Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/88 uku. 4
  • Kutangaza Habari Njema—Kwa Kitabu Creation

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutangaza Habari Njema—Kwa Kitabu Creation
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Saidia Wengine Wathamini Muumba Wetu Mtukufu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Kuwasaidia Wengine Wamheshimu Mfanyi Wetu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Msifu Mungu wa Uumbaji
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Mheshimu Muumba wa Vitu Vyote
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 9/88 uku. 4

Kutangaza Habari Njema—Kwa Kitabu Creation

1 Ithibati ni tele kwamba kuna Muumba na kwamba yeye anapendezwa na uumbaji wake. (Rom. 1:20, 21) Funzo letu la Neno la Mungu limetusadikisha kupita kivuli chochote cha shaka kwamba mwanadamu alikuja hapa kwa uumbaji, wala si kwa mageuzi. (Ufu. 4:11) Wakati wa Septemba sisi tuna fursa ya kuelekeza uangalifu wa wengine kwenye ukweli juu ya uumbaji tunapotoa kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation?

2 Kuongezea huduma yetu ya kawaida ya nyumba kwa nyumba, sisi tunaweza kutoa kitabu Creation tunapofanya kazi ya barabarani na tunaposhuhudu vivi hivi. Ni kitabu chenye kuvutia ambacho kinaweza kuvutia wauza-bidhaa na wanabiashara, na wengine ambao mara kwa mara tunakuwa na shughuli nao. Kisha kuna wale tunaopelekea magazeti kwa ukawaida. Je! wao hawangefurahia kusoma kichapo hiki kizuri? Pia huenda kuwa na watu tunaotembelea au tunaojifunza nao ambao bado hawana kitabu hiki lakini ambao wangethamini kukisoma.

3 Vijana kundini, nyinyi mna eneo lenu wenyewe ambalo katika hilo mnaweza kushiriki kichapo hiki kizuri, na eneo hilo ni shule. Je! wewe umejaribu kuchukua tu pamoja nawe nakala ya kitabu Creation? Watu ambao ni wadadisi huenda wakauliza maswali na kukupa fursa ya kuwaonyesha kitabu hicho. Ukichukua kimoja pamoja nawe shuleni na kukiacha kinapoweza kuonekana juu ya dawati au kusoma kisehemu chacho unapokuwa katika chumba cha kulia chakula cha mchana, huenda ukaona wengine wakiuliza jinsi wao wanavyoweza kupata nakala. Bila shaka, nje ya saa za shule, unaweza kuchukua hatua ya kwanza na kuonyesha wengine kitabu hiki, uongee nao juu yacho, na kuwatolea nakala kwa mchango wa kawaida.

4 Sisi sote tunaweza kuwa tumeamka kuona fursa za kutoa kichapo hiki kwa vijana tunaokuta katika utumishi. Tunapokuta wazazi mlangoni, baada ya kuzungumzia Kichwa cha Mazungumzo, tunaweza kutoa kitabu hicho kikiwa toleo la badala na kueleza jinsi kitakuwa chenye msaada kwa watoto wao. Kwa kuwa mageuzi hufundishwa katika shule, kitabu hicho kitasaidia watoto wao waelewe mambo ambayo Biblia na sayansi ya kweli husema juu ya uumbaji.

5 Kuna watu wengi wenye umri mkubwa zaidi ambao hawaitikadi katika mageuzi na ambao huenda wasipendezwe hususa na mada hiyo. Lakini kwa kawaida wanahangaikia kuteseka wanakoona katika ulimwengu na huenda wakataka kujua kama kuna tumaini lolote kwa wakati ujao. Kwa watu kama hao, tunaweza kukazia sura ya 16 au ya 19.

6 Ikiwa mwenye nyumba anazusha swali juu ya itikadi katika Biblia, unaweza kutaja kwamba sura za 17 na 18 zitajibu swali “Je! Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia?” na “Biblia—Je! Kwa Kweli Imevuviwa na Mungu?” Yaliyomo katika sura hizo huenda yakawa ndiyo hasa anayohitaji ili kurudisha imani yake katika Biblia kuwa kitabu cha ukweli.

7 Sisi tunataka watu wengi zaidi iwezekanavyo wathamini kwamba Yehova ndiye Muumba. (Mdo. 17:24-28) Kwa hiyo tutafanya vizuri kumtolea kila mmoja fursa ya kupata na kusoma Life— How Did Get Here? By Evolution or by Creation?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki