Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/89 kur. 1-2
  • Vijana—Sitawisheni Uhusiano Imara Pamoja na Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Vijana—Sitawisheni Uhusiano Imara Pamoja na Yehova
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • YALE AMBAYO LAZIMA WEWE UFANYE
  • Usafi wa Kiadili Ndio Uzuri wa Ujana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vijana—Fanyeni Maendeleo Yenu Yawe Wazi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Jizoeze Utawa Kuwa Lengo Lako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vijana—Imarisheni Tamaa Yenu ya Kumtumikia Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 1/89 kur. 1-2

Vijana—Sitawisheni Uhusiano Imara Pamoja na Yehova

1 Yakupendeza ni maneno yanayopatikana kwenye Zaburi 24:3-5: “Ni nani atakayepanda katika mlima wa BWANA [Yehova, NW]? Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake? Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, asiyeinua nafsi yake kwa ubatili, wala hakuapa kwa hila. Atapokea baraka kwa BWANA [Yehova, NW], na haki kwa Mungu wa wokovu wake.” Ndiyo, Yehova anataka katika ushirika wake wa usiri wale ambao ni safi na wasio na hatia, wale ambao hawakuwa wakiongoza maisha maradufu kwa kuapa kwa udanganyifu. Ni shangwe kuona kwamba elezo hilo linawafaa vijana Wakristo wengi sana leo. Wao ni sifa halisi kwa Yehova na tengenezo lake. Usafi wao wa kiadili huwafanya wawe wazuri machoni pa Mungu.

2 Je! ni jambo rahisi kwa vijana leo kuwa safi kiadili? Hapana. Kila siku kuna vipingamizi ambavyo lazima vikabiliwe. Kuna mweneo wa ulimwenguni pote wa mavutano machafu na mazoea ya ukosefu wa adili. Wewe unaweza kufanya nini ujihami mwenyewe? Kuna uhitaji wa kusitawisha uhusiano imara pamoja na Yehova.

YALE AMBAYO LAZIMA WEWE UFANYE

3 Kwa kuwa uhusiano imara pamoja na Yehova huhusu uthamini wa kuhisi moyoni kwa ajili ya sifa za Yehova, unahitaji kujifunza alivyo hasa. Hilo linataka funzo la bidii la Neno lake pamoja na vichapo vyenye msingi wa Biblia. Kama vile Timotheo, wewe unahitaji kulishwa “maneno ya imani, na mafundisho mazuri yale uliyoyafuata.” (1 Tim. 4:6) Funzo hilo litakusaidia kuona ‘uzuri wa Yehova.’ (Zab. 27:4) Kadiri ujifunzavyo juu yake, ndivyo utakavyovutwa karibu zaidi na yeye.

4 Kusitawisha uhusiano huo kunahitaji wakati na jitihada. Paulo alimwambia Timotheo hivi: “Uyatafakari hayo; ukae katika hayo; ili kuendelea kwako kuwe dhahiri kwa watu wote.” (1 Tim. 4:15) Ikiwa wewe hujabatizwa bado, basi fanya kazi kuelekea wakfu na ubatizo. Kwa kuwa sisi tuko karibu na mwisho wa huu mfumo, yatupasa sisi tuwe tukikaza fikira juu ya ‘yatupasa sisi kuwa watu wa namna gani katika mwenendo mtakatifu na kujitolea Mungu.’ (2 Pet. 3:11, NW) Jinsi tunavyohisi juu ya Yehova akiwa Mungu na Mpaji-Uhai wetu ni jambo la maana. Ikiwa sisi tutasitawisha uhusiano wa karibu na Yehova kama ule mmoja anapaswa kuwa nao pamoja na baba anayestahiwa na kuthaminiwa kuwa mpendwa, basi vitendo vinavyoonyesha uhusiano huo vitaonekana.—Mal. 1:6.

5 Makumi ya maelfu ya vijana wanaume na wanawake kote kote katika tengenezo wanatumia sulubu yao, nishati, na idili kushiriki katika kazi ya kuhubiri. Wao wanapatikana kwenye Jumba la Ufalme kwa ajili ya mikutano, wakiwa na moyo wa kupenda na kujitayarisha kutoa maelezo. Maelfu wanatumia nguvu zao za ujana katika utumishi wa painia. Mithali 20:29 huziita nguvu hizo zilizotumiwa vizuri “fahari ya vijana.” Ingawa kupalilia uhusiano imara wa kibinafsi pamoja na Yehova hutaka kazi ngumu katika utumishi wake, jitihada hiyo inastahili!

6 Wengi wa nyinyi wachanga mnao wazazi Wakristo ambao wamepiga ramani ya mwendo wa nyinyi kufuata. Wao wameonyesha nyinyi hatua za kufuata ili mwendelee katika njia ya uhai. Wasikilizeni wazazi wenu katika muungano pamoja na Bwana. (Efe. 6:1) Wao wanawapenda kwa kuwathamini sana na wao wanataka nyinyi mfanikiwe. Wao wanataka nyinyi mwe katika ulimwengu mpya, kwa hiyo shirikianeni nao katika vipindi vya funzo wanavyovipanga. Fanyeni ukweli uwe wenu wenyewe. Jifunzeni yote mwezayo juu ya Yehova, nanyi mtakua katika upendo kwake na kumtumikia milele.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki