Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/89 kur. 1-8
  • Tia Nguvu Upya Bidii kwa Kutumia Madokezo ya Mnara wa Mlinzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tia Nguvu Upya Bidii kwa Kutumia Madokezo ya Mnara wa Mlinzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MWITO WA USHINDANI TUNAOUKABILI
  • Watu Wenye Juhudi ya Kazi Njema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Dumisha Bidii Yako Katika Huduma
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Ukipata Matokeo, Utumie!
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Je, Utaiga Bidii ya Yehova na Yesu Katika Majira Haya ya Ukumbusho?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 4/89 kur. 1-8

Tia Nguvu Upya Bidii kwa Kutumia Madokezo ya Mnara wa Mlinzi

1 Kristo Yesu ni kielelezo kikamilifu cha mhubiri wa habari njema mwenye bidii. Tamaa yake ya moyo wenye bidii ya kufanya mapenzi ya Baba yake na kupendezwa kwake sana na watu kulimsukuma aonyeshe wengine hangaiko la kibinafsi. Huduma yake ilikuwa yenye kusisimua, naye alipata matokeo. Huduma ilimburudisha. Yeye aliiona kuwa “chakula” kilichomtegemeza. (Yoh. 4:34) Aliwatolea wengine maneno ya wokovu huku akitimiza kazi ambayo Baba yake alimwagiza aifanye. Hii ilitoa maana na kusudi kwa maisha yake.

2 Mitume na wafuasi wengine wa Kristo Yesu wa karne ya kwanza waliiga bidii yake katika huduma. Ingawa nyakati nyingine walinyanyaswa vikali, bidii yao haingeweza kupunguzwa. (Mdo. 5:28-32; 8:1, 4) Ndivyo ilivyo leo. Habari njema zinahubiriwa karibu katika kila pembe ya dunia na watu mmoja mmoja ambao wanafuata kielelezo cha Yesu Kristo. Wakiwa Mashahidi wa Yehova, wao wana “juhudi katika matendo mema” daima.—Tito 2:14.

3 Tukikosa bidii, kazi yetu inakuwa yenye uzembe, na kujihusisha kwetu kibinafsi kunakuwa kwa kijuu-juu. Tokeo ni kwamba, huenda tusipate shangwe tena katika utumishi wetu. Tukipata kwamba tumo katika hali hii, tunahitaji kutafuta njia za kutia upya nguvu bidii yetu na kukubali mwito wa ushindani ambao huduma ya shambani inatokeza. Makala ya Mnara wa Mlinzi wa Julai 15, 1988 yenye kichwa “Toa Uangalifu Daima kwa Fundisho Lako” ilikazia madokezo yenye kutumika ya kutusaidia tuimarishe au tutie upya nguvu bidii yetu katika utumishi wa Ufalme.

MWITO WA USHINDANI TUNAOUKABILI

4 Katika sehemu nyingi za ulimwengu, kuna eneo dogo sana ambalo ni jipya au linafanyiwa kazi mara chache. Katika maeneo ya miji mikubwa, si jambo lisilo la kawaida kwa makundi kufanyia eneo lao kazi mara moja kwa mwezi au hata mara moja kwa juma. Hii inaweza kutokeza mwito wa ushindani kwa sababu wenye nyumba wengi tayari wanajua sisi ni nani na mara nyingi wanajaribu kukomesha mazungumzo kabla hatujafanya utoaji. Labda wanalalamika kwamba ‘Shahidi alikuwa hapa juma lililopita tu.’ Majirani wetu wengi hawamo nyumbani, au tunaweza kupata kwamba watu waliomo katika eneo letu ni wenye ubaridi. Mambo yote haya yanaweza kuwa yenye kuvunja moyo. Lakini je! umetumia madokezo yaliyotolewa kwenye kurasa 4-7 za makala ya gazeti la Mnara wa Mlinzi lililotajwa juu?

5 Tayari mamilioni wamekusanywa katika “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine,” na mamilioni zaidi wanaendelea kuitikia habari njema za Ufalme. (Ufu. 7:9; Yoh. 10:16) Hata hivyo, huenda utoaji uliokuwa wenye matokeo wakati uliopita usiamshe kupendezwa katike maeneo yetu. Tunahitaji kuwa macho kuhusu aina, ubora, na matokeo ya utoaji wetu na kuwa tayari kufanya marekebisho yanayohitajiwa sana.

6 Ukizungumzia habari hii, Mnara wa Mlinzi ulitoa mapendekezo fulani yenye kupendeza kuhusu jinsi ya kufanyia huduma yetu maendeleo. Ulidokeza njia za kutoa ushuhuda kamili tunapohitajiwa kushughulika na ubaridi, pamoja na watu waliomo katika maeneo yaliyofanyiwa kazi mara nyingi, na pamoja na wenye nyumba wanaolalamika. Je! tunatumia madokezo haya, tukirekebisha utoaji wetu ulingane na mahitaji ya eneo? Je! tunatumia kwa faida vyombo vinavyopatikana kwetu ili kufanya hivyo? Kufuata madokezo yaliyotolewa kutatusaidia tujihusishe zaidi katika huduma. Tunapotia ndani kimakusudi yale ambayo yameonyeshwa, tunachochewa kiakili na kushughulishwa na huduma. Hivyo, bidii yetu inatiwa nguvu upya na kuzidishwa.

7 Kwa sababu ya hali za sasa za ulimwengu, ni wazi kabisa kwamba dhiki kubwa inakaribia zaidi. Hii inaonyesha uharaka wa ujumbe wetu na uhitaji wa kuangaza kama ‘nuru ya ulimwengu.’ (Mt. 5:14, 16) Acheni tuwe wenye juhudi katika kutumia madokezo ambayo tumepokea na hivyo tuzidishe bidii yetu kwa ajili ya huduma.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki