Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/89 uku. 1
  • Je! Unajizoeza Mambo Uliyojifunza?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Unajizoeza Mambo Uliyojifunza?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Habari Zinazolingana
  • Watu Waliosafishwa kwa Ajili ya Kazi Zilizo Bora
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Uwe Safi Katika Akili na Mwili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Mungu Anawapenda Watu Walio Safi
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Je! Wewe Unabaki Ukiwa Safi Katika Kila Jambo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 4/89 uku. 1

Je! Unajizoeza Mambo Uliyojifunza?

1 Ilikuwa furaha jinsi gani kuhudhuria siku nne zote za “Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wetu! Kweli kweli, kila siku programu ilijaa kitia-moyo na madokezo yenye kutumika juu ya jinsi ya kudhihirisha haki ya Kimungu na uadilifu kwa kiwango kikubwa. Kwa kuwa sasa umerudi nyumbani kwenye kawaida yako ya utendaji, je! ‘unajizoeza mambo uliyojifunza, kusikia na kuona yakionyeshwa’? (Flp. 4:9) Litakuwa jambo lenye mafaa kupitia mambo makuu fulani kutoka programu ya mkusanyiko.

2 Kumbuka hotuba “Ongoza Maisha Yenye Kusawazika Sahili (Rahisi)” iliyotolewa Alhamisi alasiri. Hii ilitegemea shauri la Yesu kwenye Mathayo 6:19-33. Je! umefikiria kwa uzito mambo unayoweza kufanya ili ujiondolee mambo yasiyohitajiwa sana, ukiruhusu wakati zaidi kwa funzo, kutayarisha mikutano, na kusaidia wengine? Unaweza kufanya marekebisho gani kibinafsi ili uongoze maisha rahisi yaliyo na vivuta-fikira vichache na kujihusisha zaidi katika mambo ya kiroho? Kutafuta Ufalme wa Mungu kwanza na uadilifu wake kunapunguza wasiwasi na kuongeza shangwe yetu maishani.

3 Uhitaji wa kunufaika kutokana na mazoezi yote ambayo Yehova anaandaa kupitia Neno lake na tengenezo kulikaziwa katika sehemu “Kubali Nidhamu na Kuwa Mwenye Hekima.” Sehemu moja ambamo huenda wengine wakahitaji kuelekezea fikira hasa ni kutakasa na kufanyia maendeleo huduma yao. Je! tunatumia kwa ukawaida Kichwa cha Mazungumzo kilichodokezwa, tukimhusisha mwenye nyumba katika mazungumzo ya Biblia? Au tunaridhika na utoaji mfupi wa magazeti? Je! tunatumia shauri na madokezo kuhusu kutumia kitabu Reasoning, kufuatia kupendezwa, na kuongoza mafunzo ya Biblia?—Mit. 8:33.

4 Programu ya Ijumaa ilitia ndani hotuba yenye kichwa “Uwe Safi Katika Akili na Mwili.” Haki ya Kimungu inahitaji watu wa Mungu wawe safi kiroho, kiadili, kiakili, na kimwili. (2 Kor. 7:1) Je! ‘unajizoeza uliyojifunza’ katika habari hii ya maana? Jinsi gani? Tutadumisha usafi wa kiroho kwa kujiweka mbali na dini chafu za ulimwengu huu na kutoka kwa waasi-imani. Kutia akili nidhamu kunahitajiwa ikiwa tutaepuka tabia za kuwaza kuchafu au kufurahia tamaa mbaya za kingono, zinazoongoza kwenye uchafu wa kiakili na kiadili. (Ayu. 31:1, 9-11) Je! umechukua hatua thabiti ili kuepuka sinema, vipindi vya Televisheni, au vifaa vya kusoma ambavyo vina uvutano wenye kufisidi juu yako au wale waliomo katika jamaa yako? Ilionyeshwa pia kwamba wengine wameachilia uchafu wa kimwili na usafi nyumbani. Ikiwa wowote wana udhaifu katika sehemu hii, hakika marekebisho yanaweza kufanywa katika tabia za kibinafsi ili kuhakikisha usafi wa kimwili. Kila mshiriki wa jamaa anahitaji kushiriki katika kudumisha usafi na utaratibu wa jamaa. Hasa wakati wa kumwakilisha Yehova katika huduma tungetaka kuchana nywele vizuri na kuvaa nguo zilizo nadhifu, safi na kuonekana kuwa zenye kiasi. Hivyo tunastahi Mungu wetu Mtakatifu.—1 Pet. 1:14-16.

5 Matoleo ya wakati ujao ya Huduma ya Ufalme Yetu yatatukumbusha pande nyingine za muhimu za haki ya kimungu ambazo tulijifunza juu yazo kwenye mkusanyiko wetu. Jambo hili litakuwa lenye msaada kwa wote tunapojizoeza kanuni hizi za haki katika maisha yetu ya kila siku na katika huduma yetu. Tofauti na wengi katika Jumuiya ya Wakristo wanaosikiliza ujumbe wa Biblia kwa upendezi lakini hawautendi, tunapata furaha nyingi na manufaa ya kibinafsi kwa kuwa “watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu.”—Yak. 1:22-25; Eze. 33:32.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki