Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/88 kur. 1-2
  • Kujiwekea Miradi ya Mwaka Mpya wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujiwekea Miradi ya Mwaka Mpya wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MIRADI UNAYOWEZA KUFIKIRIA
  • Vijana—Miradi Yenu ya Kiroho Ni Ipi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Jinsi Unavyoweza Kufikia Miradi Yako ya Kiroho
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Tumia Miradi ya Kiroho ili Kumtukuza Muumba Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Ninaweza Kufikia Miradi Yangu Jinsi Gani?
    Amkeni!—2010
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 9/88 kur. 1-2

Kujiwekea Miradi ya Mwaka Mpya wa Utumishi

1 Je! wewe una furaha kwa sababu ya mambo ya kiroho uliyotimiza? Ni vizuri kuendelea kusonga mbele kiroho, lakini jambo hilo linahitaji jitihada. Kuweka miradi kwa ajili yetu sisi wenyewe na kwa ajili ya jamaa zetu kunasaidia. Mradi ni mwisho ambao kwa huo jitihada zinaelekezwa. Ili kumpendeza Yehova, miradi yetu lazima ipatane na mapenzi yake. Kwa hiyo, sisi hufanya kufikiri kwa Yehova kuwe kwetu sisi wenyewe na kufuatia miradi ya kitheokrasi, kama alivyofanya Yesu. (Yohana 17:4) Hivyo sisi tutapata shangwe kubwa na utoshelezo katika maisha yetu ya utumishi kwa Yehova.—Yohana 15:10, 11.

2 Umeweza kutimiza miradi gani katika kuendeleza masilahi ya Ufalme wakati wa mwaka wa utumishi uliopita? Uhakika wa kwamba wengine walifikia miradi waliyokuwa wamejiwekea unaweza kuonwa katika hesabu ya wale waliobatizwa. Pia, makumi ya maelfu walijiandikisha kuwa mapainia wasaidizi na wa kawaida. Hesabu fulani walipanga kutumikia mahali ambako uhitaji ni mkubwa. Baadhi ya akina ndugu walifikia mradi wa kibinafsi walipoalikwa kwenda Gileadi, Betheli, au kwenye Shule ya Mazoezi ya Kihuduma.

MIRADI UNAYOWEZA KUFIKIRIA

3 Je! kuna miradi inayofaa ambayo unaweza kuifikia? Ili wapya wafanye maendeleo ya kiroho, kuwa wa kawaida katika uhudhuriaji wa mikutano na kujiunga na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ingekuwa miradi mizuri. Ikiwa wewe hukuwa ukitoa maelezo kwenye mikutano kwa ukawaida, sababu gani usiufanye huo kuwa mradi. Wengine wanaweza kunufaishwa na funzo na utafiti wako, na uelewevu wako wa kushika ukweli utaimarishwa.—Waebrania 10:24, 25.

4 Je! wewe umehitimu kuanza kushiriki katika huduma ya shambani? Je! unafanya hivyo kwa ukawaida? Je! unasoma vichapo vipya vinapotokea, ili kwenda samba samba na maagizo mazuri kutoka kwa mtumwa mwaminifu? Ikiwa wewe tayari umefikia miradi hiyo, basi wakfu na ubatizo haingekuwa miradi inayofaa kufikiriwa na wewe?

5 Je! wewe unaongoza funzo la Biblia? Je! umesali upate msaada katika kuanzisha moja? Je! umefuatilia kwa bidii-endelevu ziara za kurudia, ukijitolea kujifunza na watu wenye kupendezwa unaokuta? Ikiwa mtu fulani unayejifunza naye anastahili kushiriki katika utumishi wa shambani, je! wewe unamzoeza katika huduma?

6 Je! wewe umeweka mradi wa saa kwa kila mwezi? Au umejaribu utumishi wa painia msaidizi? Pengine wewe hata uko katika hali ya kuanza utumishi wa painia wa kawaida, kushiriki zile habari njema pamoja na wengine saa 90 kila mwezi. Kwa wakati, wewe huenda ukawa na shangwe ya kupokea manufaa za mazoezi ya pekee zinazoandaliwa katika Shule ya Utumishi wa Painia. Akina ndugu wapaswa kuwa wakifikilia mapendeleo ya kutumikia wakiwa watumishi wa huduma na wazee.—1 Tim. 3:1.

7 Ile miradi ya kibinafsi tunayojiwekea sisi wenyewe yapasa itulete karibu zaidi na Yehova na kuturuhusu kushiriki kwa ukamili zaidi katika kufanya penzi lake. Paulo alisema kwamba yeye ‘alikuwa akisahau mambo yaliyo nyuma na kujinyoosha kufikia mambo yaliyo mbele.’ Yeye alitutia moyo tuwe na mwelekeo chanya wa akili juu ya mafuatilio ya kitheokrasi ili kwamba “kwa kadiri tulivyofanya maendeleo,” sisi ‘tungeweza kuendelea kutembea kwa utaratibu katika kawaida ii hii.’—Flp. 3:13, 16, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki