Anza Mafunzo ya Biblia—Sasa Ndio Wakati Unaofaa
1 Wakati wa 1987 wastani wa hesabu ya mafunzo ya Biblia yaliyoongozwa ulikaribia kulingana na jumla ya wahubiri ulimwenguni pote. Ni uwezekano mzuri ajabu kama nini wa ongezeko katika watangazaji wa Ufalme! Je! wewe unashiriki katika upande huu wa kazi ya kufanya wanafunzi? Sasa kwa kuwa wengi wamerudi kutoka likizo ya wakati wa kiangazi, ndio wakati unaofaa kukazia fikira kuanzisha mafunzo.—Linganisha 2 Wakorintho 6:2, NW.
2 Kitabu Huduma Yetu, kurasa 90-91, hukazia juu yetu pendeleo letu la kusaidia wengine kiroho kwa njia ya mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Ukurasa 91 huchagiza hivi: “Ikiwa inawezekana, zaidi ya funzo lo lote ambalo huenda unaongoza pamoja na watoto katika jamaa yako, fanya iwe shabaha yako kuongoza angaa funzo moja la Biblia la nyumbani kwa ukawaidi.” Huu ni mradi mzuri ambao sisi sote tunaweza kujitahidia kwa kutolea mwenye nyumba funzo la Biblia katika kila fursa.
KWA MSAADA WA KITABU REASONING
3 Je! wewe umejaribu kutolea mwenye nyumba funzo la Biblia katika ile ziara ya kwanza? Kwenye ukurasa 12 chini ya “Funzo la Biblia la Nyumbani,” kitabu Reasoning hudokeza matangulizi mawili ambayo huchukua njia hii ya moja kwa moja. Hayo hujulisha mwenye nyumba kwamba kusudi la ziara yetu ni kumtolea funzo la Biblia la nyumbani la bure. Si kitu utoaji wetu uwe nini, sisi tunaweza kujitolea tuonyeshe jinsi funzo huongozwa. Wengi wa wenye nyumba wana baadhi ya vitabu vyetu ambavyo vinaweza kutumiwa. Au trakti inaweza kutumiwa kuwa msingi wa kuanzisha funzo. Hili linaweza kufanywa hata wakati toleo la kitabu limekataliwa, ikiwa inaonekana kuwa inafaa na mwenye nyumba anakubali. Mathalani, tunapotoa kitabu Creation, huenda mtu akasema yeye hapendezwi na uumbaji na mageuzi. Basi sisi tunaweza kumwonyesha jinsi sisi tunavyoongoza funzo la Biblia kwa kutumia sura ya 19 ya kitabu Creation, “Paradiso ya Kidunia Yaja Karibuni.” Ikitegemea upendezi wa mtu huyo, sisi tungeweza kuchagua habari inayofaa kutoka sura 16 kufika 20.
4 Njia nyingine ya kuanza mafunzo inahusu kutumia kitabu Reasoning wakati wa ziara za kurudia. Wakati wa kufanya mipango ya kurudia mtu mwenye kupendezwa, zusha swali, “Je! sayari Dunia itaharibiwa katika vita ya nyukilia?” Kisha badala ya kumwambia mwenye nyumba kwamba jibu litatolewa urudipo, mwagize aandike marejezo matatu au manne ya Maandiko kutoka kurasa 112 na 113 za kitabu Reasoning. Mkaribishe mwenye nyumba asome maandiko hayo katika kujitayarishia ziara yako itakayofuata. Rudi upesi iwezekanavyo katika juma ilo hilo, na kuangalia yale maandiko pamoja. Zungumzieni jinsi kila andiko linavyohusiana na swali lililozushwa. Halafu zusha swali jingine ambalo litajibiwa kwenye ziara inayofuata. Mara nyingine tena mpe mwenye nyumba maandiko kadhaa ayaangalie kabla ya wewe kurudi.
5 Ni vizuri kumwonyesha huyo mtu mwenye kupendezwa kwamba unapata habari yako kutoka kitabu Reasoning. Baada ya wakati uangalifu wake unaweza kuelekezwa kwenye kitabu Kuishi Milele kwa ajili ya funzo la Biblia la nyumbani la kawaida. Kama unavyoweza kuona, njia hii ni yenye matokeo hata ikiwa mwenye nyumba hakukubali kitabu mwanzoni lakini huonyesha hangaiko juu ya hali za ulimwengu na anataka kujua wakati ujao una nini.
6 Weka akilini maneno ya Yesu kwa wanafunzi wake kwenye Mathayo 28:19, NW: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi.” Je! wewe ungetaka kushiriki katika kazi hii ya kuokoa uhai kwa kuongoza funzo la Biblia la nyumbani? Hata kama wewe tayari unaongoza moja, je! una nafasi katika ratiba yako kwa ajili ya jingine moja au mawili? Fanya kuanzisha mafunzo jambo la kufikiriwa kwa sala huku wewe ‘ukinunua wakati.’—Efe. 5:15, 16, NW.