Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/89 uku. 2
  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • JUMA LINALOANZA JANUARI 2
  • JUMA LINALOANZA JANUARI 9
  • JUMA LINALOANZA JANUARI 16
  • JUMA LINALOANZA JANUARI 23
  • JUMA LINALOANZA JANUARI 30
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 1/89 uku. 2

Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

JUMA LINALOANZA JANUARI 2

Wimbo 111 (206)

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Kazia Toleo la Januari la kitabu chochote cha kurasa 192 kilichotangazwa kwa kupigwa chapa kabla ya 1980, kwa nusu ya bei ya kawaida. Andaa majina ya vichapo vya zamani vilivyo akibani katika kundi lenu. Zungumzia kifupi matangulizi yanayoweza kutumiwa pamoja na Kichwa cha Mazungumzo cha sasa. Katika eneo la watu wasio “Wakristo” ungeweza kusema: “Sisi tumekuja kuongea na wewe juu ya mpango mzuri ajabu alio nao Mungu kuleta baraka tele kwenye dunia hii. Unaitwa Ufalme wa Mungu. Ufalme huo utahakikisha kihalisi usalama na uhuru wa kutokuwa na hatari apa hapa duniani. Tafadhali soma pamoja nami maneno haya ya Zaburi 37:10, 11.” (Ona kitabu Reasoning, kichwa kidogo “Ufalme,” kurasa 12-13.) Pia, tia moyo kazi ya kutoa ushuhuda kwa magazeti nyumba kwa nyumba Jumamosi. Dokeza makala moja au mbili ambazo huenda zikafaa eneo lenu.

Dak. 15: “Toa Uangalifu Daima kwa Fundisho Lako.” Zungumzia mambo yenye mafaa kutoka makala katika toleo la Julai 15, 1988, la Mnara wa Mlinzi. Kazia kutumia kitabu Reasoning ili kufanyia maendeleo matangulizi, kama ilivyotajwa kwenye kurasa 16 na 17 za makala hiyo.

Dak. 18: “Kutangaza Habari Njema—Katika Eneo Linalofanyiwa Kazi Mara Nyingi.” Kutoka Huduma ya Ufalme Yetu ya 12/88. Rekebisha kulingana na mahitaji ya kundi lenu. Kazia uhitaji wa kufanyia eneo kazi kikamili na kurudia maangusho yote.

Wimbo 78 (144) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA JANUARI 9

Wimbo 112 (207)

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 20: “Je! Wewe Unatoa Sababu ya Tumaini Lililo Ndani Yako?” Mazungumzo na wonyesho. Wakati wa kuzungumzia fungu 5, panga kuwe na wonyesho mfupi ukifanywa na mhubiri anayestahili akiunganisha andiko la mwisho kutoka kwa Kichwa cha Mazungumzo na toleo la kichapo cha zamani au toleo badala lililodokezwa.

Dak. 15: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Vichapo vya Zamani.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Wakati wa kuzungumzia fungu 6, panga kuwe na wonyesho mfupi, ukionyesha toleo la sasa.

Wimbo 74 (139) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA JANUARI 16

Wimbo 48 (93)

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na matangazo yaliyochaguliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Tia ndani ripoti ya hesabu. Taja michango yoyote iliyotumwa na kundi kwa Sosaiti kwa ajili ya kazi ya Ufalme au Akiba ya Jumba la Ufalme ya Sosaiti.

Dak. 20: “Nufaika Kabisa na Mikutano ya Utumishi.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Pata maelezo mafupi kutoka kwa wasikilizaji kuhusu jinsi wao wamenufaishwa kibinafsi na Mikutano ya Utumishi.

Dak. 15: Kutumikia Mahali Ambako Uhitaji Ni Mkubwa Zaidi. Ndugu wawili wazungumzie makala “Toka Katika Bara Lako na Kutoka kwa Watu wa Ukoo Wako” katika toleo la Agosti 15, 1988 la Mnara wa Mlinzi, kurasa 21-3. Kazia uhakika wa kwamba kuna maeneo mengi katika nchi zote katika Afrika Mashariki ambako uhitaji ni mkubwa zaidi. Kazia uhitaji wa kutafuta ushauri wa wazee wa kundi lenu, kuwasiliana na Sosaiti, na kuhesabu gharama kabla ya kuondoka. (Angalia kitabu Huduma Yetu, kurasa 112-13, na Huduma ya Ufalme Yetu, Februari 1985 ukurasa 4.

Wimbo 1 (21) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA JANUARI 23

Wimbo 73 (157)

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Sanduku la Swali. Watie wote moyo washiriki katika utumishi wa shambani katika Jumamosi ya nne ya mwezi.

Dak. 18: “Vijana—Sitawisheni Uhusiano Imara Pamoja na Yehova.” Maswali na majibu. Wasihi vijana wa kundi lenu, ukiwatia moyo wazidi kufanya maendeleo kiroho.

Dak. 15: Kumsikiliza Mwalimu Mkuu. Hotuba na mahoji. Kazia thamani ya kitabu Mwalimu Mkuu (ambacho kinapatikana kwa Kiingereza katika kanda za kaseti kwa ajili ya watu wachanga.) Zile hadithi za Biblia 46 huvutia watoto na kuwafundisha kanuni za Biblia zenye umaana. Hadithi hizo husaidia kuvuta watoto kwa Yehova, Yesu Kristo, na Biblia. Fanya pitio la mambo makuu ya ujumbe kutoka kwa watangazaji wa kitabu Mwalimu Mkuu, kurasa 5-6. Hoji vijana na wazazi, ukikazia manufaa ambazo watoto wamepokea.

Wimbo 118 (205) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA JANUARI 30

Wimbo 64 (127)

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Watie moyo wote washiriki utumishi wa shambani katika siku ya magazeti. Tangaza ni vitabu vipi vya zamani vilivyo akibani vya kutolewa katika Februari. Ikiwa akiba ya vitabu vya zamani imekwisha, tumieni kitabu kingine chochote cha kurasa 192 kinachopatikana kundini kwa mchango wa kawaida. Kadiri wakati uruhusuvyo, wahubiri wasimulie maono yakikazia mafanikio ya kutoa vichapo vya zamani wakati wa Januari.

Dak. 15: “Watoto wa ‘Kuazimwa’—Zoea Hili Ni la Hekima Kadiri Gani?” Hotuba yenye kuarifu iliyo juu ya msingi wa makala katika Mnara wa Mlinzi wa Septemba 1, 1988, kurasa 28-30.

Dak. 15: Tayarisheni Mambo ya kwenu. Mwaweza kufanya pitio la mambo kutoka ziara ya mwangalizi ya karibuni.

Wimbo 5 (28) na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki