunguko wakati wa ziara yake iliyopita.

Wimbo 90 (166) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 19

Wimbo 81 (165)

Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Tia moyo wote washiriki kazi ya magazeti siku za Jumamosi.

Dak. 17: “Anza Mafunzo ya Biblia—Sasa Ndio Wakati Unaofaa.” Mazungumzo ya makala pamoja na wasikilizaji. Kuhusiana na fungu la 3, mhubiri mwenye uwezo atoe wonyesho mfupi juu ya utangulizi wa pili chini ya “Mafunzo ya Biblia Nyumbani” katika ukurasa 12 wa kitabu Reasoning. Baada ya kuzungumzia fungu la 5, anza wonyesho mwingine mwenye nyumba akatae toleo kwa upole. Halafu Mhubiri auliza kama mwenye nyumba amepata kutaka kujua kama dunia itaharibiwa katika vita ya nyukilia na kuruhusu itikio. Kisha Mhubiri ajitolea kurudi azungumzie mada. Adokeza mwenye nyumba aandike chini maandiko fulani na ayasome baadaye kabla ya ziara itakayofuata. Ndugu anayeshughulikia sehemu hii apasa awe mchangamfu na mwenye idili, akiwaalika wote washiriki katika kazi ya funzo la Biblia.

Dak. 13: Tunafanyaje Katika Utendaji wa Funzo la Biblia? Mazungumzo ya utendaji wa kundi na mwangalizi wa utumishi. Toa hesabu ya mafunzo ya Biblia yanayoripotiwa. Ni chanzo cha shangwe kuona wenye kupendezwa wakiitikia ukweli. (Mdo 11:18; 15:3) Ondoa hesabu ya mafunzo ya jamaa yaliyoripotiwa kuonyesha ni mafunzo mangapi yanayoongozwa katika eneo. Linga maangusho ya magazeti na vitabu na hesabu ya ziara za kurudia zilizoripotiwa. Je! hili ni eneo ambamo mafunzo ya Biblia yangesitawishwa? Linga wastani wa hesabu ya mafunzo ya Biblia (kutia mafunzo ya jamaa) kwa kila mhubiri na wastani wa taifa. Toa kitia-moyo na kusifu ifaavyo. Mwaweza kutia ndani maono juu ya kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia.

Dak. 10: Ongozeni Mafunzo ya Jamaa. Ishughulikiwe na kichwa cha jamaa anayestahiwa. Kumbusha wazazi daraka lao walilopewa na Mungu. (Efe. 6:4) Madokezo yenye msaada yanatolewa katika Mnara wa Mlinzi, Agosti 1, 1986, ukurasa 28, na Novemba 1, 1986, ukurasa 24. Eleza jinsi funzo la jamaa la watoto wasiobatizwa linavyoweza kuripotiwa. (kmSW 7⁄83, Sanduku la Swali, fu. 2) Hoji mzazi ambaye amekuwa na matokeo mazuri kutokana na kujifunza kwa ukawaida na watoto wake.

Wimbo 84 (168) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 26

Wimbo 76 (143)

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Jitayarishieni toleo la andikisho linaloanza mwisho-juma ujao. Toa wonyesho wa kuunganisha toleo na Kichwa cha Mazungumzo. Tia wote moyo watoe maandikisho katika Jumapili ya kwanza ya mwezi.

Dak. :10: Shangwe za Kupainia. Hoji baadhi ya mapainia wa kawaida ambao wamekuwa kwenye Shule ya Utumishi wa Painia juu ya jinsi shule hiyo ilivyowanufaisha. (Ikiwa hakuna mapainia wa kawaida kundini ambao wamekuwa kwenye shule, mwaweza kuomba maono ya shambani kutoka kwa mapainia au wale ambao wamefanya painia msaidizi karibuni.)

Dak. 13: “Ripoti Utumishi wa Shambani kwa Usahihi.” Mwandishi wa kundi ashughulikie mazungumzo pamoja na wasikilizaji.

Dak. 10: Mahitaji ya kundi lenu au hotuba juu ya “Kuwa Mhudumu Aliyeagizwa Rasmi—Kwa Njia ya Mungu!” kutoka Mnara wa Mlinzi wa Juni 15, 1988, kurasa 28-31.

Wimbo 112 (207) na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki