Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
ANGALIA: Huduma ya Ufalme Yetu haitaonyesha Mkutano wa Utumishi kwa juma linaloanza Desemba 19, hiyo ikiruhusu juma lililo wazi kwa ajili ya kuhudhuria “Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya. Mkutano wa Utumishi kwa juma linaloanza Desemba 26 utapangwa ili uruhusu dakika 10 kwa ajili ya matangazo ya kwenu na dakika 35 za pitio la mambo makuu katika programu ya mkusanyiko. Makundi ambayo yana mikusanyiko mapema yatarekebisha ratiba yayo na kuingiza ndani Mikutano ya Utumishi iliyoonyeshwa kwa kupatana na hali. Katika njia hiyo habari yote katika Huduma ya Ufalme Yetu kwa Desemba na Januari itazungumzwa. Wahubiri wanapaswa walete toleo linalofaa la Huduma ya Ufalme Yetu kwenye Mkutano wa Utumishi kwa majuma yanayohusika. Mapitio ya siku kwa siku ya programu ya mkusanyiko yanaweza kugawiwa ndugu wanaostahili wawili au watatu kimbele. Mapitio haya yaliyotayarishwa vizuri yatawasaidia akina ndugu kukumbuka mambo ya msingi kwa matumizi ya kibinafsi na matumizi ya shambani. Mambo yoyote yaliyoonwa yatakayotumiwa au maelezo kutoka kwa wasikilizaji yapaswa yawe mafupi na yenye kuonyesha mambo yaliyo ya maana.
JUMA LINALOANZA OKTOBA 31
Wimbo 20 (46)
Dak. 10: Matangazo yaliyochaguliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu na matangazo ya kwenu. Watie moyo wote washiriki katika kutoa ushuhuda Jumamosi na Jumapili. Sihi vichwa vya jamaa wafanye kazi pamoja na mke na watoto.
Dak. 20: “Watie Moyo Wengine Wasome na Kujifunza Neno la Mungu.” Mzee ashughulikie sehemu hii kwa maswali na majibu. Wakati wa kuzungumzia fungu 6, toa onyesha lililofanyiwa mazoezi vizuri ukitumia mojapo matangulizi yanayodokezwa pamoja na Kichwa cha Mazungumzo.
Dak. 15: Uwe Tayari Kupendekeza New World Translation. Mzee ambaye ni mwenye matokeo mazuri shambani anakazia sehemu zinazofaa za habari iliyo kwenye kurasa 276-80 ya kitabu Reasoning. Waalike wasikilizaji wakufuate na kushiriki mazungumzo ya habari ambazo zinaweza kuwa zenye msaada katika eneo la kwenu chini ya “New World Translation.” Ikiwa kitabu Reasoning hakipatikani mnaweza kutumia habari kutoka Huduma ya Ufalme Yetu ya Januari 1982, ukurasa 4.
Wimbo 62 (113) na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA NOVEMBA 7
Wimbo 85 (158)
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Zungumzia utoaji unaofaa wa magazeti ya karibuni, na tia moyo wote washiriki kazi ya magazeti Jumamosi au siku ya soko inayofuata.
Dak. 20: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Watoto.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Baada ya fungu 5, mhubiri mwenye uwezo atoe onyesho akirekebisha Kichwa cha Mazungumzo cha sasa anapozungumza na kijana. Fasihi inaweza kutolewa jinsi gani? Mazungumzo yanaweza kumalizwa jinsi gani bila kutoa fasihi?
Dak. 15: “Kuiga Yehova kwa Kuzoea Haki.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu. Baada ya kuzungumzia fungu 6, toa onyesho kuhusu njia moja au mbili za kutoa ushuhuda wa vivi hivi wakati wa kusafiri au wakati wa kuhudhuria mikusanyiko. Tia ndani mambo mafupi yaliyoonwa yanayofaa kutoka kwa wasikilizaji wakati ukiruhusu.
Wimbo 119 (222) na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA NOVEMBA 14
Wimbo 64 (127)
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Julisha kundi shukrani zozote zilizopokewa kutoka kwa Sosaiti kwa ajili ya michango. Mwangalizi wa utumishi arudie ripoti ya utumishi ya Agosti kutoka Huduma ya Ufalme Yetu na kuzungumzia utendaji wa mahali penu wakati wa mwezi huo. Toa maelezo kuhusu pande za utumishi wa shambani zinazohitaji kuelekezewa fikira mahali penu kama inavyoonyeshwa katika ripoti au kama ilivyoonyeshwa wakati wa ziara ya mwangalizi wa mzunguko.
Dak. 15: “Je! Wewe Unatumia Utangulizi Unaofaa?” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu. Tia moyo wote wafanyie matangulizi maendeleo. Wafanye mazoezi na wengine, wakitumia madokezo katika kitabu Reasoning. (Mnaweza kutumia habari katika Huduma ya Ufalme Yetu, Januari 1983, kurasa 6, ikiwa hamna kitabu Reasoning.) Wakati wa kuzungumzia mafungu 4-6, wahubiri wanaostahili ambao wanaweza kufuatia kwa ukaribu sana matangulizi yaliyo katika kitabu Reasoning watoe mawonyesho mafupi.
Dak. 20: “‘Haki ya Kimungu’ Mkusanyiko wa Wilaya wa 1988.” Zungumzia mafungu 1-16 ya nyongeza kwa maswali na majibu.
Wimbo 23 (50) na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA NOVEMBA 21
Wimbo 38 (67)
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Wakumbushe wote wajitayarishe kwa ajili ya kutoa ushuhuda kwa magazeti Jumamosi. Toa mawonyesho mawili mafupi, moja likionyesha Amkeni! na lingine Mnara wa Mlinzi. Chagua makala ambazo zinaweza kuvutia watu mahali penu, na tumia wahubiri ambao ni vielelezo vizuri vya kuonyesha busara na mwelekeo chanya.
Dak. 25: “‘Haki ya Kimungu’ Mkusanyiko wa Wilaya wa 1988.” Mwangalizi msimamizi azungumzia mafungu 17-29 ya nyongeza kwa maswali na majibu. Saidia akina ndugu wathamini kwamba wote kundini wanatazamiwa kuwa na mwenendo na mavazi mazuri. Maelezo yanaweza kutolewa pia kuhusu matatizo yoyote ya mahali penu kuhusiana na mkusanyiko. Zungumzia “Vikumbusho vya Mkusanyiko wa Wilaya” kadiri wakati unavyoruhusu.
Dak. 10: “Endeleza Mwelekeo wa Kutazamia Mazuri.” Hotuba ikitegemea makala katika Mnara wa Mlinzi wa Juni 1, 1986, kurasa 28-30. Fanya matumizi kulingana na hali za kwenu.
Wimbo 18 (55) na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA NOVEMBA 28
Wimbo 34 (62)
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Watie moyo wote washiriki katika utumishi wa shambani siku ya Jumamosi na Jumapili. Pitio la toleo la fasihi kwa Desemba na kutoa onyesho fupi. Kazia habari hususa kutoka kichapo kinachotolewa.
Dak. 18: Kuelimisha Ulimi Wetu Ili Uwasaidie Wenye Kuvunjika Moyo. Mambo mengi yanaelekea kuwavunja watu moyo leo: matatizo ya kiuchumi, kupoteza mpendwa katika kifo, ugonjwa, matatizo ya kiroho upande wa watoto au mwenzi, na kadhalika. Kujiachilia tushindwe na kuvunjika moyo kunatufanya tuelekee zaidi kuumizwa na mashambulizi ya Shetani. (Mit. 24:10; linganisha Luka 22:31.) Wakristo wana wajibu wa kutiana moyo na kutegemezana. (1 The. 5:14; Gal. 6:2) Kwa kufanya hivyo tunaiga Kristo. (Mt. 11:28-30) Jinsi gani? Kwa kuwa wenye huruma. (Rum. 12:15) Kwa kuwa tayari kuitikia katika njia zenye mafaa. (Yak. 2:14-17; rs kur. 117-21) Kwa kutumia kitabu Reasoning, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yanayoweza kutumiwa kuwasaidia watu katika kundi na shambani washughulike na matatizo hususa yanayoonyeshwa. Omba wasikilizaji wawili au watatu waliotayarishwa watoe maelezo wakiwa wameketi kuonyesha jinsi wengine walivyowatia moyo wakati wa uhitaji na wakati walipokabili matatizo ya kibinafsi. (Mdo. 28:15) Mkaribie Yehova, tafuta msaada wa wazee, na dumu katika sala, hivyo ukishinda kuvunjika moyo kwa mafanikio.—Yak. 4:8; Isa. 32:1, 2; Efe. 6:17, 18.
Dak. 15: Shirikiana Kikamili Na Mpango wa Funzo la Kitabu la Kundi. Hotuba ikitolewa na mwangalizi wa utumishi au kiongozi wa funzo la kitabu mwenye kustahili. Watie moyo wote washiriki katika funzo na utumishi wa shambani na kuunga kikundi mkono katika kutunza migawo kama vile usafi na kutunza Jumba la Ufalme. Toa sifa na shauri linalofaa kulingana na mastakimu ya kwenu.
Wimbo 97 (182) na sala ya kumalizia.