Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
JUMA LINALOANZA APRILI 3
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyochaguliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Kazia mambo ya msingi katika “Jitayarishe kwa Ajili ya Pitio la Kuandika.” Tangaza mipango ya kutoa ushuhuda kama kikundi Jumamosi na Jumapili.
Dak. 15: “Wasaidie Wenye Mioyo Yenye Ufuataji Haki Watoroke Babuloni Mkubwa.” Mazungumzo kwa maswali na majibu na mwangalizi wa utumishi.
Dak. 20: Kichwa cha Mazungumzo kipya. Zungumza na wasikilizaji Maandiko yatakayotumiwa, mabadiliko kati ya Maandiko na kuingia katika toleo, na pia umuhimu wa kuonyesha upande mmoja tu au ubora unaotambulisha ibada ya kweli. Mhubiri mwenye uwezo au painia atoe onyesho la kichwa kipya kwa kutumia madokezo yanayofuata:
“Je! umeona namna nyingi tofauti-tofauti za ibada zilizopo? Ingawa hili linaonyesha kwamba mwanadamu ana uhitaji wa msingi wa kuabudu kitu fulani kilicho juu kuliko yeye mwenyewe linatokeza swali pia, Ikiwa kuna dini ya kweli, ni ipi? Biblia inaonyesha kwamba Mungu mwenyewe anaweka viwango kwa ibada ya kweli kwa kusisitiza itegemee ukweli. Angalia jinsi jambo hili limekaziwa katika Yohana 4:23, 24: (Soma, ukikazia ibada lazima itegemee ukweli.) Kwa kuwa Mungu atakubali ibada ya kweli tu, ni nini kitakachotusaidia tutambue wale wanaoabudu katika njia iliyo sawa? Hapa katika Mathayo 7:20 kuna kanuni nzuri ya kufuata: (Soma) Ungetazamia waabudu wa kweli wa Mungu watokeze matunda gani mazuri au mwenendo? Wanapasa kusema na kufanya nini? Kwa kielelezo, Biblia inasema kwamba kwapasa kuwa na masikilizano miongoni mwa washiriki wa dini ya kweli. (Soma 1 Wakorintho 1:10) Hivyo tukipata kwamba hakuna masikilizano miongoni mwa washiriki wa kikundi cha kidini, je! kweli hiyo inaweza kuwa dini ya kweli? Kwa hivyo tunapasa kutafuta kikundi cha kidini ambacho washiriki wacho wana masikilizano mmoja na mwenzake, si kugawanyika na kukosa sana masikilizano. Habari za ziada kuhusu jinsi ya kutambua dini ya kweli au wahudumu wa kweli wa Mungu zinapatikana katika toleo la Mnara wa Mlinzi, (Elekeza fikira kwenye habari iliyo wazi katika toleo ulilo nalo.”
Badala ya kutumia 1 Wakorintho 1:10 huenda ukahisi ukiwa umestarehe zaidi kutumia Yohana 13:34, 35 na ukikazia sifa ya “upendo ninyi kwa ninyi.” Au huenda ukachagua kutumia uhakika wa kwamba dini ya kweli inaheshimu na kushikilia Biblia kuwa Neno la Mungu na kuishi kulingana na mafundisho yayo na haikubali wala kuachilia kuishi kwa njia ya ukosefu wa adili. (Tito 1:16) Hakikisha kwamba unaonyesha sifa moja tu inayotambulisha dini ya kweli ukiwa mlangoni. Usijaribu kutumia yote matatu ambayo yamedokezwa hapa kwenye mlango ule ule.
Wimbo 20 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA APRILI 10
Dak. 8: Ukaribishaji wenye uchangamfu kwenye mkutano. Matangazo ya kwenu na ripoti ya hesabu. Toa maelezo kifupi kuhusu magazeti ya karibuni yanayotolewa Jumamosi hii. Mashahidi wote waliobatizwa wanapasa kufanya jitihada ya pekee kuwa kwenye Mkutano wa Utumishi juma linalofuata.
Dak. 23: “Elekezea Sana Fikira Mpango wa Kibinafsi.” Mzee apasa azungumzie makala katika nyongeza kwa mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Anapasa kuuliza maswali yenye kutumika yatakayotokeza majibu kuhusu jinsi akina ndugu wanavyoweza kutumia madokezo ili kufanyia maendeleo mpango wao wenyewe wa kibinafsi. Pia, omba mambo yaliyoonwa kuhusu yale wanayofanya ili watumie wakati wao kwa matokeo.
Dak. 14: “Kutumia Kinga Zetu Kikamili.” Mazungumzo ya habari kwa maswali na majibu na kukazia jinsi inavyotumiwa katika kundi la mahali penu.
Wimbo 136 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA APRILI 17
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 7: Hati ya Kitiba na Kadi ya Kitambulisho. Hotuba ikitolewa na mwandishi. Wape Mashahidi wote waliobatizwa kadi. Rudia kifupi mambo makuu ya barua ya Sosaiti ya Desemba 21, 1987, kwa makundi yote. Tia moyo wote wajaze kadi mara moja na kuhakikisha kwamba imetiwa sahihi na tarehe vizuri.
Dak. 18: “Tia Nguvu Upya Bidii kwa Kutumia Madokezo ya Mnara wa Mlinzi.” Mazungumzo ya maswali kwa majibu. Wakati wa kuzungumzia mafungu 4-6, rudia madokezo yaliyotolewa kwenye kurasa 16-20 katika Mnara wa Mlinzi wa Julai 15, 1988. Chagua na kukazia moja au mawili ya yale yaliyoonyeshwa katika makala ya Mnara wa Mlinzi ambayo yangekuwa yenye msaada zaidi katika eneo la kwenu. Toa onyesho kuhusu matumizi ya madokezo yaliyotolewa katika gazeti.
Dak. 12: Mahitaji ya kwenu. Au hotuba juu ya “Kwa Nini Tunapaswa Kuhofu Mungu?” ikitegemea makala katika Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1989 kurasa 29-30.
Wimbo 64 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA APRILI 24
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Toa onyesho kuhusu utoaji mfupi wa magazeti ya karibuni yatakayotolewa juma hili. Onyesha makala katika kila toleo ambalo huenda likavutia sana watu wa mahali penu. Tia moyo ushiriki katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu.
Dak. 15: “Je! Unajizoeza Mambo Uliyojifunza?” Maswali na majibu. Wasaidie akina ndugu watumie kibinafsi mambo waliyojifunza kwenye “Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya.
Dak. 20: Wasaidie Wapya na Wasiotenda. Mzee azungumzia uhitaji wa kuwasaidia wasiotenda na wengine wanaohitaji kitia-moyo. Kundi linaweza kufanya nini ili kusaidia? Kazia uhitaji wa wote kushirikiana kwa ukaribu katika kutia moyo wasiotenda na kuimarisha wengine. (Ebr. 6:1-3) Ni jambo la muhimu ikiwa tutashiriki katika ‘kutimiza kikamili huduma yetu.’ (2 Tim. 4:5, NW) Onyesha jinsi msaada unavyoweza kutolewa kupitia Funzo la Kitabu la Kundi. Angalia Index ili kupata madokezo yenye kutumika mahali penu.
Wimbo 193 na sala ya kumalizia.