Ripoti Utumishi wa Shambani kwa Usahihi
1 Upesi sasa Kitabu cha Mwaka kipya kitakuja kikiwa na ripoti ya ulimwenguni pote ya mwaka wa utumishi wa 1988. Sisi tunangojea kwa hamu nyingi kupokea kichapo hiki ili tuweze kusoma mambo ya karibuni zaidi yaliyotimizwa katika utendaji wetu wa kuhubiri kotekote duniani. (Isa. 60:22) Kwa kuwa wahubiri wote wanachangia ripoti hii ya kila mwaka, sisi tukiwa mmoja mmoja tunaweza kufanya nini kuhakikisha kwamba ni sahihi?
2 Kwenye Mathayo 24:14 tunasoma juu ya utume wetu kuhubiri katika siku za mwisho za mfumo huu. Sisi tunaweza kuonyesha staha kwa mpango wa Yehova wa kitengenezo na kuonyesha uthamini wetu kwa ajili ya sehemu ndogo tuliyo nayo kwa kuripoti utumishi wetu wa shambani kwa kudhamiria kila mwisho wa mwezi. Je! wewe unaripoti utumishi wako kwa ukawaida na kwa usahihi?
MAMBO YA KURIPOTI
3 Saa nzima nzima ndizo zapasa kuripotiwa kwa kundi. Saa isiyo kamili yaweza kutiwa ndani ya ripoti ya mwezi ujao ya mhubiri. Kwa minajili ya usahihi, ni bora kuandika wakati uliotumiwa, vitabu vilivyoangushwa, na hesabu ya ziara za kurudia zilizofanywa kila wakati tunapokwenda nje katika utumishi wa shambani. Kikaratasi cha Ripoti ya Utumishi wa Shambani kinachotolewa na kundi hufanya iwe rahisi kuweka rekodi hii.
4 Usisahau kwamba ziara ya kurudia yapasa ihesabiwe kila wakati unapoongoza funzo la Biblia. Mwishoni mwa mwezi, kikaratasi cha Ripoti ya Funzo kwa ajili ya kila funzo la Biblia lililoongozwa chapasa kujazwa na kurudishwa pamoja na kikaratasi chako cha Ripoti ya Utumishi wa Shambani. Baada ya kujaza kila kikaratasi cha Ripoti ya Funzo kabisa na kwa usahihi, jumla ya hesabu ya mafunzo ya Biblia tofauti-tofauti yaliyoongozwa wakati wa mwezi yapasa iandikwe katika kisanduku kinachofaa kwenye kona ya chini ya mkono wa kulia ya kikaratasi cha Ripoti ya Utumishi wa Shambani.
5 Inaonekana inafaa kutia ndani kikumbusha kwamba wakati wako wa utumishi wa shambani wapasa kuanza unapoanza kazi yako ya ushuhuda na kumalizika unapomaliza ziara yako ya mwisho katika kila pindi yako ya kushuhudu. Hivyo, wakati unaochukuliwa kwa ajili ya viburudisho au milo wakati wa pumziko la kuacha utumishi wa shambani haungehesabiwa kuwa utendaji wa utumishi wa shambani. Wale wanaotoa hotuba za watu wote wanaweza kuhesabu wakati uliotumiwa hasa kutoa hizo. (Ona Huduma Yetu, ukurasa 104, fungu 1.) Kwa kuwa wenye kudhamiria katika kuripoti utumishi wa shambani wetu, sisi tutachangia ripoti sahihi inayochapwa katika Kitabu cha Mwaka.
6 Kwa kuwa mwandishi lazima apelekee Sosaiti ripoti ya utumishi ya kundi kufikia tarehe 6 ya mwezi unaofuata, inaweza kuonwa kwa urahisi kwa nini ni jambo la maana kwa kila mhubiri kurudisha ripoti yake ya utumishi wa shambani mara mwishoni mwa mwezi. Kwa kufikiria mpango huu, kila mhubiri atataka kufuata mwelekezo huu kwa uangalifu. Mwandishi ana siku sita tu ambazo katika hizo anakusanya ripoti zote pamoja, kuzijumlisha, na kutuma ripoti ya kundi ili Sosaiti iipokee kwa wakati ili kutia pamoja na utendaji wa utumishi wa shambani wa makundi mengine zaidi ya 260 katika Afrika Mashariki.
7 Kila mhubiri anayeshirikiana kwa nia na mpango huu wa kitengenezo anaweza kutosheka kwa kujua kwamba amechangia kufanya ripoti sahihi ya utendaji wa ulimwenguni pote wa Mashahidi wa Yehova. (Linga Ezekieli 9:11.) Sisi sote na turudishe ripoti za utumishi wa shambani ambazo ni sahihi na kwa wakati!