Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/89 uku. 7
  • Kutumia Kinga Zetu Kikamili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutumia Kinga Zetu Kikamili
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MADARAKA YA WAZAZI
  • WATOTO—YEHOVA ANATAZAMIA NINI KUTOKA KWENU?
  • Jinsi ya Kuwalinda Watoto Wako Kupitia Hekima ya Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Wazazi—Wasaidieni Watoto Wenu Wampende Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha​—Sehemu ya 2
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Kufurahisha Mioyo ya Wazazi Wako
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 4/89 uku. 7

Kutumia Kinga Zetu Kikamili

1 Shetani anashambulia jamaa leo, akifanya yote yote awezayo ili aziharibu. Wakristo wanajua jambo hili vizuri sana. Lingekuwa jambo lenye kuhuzunisha sana watoto wakihusika katika ukosefu wa adili katika ngono, ulevi, matumizi mabaya ya dawa za kulevya, na kutenda makosa mengine! Wengine wameona wana au binti zao wakipeperuka mbali na Yehova kihalisi, wakinaswa katika kuwaza na tamaa za ulimwengu. (Mit. 10:1; 17:21) Wakati ule ule, vijana wengi wamebaki wakiwa safi na wamejishughulisha katika utumishi wa Yehova. Mwenendo wao umeletea Mungu staha na shangwe kwa wazazi wao na wengine. (3 Yoh. 3, 4) Ni nini kimefanyiza tofauti? Katika visa vingi ni kupiga moyo konde kwa wazazi na watoto vilevile kutumia kikamili kinga zilizoandaliwa.

2 Kwenye “Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya, fikira zilielekezwa kwenye kinga ambazo wazazi na watoto wanahitaji leo. Nyingine zazo zilishughulikiwa katika mazungumzo-mfululizo “Kutoa Nidhamu kwa Uadilifu Katika Jamaa” na hotuba “Usafi wa Kiadili Ndio Uzuri wa Ujana.” Je! unakumbuka habari hii na umeitumia kibinafsi na katika jamaa yako?

MADARAKA YA WAZAZI

3 Kinga ya maana sana ni akina baba waelewe kikamili matakwa ya Yehova kwa kichwa cha jamaa na kutambua uhitaji wa kumtegemea Yehova kwa mwongozo. Kwanza lazima kichwa cha jamaa ajue kanuni za Biblia ili afunze jamaa yake. Lakini kujua tu hakutoshi. Ikiwa jamaa itapata manufaa kamili lazima kanuni hizi zitumiwe. Baba aliyejiweka wakfu apasa kuongoza jamaa katika programu ya kiroho ya sala, funzo, na utumishi mtakatifu. (1 Tim. 5:8) Ikiwa atatazamie mke wake na watoto watii mamlaka yake, lazima aonyeshe shangwe katika utii wake kwa Mungu na tengenezo lake. (1 Yoh. 5:3) Baba anapotii Yehova kwa kushughulika na jamaa yake katika njia yenye uchangamfu, upendo na uthabiti, wanamstahi, nao wataelekea kufuata kielelezo chake zaidi. Hii itamletea Yehova sifa na heshima.

4 Je! unakumbuka sehemu ya mkusanyiko yenye kichwa “Wazazi—Rekebisheni Mafundisho Mfikie Watoto Wenu”? Ilitia ndani onyesho likionyesha jamaa ikijifunza makala kutoka toleo la Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 1987. Wazazi walimfikiria kila mtoto na kiwango cha uwezo wake wa kujifunza. Halikuwa lenye kushikilia mno kawaida fulani ya maswali na majibu, lakini wazazi walikusudia kufikia mioyo ya watoto wao kwa ukweli. Nyinyi akina dada mnaweza kukumbuka hasa vile mama alivyomuunga mkono sana mume wake, hiyo ikionyesha kutii ukichwa na hivyo kuwekea watoto kielelezo kizuri.—Efe. 5:21-24.

WATOTO—YEHOVA ANATAZAMIA NINI KUTOKA KWENU?

5 Kama vile wazazi wenu wanashambuliwa na Shetani, ndivyo na nyinyi. Kinga yenu ni nini? Utii kwa Yehova na wazazi wenu. Katika hotuba za mkusanyiko, madokezo mazuri yalitolewa yawasaidie. Je! mnayakumbuka? Jambo moja ambalo huenda mkakumbuka ni kwamba hamwezi kuingia katika ulimwengu mpya kwa sababu ya matendo mema ya wazazi wenu. Yaani, lazima mfanye ukweli uwe wenu. Wazazi wenu wanawalisha na kuwategemeza. Wamekuwa wakifanya hivyo kwa miaka mingi. Lakini mnapoendelea kukomaa, inatazamiwa kwamba mtashika madaraka ya kiroho. Yehova anatazamia mfanye kile mnachojua kuwa sawa. (Mhu. 11:9) Ikiwa mmejifunza kwamba njia ya Yehova ni sawa, basi ni juu yenu kuwa na busara ya kuifuata.

6 Mnapoendelea kukua wenye umri mkubwa, mwito wa ushindani wa kubaki mkiwa safi kiadili unakuwa wenye kudumu zaidi. Kuna tauni ambayo imeenea ulimwenguni pote ya uvutano mchafu, na mnakabiliana nao kila siku. Kinga yenu inategemea kupenda yale mnajua kuwa mema na kuchukia mabaya. (Zab. 52:3; 97:10) Shirikini na wale wanaopenda Yehova. Someni mambo yanayojenga. Tazameni mambo yanayofaa. (Flp. 4:8) Mkishawishwa, kumbukeni matokeo ya mwanamume kijana akiwa na tamaa. (Mit. 7:6-27) Mwelekezwe na Yehova katika mawazo na matendo yenu, na mtabaki upande wake kwa usalama.

7 Ndiyo, wazazi na watoto pia lazima waendelee kuwa macho kuhusu hatari zinazotuzunguka sisi sote. Kwa kutumia kinga zetu kikamili, tunaweza kuwa washindi vitani na kupendelewa kusifu Yehova milele.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki